Serikali kuleta ndege mpya nchini Machi 26, 2024

Serikali kuleta ndege mpya nchini Machi 26, 2024

Badala ya kuendelea kuwa na mawazo au fikra potofu kila wakati za kununua ndege mpya kutoka ktk viwanda vya nchi za nje, nadhani umefika wakati sasa wa kufikiria kuwa na kiwanda au viwanda vyetu weyewe vya kuunda ndege hapa hapa nchini kwetu Tanzania. Tuwe na wazo kama hili, hata kama sisi wenyewe bado akili zetu hazijawa kubwa kuweza kuwa na viwanda vya namna hii, basi tuanze hata kwa kuwakaribisha wawekezaji kutoka nje ya nchi, tunaweza kuingia nao mikataba maalumu ya uwekezaji wa namna hii. Viongozi wa nchi hii wawe na Maono Mapana ili wayaone haya mambo mazuri kwa mustakabali mwema wa nchi hii.
Kiwanda kipo moro mkuu
 
hivi tungekuwa tumeorder ndege 500 si kila siku tungekuwa tunafanya mapokezi. hakuna kazi zengine za kufanya?.
alafu sio hiyo hayo tu yani hata kibarabara au kidaraja nayo inatengwa siku kuzinduliwa.

tutaacha lini
 
Tupunguziwe na nauli, sisi wakulima tusafirishe mazao yetu kwa bei nafuu
 
Hizo zinanunuliwa maalum kwa ajili ya kuzikamatisha ili walipwe madeni wanayojishtaki wenyewe ICSID
 
Kama hiyo ndege imenunuliwa kwa faida iliyotokana na kuendesha ndege zilizopo,hiyo ni hatua kubwa kimaendeleo.
 
hii si kama ile iliyomwaga watu Ethiopia,rubani akiweka autopilot inavurugwa haielewi somo inarudi chini?
 
Nchi inaendeshwa kama gari bovu. @ATCL watuambie ilipo ndege aina ya Boeing 787-8(5H-TCJ) ni kwa nini haifanyi kazi tangu August 2023. na kama kweli ilinunuliwa mpya.
Hapo chini inaonekana Baiyun China ikiwa na hitilafu za kiufundi labda inatengenezwa Malaysia.
Hivi kweli tuna utashi wa kuendesha kampuni ya ndege ya taifa hili kiushindani au ni kwa ajili ya matanuzi ya viongozi?😳
Kesho tunatangaziwa kupokea ndege nyingine ambayo aina yake ina utata hata huko inakotengenezwa....
 

Attachments

  • Screenshot_25-3-2024_231314_www.jetphotos.com.jpeg
    Screenshot_25-3-2024_231314_www.jetphotos.com.jpeg
    385.7 KB · Views: 1
Back
Top Bottom