Serikali Kujenga Barabara ya Musoma - Makojo - Busekera 2023/2024

Serikali Kujenga Barabara ya Musoma - Makojo - Busekera 2023/2024

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

SERIKALI KUJENGA BARABARA YA MUSOMA-MAKOJO-BUSEKERA KWA AWAMU MBILI
(Bajeti ya Wizara ya Ujenzi & Uchukuzi, 2023/2024)

Urefu wa barabara Kilomita 92

Sehemu zenye lami Musoma Mjini-Buhare: km 5.9 (Eneo lote hili liko ndani ya Manispaa ya Mji wa Musoma)

Kusenyi-Kwikonero: km 5 (Eneo lote hili liko Musoma Vijijini)

BAJETI YA MWAKA 2023/2024; Barabara letu limepewa KM 40 (Kilomita Arobaini, Awamu I)

Wananchi na Viongozi wote wa Chama na Serikali wa Jimbo la Musoma Vijijini wanaishukuru sana SERIKALI yetu kufanya maamuzi mazuri ya kukamilisha ujenzi wa barabara hili (Musoma-Makojo-Busekera) kwa awamu mbili. Ahsante sana Rais wetu, Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kusikiliza kilio chetu cha miaka mingi na hatimae kuamua kutatatua tatizo hili sugu. Tunashukuru sana!

AWAMU I (40 km)
Ujenzi wa barabara hili ulishaanza kwa kujenga KILOMITA 5 kuanzia Kijiji cha Kusenyi kuelekea Kijiji cha Makojo hadi Kijijini Busekera (mwisho wa barabara)

Ujenzi wa km 40 uendelee kwa mpangillio huo huo, yaani, kuanzia Kitongoji cha Kwikonero (Kijiji cha Suguti) kuelekea Kijijini Busekera - tusiache vipande vipande!

AWAMU II (km 40+)
Ujenzi utaanzia Kijijini Kusenyi kuelekea Musoma Mjini

USHAURI:
Achukuliwe Mkandarasi mzoefu, na anayejitosheleza kwenye vifaa vya ujenzi

Ujenzi uanze haraka baada ya Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2023/2024 kuanza kutumika, yaani tarehe 1.7.2023.

Usisahau kutembelea TOVUTI ya Jimbo letu ambayo ni:
www.musomavijijini.or.tz

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumanne, 23.5.2023
 
Back
Top Bottom