Serikali Kufanya Marekebisho ya Sheria za Barabarani Ili Kukabiliana Ipasavyo na Ajali za Barabarani

Serikali Kufanya Marekebisho ya Sheria za Barabarani Ili Kukabiliana Ipasavyo na Ajali za Barabarani

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301


Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa, Mhe. Amina Ali Mzee; Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Daniel Sillo amesema Serikali iko hatua za mwishoni kuleta Muswada wa Sheria Bungeni ili ifanyiwe marekebisho kwa lengo la kukabiliana na ajali za Barabarani zinazosababishwa na Madereva wazembe.

"Je, lini Serikali itaanza kuweka Sheria na Utaratibu mzuri wa kupunguza ajali za barabarani zinazotokana na uzembe wa Madereva" - Mhe. Amina Ali Mzee, Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa

"Jeshi la Polisi kupitia kikosi cha Usalama Barabarani kwasasa kinasimamia masuala ya Usalama Barabarani kwa kutumia Sheria ya Usalama Barabarani Sura 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002 katika mkakati wa Kuboresha Sheria hii ili kupunguza ajali za Barabarani, Serikali imekusanya maoni kutoka kwa wadau na sasa inamalizia kuyafanyia kazi na baada ya hapo itawasilisha Muswada wa Sheria Bungeni" - Mhe. Daniel Sillo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

"Je, ni hatua zipi zinazochukuliwa na Serikali kuwadhibiti Madereva wazembe? Serikali haioni sasa iko haja ya kuhakikisha Sheria hii inakuja Bungeni ili kudhibiti ajali za Barabarani?" - Mhe. Amina Ali Mzee, Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa.

Soma Pia: Tatizo la Ajali za Barabarani Litatumaliza Watanzania, Je Kweli Serikali Haiwezi Kufanya Kitu?

WhatsApp Image 2024-11-06 at 13.54.33.jpeg

"Hatua stahiki ya kwanza kwa Madereva wazembe ni kuwafutia leseni kwa Dereva anayeendesha gari kwa uzembe na kusababisha ajali. Pili, ni kumfikisha Mahakamani na ikithibitika ni kufungwa Jela . Tatu, ni kulipa faini"

"Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ajali za Barabarani ama zinapungua ama zinakwisha kabisa. Tumekusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali, lengo ni kuhakikisha tunarekebisha Sheria"

nida-pic.jpg
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-11-06 at 13.58.16.jpeg
    WhatsApp Image 2024-11-06 at 13.58.16.jpeg
    352.4 KB · Views: 3
Moja ya kusababisha vikuuu vya ajali za barabara ni ufinyu/ wembamba wa barabara. Sijawahi kuelewa ni kwa nini miaka 60 baada ya kupata uhuru tumeshindwa kuwa na walau barabara zenye njia 3 (three lanes roads) kwenye barabara kuu zote mfano dar -Tunduma, Dar -Arusha, dar -Mwanza nk.... Sababu/chanzo cha pili cha uzembe wa madereva (unaosababishwa na ulevi, uendeshaji mbovu , kutozingatia sheria za barabarani ni) dawa yake ni moja tuu kuanzisha mamlaka kamili ya usalama barabarani, hawa wawezeshwe ili barabara zote waweke CCTV camera, kuwe na check points za kusimamisha gari zilizovunja sheria (ziwekwe CCTV pia). Jeshi la polisi lihusike tuu kuongeza nguvu kama itahitajika...
 
Toa matuta! Toa na wale wapenda rushwa wote barabarani! Weka kamera za usalama! Weka 70/KPH badala ya 50/KPH ya toka enzi za Mkoloni!

Piga marufuku wale jamaa wenye nguo nyeupe kama sanda, kutembea na mashine za kutafutia tozo kwa nguvu! Weka check point chache, na watakaopata bahati ya kuwepo kwenye hizo check points, wavishwe makoti maalum yenye camera.
 
Back
Top Bottom