Serikali kutolipa mishahara watumishi kwa kisingizio cha kutojaza majukumu yao kwenye mfumo wa ESS ni unyang'anyi usiotumia Silaha

Ujazaji wa taarifa ni majukumu ya HR wao walikuwa wanahakikisha watu wanajaza, HR department ndio ilikuwa inafanya enforcement kupitia wakuu wa vitengo .

Wakuu za vitengo ,managers wanahakikisha watu wanajaza na kutoa maelekezo kwa sababu wao ndio masupervisors hata account zao ni special...Hao ndio wazembe kwa kwanza mpaka kufika trh ya ukomo walitakiwa kujua watu waliopo chini yao kama wametekeleza zoezi.

Kama zoezi dogo la mara moja unashindwa ,je wataweza ku'manage watu kila siku kweny majukumu yao.
 
Ni suala la ustahimilivu na subra tu, bilashaka iko namna inafanyika kitatua changamoto hiyo mpya na hizo nyingine ulizozitaja kwa wakati muafaka 🐒
 
Serikali ya awamu ya Sita iliachana na mfumo wa kujaza OPRASS kwenye makaratasi (nakala ngumu) badala yake ikatambulisha PEPMIS kupitia mfumo Employee Self Service kwa kifupi ESS.
Huu mfumo ni mzuri, kuzuia mchwa na wafanyakazi hewa kuendelea kula mshahara,
Tatizo la watumishi wa umma, ni wavivu,wabadhirifu, sekta binafsi kuna hiyo mifumo kwa miaka mingi sana, fateni u taratibu,
 
I think, respective institutions which are responsible on the matter are learning very closely, from these public opinions, constructive and deconstructive criticisms so that to avoid confusions like this one next time
 
Ukishajisajili unapewa section na Afisa Utumishi ili Mkuu wako akuoe Role (Activity) then wewe utaweka Sub Activity

Lakini kwa Sasa ukiwa Mtumishi hivo sub activity inagoma ila unatakiwa upewe Section then wewe mwenyewe uweke Task na Sub Task

Hii ya Task na Sub Task ipo kwa Maafisa Watendaji na wengi wao wapo kwenye section ya Administratio.
Utakachokifanya unajaza Task na Sub Task then una submit Kila sub task kwa Mkuu wako yeye ana approve

Huko kwenye loan sijaingia ila nakushauru usije ukafanya top up jibane bane hadi mkopo wako uishi, kwenye top up upigaji ni mkubwa sana kuliko kawaida
 
Kuna uzembe wa mtu mmoja mmoja , boss na taasis kwa ujumla.
Mfano ukishajili hujui km kunapewa Role, anayetakiwa kukupa Role ni Mkuu wa Idara au Kitengo , Sasa watumishi wengi waliambiwa TU wajisajili basi.
Hapo kama hawakuambiwa kinachofuata baada ya kujisajili ni shida,inatakiwa waanze kutolipwa hiyo mishahara hao walioshindwa kulisimamia hilo zoezi kikamilifu.

Huku nilipo DED hakuingiziwa mshahara wake mwezi uliopita kwa kushindwa kukamilisha zoezi hili kwa watumishi wa chini yake.
 
Wagonjwa wa muda mrefu,walio masomoni kuna utaratibu unafanywa,hawanyimwi mishahara yao
 
Namaanisha kwamba kama unaona kuna jambo la msingi na la lazima unatakiwa kulifanya kwann usubir mpaka Point ya kukatwa mshahara ndipo uchukue hatua.! Yn upo sehemu hakuna internet, kwann Siku ya off yako usiende mjini kwa ajili ya jambo moja tuu kwamba naenda kuweka mambo yangu sawa huko kwenye system.?
 
Mzee, unajisikia lakini au uko kukaza fuvu tu?

Kuna watu wanafanya utumishi wa umma, wako mazingira bora kabisa ya kazi, marupurupu yao ni zaidi ya mishahara ya wengi kwenye utumishi huo huo wa umma; anapewa nyumba nzuri, anapewa usafiri, anapewa mawasiliano, n.k ili aweze kutimiza majukumu yake....


Wapo wanaokaa bungeni kule, tangu nchi iundwe hakuna la maana walilowahi kufanya, bado kutimiza majukumu yao, wanalipwa kwa siku nje ya mshahara na marupurupu yote.

Unataka afisa kilimo aliyeko Nanjilinji huko, anayelipwa mshahara wa 700,000 tu kabla ya kodi, anayetumia siku 3 kuufuata mshahara mjini kwa gharama zake mwenyewe, akitumia nauli chungu tele, aende kutafuta internet kwa gharama zake? Kwa upuuzi usio na tija?
  • Mkongo wenu wa taifa umeishia wapi?
  • Kutengeneza madawati tu mmeshindwa, unataka mtumishi aitafute internet isipokuwepo?
  • Mnaanzisha mifumo, mmetoa vitendea kazi?

Hakuna asiyelipwa na serikali kama ni mtumishi wa umma, unaweza thibitisha kuwa kuanzia namba 1 mpaka messenger wa Halmashauri kule, wote wanapaswa kujaza hizo mambo?
  • Na kama sio, kwanini?
  • Na kama ndio, wote wana abide kiasi cha kusema, wakurugenzi na makatibu wakuu waliokosa kufanya hivyo wamenyimwa mishahara?

Natumia nguvu kubwa kukusanya upepo nadhani....si ajabu najadili na sisiemu!
 
Huenda si unyang'anyi ,nali kudhibiti wahuni ambao wamekuwa wanaliowa mishahala zaidi ya mmoja ikihali mtu ni mmoja.

Unajua nchi yetu kila mtu anatamani kuwa mpigaji ,yaani uzalendo ni tabu inchi
 
Nimekaza fuvu
 
Sasa kujaza tu task au sub task unashindwa.?

Kazi ya serikali unafanyaje??

Uzembe tu,
 
Mi kama aliyejenga vituo vya mwrndokadi hakufikiria kama mabus Yale watapanda wazee na wslemavu.Ni mwendo wa wenye nguv tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…