Serikali: Kila Mtanzania mwenye umri wa zaidi ya miaka 18 na mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi

Serikali: Kila Mtanzania mwenye umri wa zaidi ya miaka 18 na mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi

Hivi hii nchi mbona tuna makodi mengi sana jamani na yanaumiza kweli kweli ila serikali bado hairidhiki tu?

Shida hapa ni ukusanyaji wa kodi ambao hauna ubunifu ndani yake unaacha mianya ya ukwepaji mingi sana na pia kwenye matumizi yamekuwa makubwa tena ambayo si ya maendeleo ndio maana wanaona kodi tunazolipa hazitoshi wanaleta tena zingine. Hawa watu tuliowapa dhamana hawatufai maana wanaichonganisha serikali yetu na wananchi wake badala wajikite katika kupunguza matumizi yasiyo ya kimaendeleo hilo hawana habari nalo sababu linawanufaisha wao na familia zao wanakaa kubuni kero kwa wananchi.

Watanzania tunachezewa sana ila tuwakatae hawa watu ni hatari sana. Hawa ni wahuni tu kama walivyo wahuni wengine.
 
wafanyakazi wote wa umma na sekta binafsi wanalipa kodi wanaponunua bidhaa lakini wanalipa kodi kwa kukatwa kwenye mishahara yao. Hii ilikuwa substandard, wafanyakazi wa umma walikuwa wakilipa kodi kuliko wananchi wengine mfano mkulima, mfugaji, mfanyabiashara nk
Wafanya Kazi wao si wana mapato rasmi...kwani sisi mkitupatia kazi serikalini tutakataa?..tupeni kazi mkate kodi hatuta nongwa mbona.

Na pia wana marupurupu mengi pamoja na fursa hata za kukopa...kila Bank au Microfinance kipaumbele chao ni Wafanya Kazi haswa wa Seriklali.

Sasa sisi Kajambanani ukifikiria kwa kuupata Mtaji kichwa kinataka kupasuka maana kila unapopeleka miguu wanakufurusha, hakuna Bank wala Taasisi ya fedha inakusikiliza, ukirudi Mtaani unaambie ucheze kamari upate mtaji.

Na hao Wakulima, Wafugaji, Wafanyabiashara n.k kwani wamekuwa hawalipi kodi?..ni kodi gani tena mnatamani wakatwe nje ya mfumo rasmi?.
 
Wafanya Kazi wao si wana mapato rasmi...kwani sisi mkitupatia kazi serikalini tutakataa?..tupeni kazi mkate kodi hatuta nongwa mbona.

Na pia wana marupurupu mengi pamoja na fursa hata za kukopa...kila Bank au Microfinance kipaumbele chao ni Wafanya Kazi haswa wa Seriklali.

Sasa sisi Kajambanani ukifikiria kwa kuupata Mtaji kichwa kinataka kupasuka maana kila unapopeleka miguu wanakufurusha, hakuna Bank wala Taasisi ya fedha inakusikiliza, ukirudi Mtaani unaambie ucheze kamari upate mtaji.

Na hao Wakulima, Wafugaji, Wafanyabiashara n.k kwani wamekuwa hawalipi kodi?..ni kodi gani tena mnatamani wakatwe nje ya mfumo rasmi?.
ukweli ni kwamba serikali haiwezi kuajiri wananchi wote, na tukumbuke hamna mfanyakazi wa umma au wa binafsi bilionea
 
Juzi Kati nimeenda ku-renew leseni ya biashara nimeandaa 52k niliyozoea, nafika naambiwa eti kuna upuuzi mwingine umeongezeka inaitwa service levy. Kwahiyo itakuwa jumla 77k (52+25 k)


Sijui ni national wide, sijui ni halmashauri yetu!!

Upuuzi!!!!
Kote ni hivyohivyo na unatakiwa kupeleka return kila mwezi halmashauri ili ulipie service levy bila hivyo mwakani hawakupi leseni, watakwambia lete mahesabu yako ya mwaka mzima ili tukate service levy yetu.
 
Hii naona imekaa sawa wafanyabiashara wanaotambulika wanaonewa sana, nadhani mapato yakiwepo ya kutosha wafanyabiashara nao watapumua, mfano angalia anayelipa VAT anavyonyanyasika.
 
View attachment 2261264

"Kila mtanzania mwenye umri wa zaidi ya miaka 18 na mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi. Ili kutimiza amza hiyo, Serikali inakusudia kutoa namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) kwa kila mtanzania mwenye umri wa kuanzia miaka 18 au zaidi"

"Kwa kuwa utaratibu wa usajili wa namba ya utambulisho wa Taifa (NIDA) unamtaka kila mwananchi mwenye umri wa miaka 18 au zaidi kujisajili NIDA, napendekeza kuwa wale wote wenye NIDA kwa sasa (wanaofikia milioni 19 nchi nzima) wapatiwe namba ya TIN na itumike kwenye miamala yote inayofanyika katika ununuzi na mauzo yanayofanyika ndani ya nchi"
"Kila mwenye namba ya mlipakodi atapata makadirio yake kwa njia ya simu na kulipa kodi husika kwa njia ya mtandao"

- @mwigulunchemba ,Waziri wa Fedha na Mipango

#BajetiKuu
Kama hutaki, hamia Burundi! hamia Burundi! hamia Burundi!!!
 
Back
Top Bottom