Serikali kuzima Mitambo yote ya TANESCO inayotumia mafuta mazito kufikia mwaka 2020: Ni baada ya kukamilika kwa Mradi wa Stiegler's Gorge

Serikali kuzima Mitambo yote ya TANESCO inayotumia mafuta mazito kufikia mwaka 2020: Ni baada ya kukamilika kwa Mradi wa Stiegler's Gorge

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2017
Posts
2,869
Reaction score
3,187
IMG_7744.JPG

Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, akiwa mkoani Njombe, ameahidi kuwa, Serikali inatafajia kuzima mitambo yote ya TANESCO, inayotumia mafuta mazito baada ya kukamilika kwa Mradi wa Stiegler's Gorge ifikapo mwaka 2020.

Dk. Kalemani alieleza kuwa, umeme wa mafuta mazito ni wa gharama kubwa ndiyo maana Serikali inapambana kuhakikisha Mradi wa kuzalisha umeme wa Rufiji unakamilika haraka kama ilivyokusudiwa.

"Tulifanikiwa kuzima vituo vichache mwaka jana ikiwemo mitambo ya IPTL na kuacha mitambo ya Simbion na Agreco, lengo ni kupunguza matumizi ya uendeshaji wa TANESCO ambayo yalikuwa ni makubwa na tumefanikiwa kwa asilimia chache Shirika kuweza kujiendesha."

Mradi wa Stiegler's Gorge utazalisha MW 2,100 kwenye Gridi ya Taifa. Vilevile, utaongeza kilimo cha umeagiliaji kwa maeneo yaliyoko pembezoni mwa Mradi huo. Aidha, utaongeza utalii na kutoa ajira zaidi ya 1,500 wakati wa ujenzi na 500 wataajiriwa.

IMG_7745.JPG


IMG_7743.JPG
 
2020?
Huyu Waziri anatania au anafikiri kujenga huu mradi ni kama kufyeka pori?
Nategemea mradi kuchukua miaka 5~10.
Ndio tatizo la kuingiza siasa kila mahali, Hydro ya kiwango cha Stiegler's Gorge miaka miwili.
 
Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, akiwa mkoani Njombe, ameahidi kuwa, Serikali inatafajia kuzima mitambo yote ya TANESCO, inayotumia mafuta mazito baada ya kukamilika kwa Mradi wa Stiegler's Gorge ifikapo mwaka 2020.

Leo ni September 2018, 2020 ni miezi 16 ijayo. Huu utakuwa muujiza wa dunia 😵😀😀😀😛😛😛 LoL
 
Leo ni September 2018, 2020 ni miezi 16 ijayo. Huu utakuwa muujiza wa dunia 😵😀😀😀😛😛😛LoL
Mnasema kweli. Miradi ya HEP huwa siyo ya kitoto kwani inahusisha engineering ya hali ya juu. Nikiangalia Grand Renaissance ya Ethiopia ilivyochukua miaka mingi, ni ngumu kuona Stiegler's Gorge ikikamilika mwaka 2020.
Muhimu tuna-recommend jitihada kubwa ya Serikali kuwa, inataka kuujenga Mradi huo. Mambo ya lini utakamilika kwangu mimi siyo ishu at all.
 
Nami nafahamu fika kuwa huo mradi hauwezi kukamilika kwa miezi 18 ilahali hata source of funding is not certain.

Hii inaweza kuja kuwa kama ile hadithi ya makinikia ambayo ili-involve kamba kibao wakati kumbe tumeshaburuzwa kwenye International Court of Arbitration tukisubiri kulizwa....!!!

Hii miradi inayoendeshwa na Political Gerrymandering than Economic Sense mara nyingi huishia kubaki magofu kwa kukosa wawekezaji.
 
Mnasema kweli. Miradi ya HEP huwa siyo ya kitoto kwani inahusisha engineering ya hali ya juu. Nikiangalia Grand Renaissance ya Ethiopia ilivyochukua miaka mingi, ni ngumu kuona Stiegler's Gorge ikikamilika mwaka 2020.
Muhimu tuna-recommend jitihada kubwa ya Serikali kuwa, inataka kuujenga Mradi huo. Mambo ya lini utakamilika kwangu mimi siyo ishu at all.
Wewe jamaa ndio Chahali alikufananisha na nani sijui ? Ule msiba hauwezi kuwa na akili hizi

Asalalee!
 
Yalishasemwa mengi sana kuhusiana na kuondoa tatizo la Umeme Tz ila hakuna lililotimia je huu utakuwa ni muujiza?!
 
Leo ni September 2018, 2020 ni miezi 16 ijayo. Huu utakuwa muujiza wa dunia 😵😀😀😀😛😛😛LoL
Tanzania ni nchi ya miujiza ......... kila siku kuna muujiza unajitokeza!!

Kama daraja la Tazara tu wameshindwa kulijenga ndani ya miezi 16 ...........!!
 
View attachment 856424

Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, akiwa mkoani Njombe, ameahidi kuwa, Serikali inatafajia kuzima mitambo yote ya TANESCO, inayotumia mafuta mazito baada ya kukamilika kwa Mradi wa Stiegler's Gorge ifikapo mwaka 2020.
Dk. Kalemani alieleza kuwa, umeme wa mafuta mazito ni wa gharama kubwa ndiyo maana Serikali inapambana kuhakikisha Mradi wa kuzalisha umeme wa Rufiji unakamilika haraka kama ilivyokusudiwa.
"Tulifanikiwa kuzima vituo vichache mwaka jana ikiwemo mitambo ya IPTL na kuacha mitambo ya Simbion na Agreco, lengo ni kupunguza matumizi ya uendeshaji wa TANESCO ambayo yalikuwa ni makubwa na tumefanikiwa kwa asilimia chache Shirika kuweza kujiendesha."
Mradi wa Stiegler's Gorge utazalisha MW 2,100 kwenye Gridi ya Taifa. Vilevile, utaongeza kilimo cha umeagiliaji kwa maeneo yaliyoko pembezoni mwa Mradi huo. Aidha, utaongeza utalii na kutoa ajira zaidi ya 1,500 wakati wa ujenzi na 500 wataajiriwa.

View attachment 856426

View attachment 856423
Stiegler's Gorge kuanza kuzalisha umeme 2020 ni ndoto za mchana!
 
Waziri umesahau kuwa hayo mafuta mazito HFO sio gharama ukilinganisha na Diesel.Tanzania inazo Hydrcarbon yaani mafuta ghafi na gesi asilia.
Weka ushujaa kwanza,acha kuuza vitaru,chimba mafuta na gesi mwenyewe hayo mazao yake yatakuwa nafuu,usisahau kujenga au kufufua Refiney ya Kigamboni.
Acha story weka majibu ya miradi ya mafuta na gesi mezani.Ikiwa umezidiwa karibu Texas upate somo bila chenga.
 
Waziri umesahau kuwa hayo mafuta mazito HFO sio gharama ukilinganisha na Diesel.Tanzania inazo Hydrcarbon yaani mafuta ghafi na gesi asilia.
Weka ushujaa kwanza,acha kuuza vitaru,chimba mafuta na gesi mwenyewe hayo mazao yake yatakuwa nafuu,usisahau kujenga au kufufua Refiney ya Kigamboni.
Acha story weka majibu ya miradi ya mafuta na gesi mezani.Ikiwa umezidiwa karibu Texas upate somo bila chenga.


Kuna mwanafalsafa sikumbuki ni nani alisema " unaweza kuwadanganya watu wote kwa wakati fulani, na unaweza kuwadanganya watu fulani wakati wote, lakini haiwezekani kuwadanganya watu wote wakati wote"
Hapa naona kiongozi anashughulika na kipande kimja cha hiyo nukuuzi.
 
Umeme wa Gesi u umeishia wapi kwani?
 
Huyu jamaa ni muongo ndio maana harefuki. miradi tubya REA3 ya kupanda nguzo na kuweka nyaya inawashinda , sasa ndo ije stiglers.
Nasema hivi Magufuli anaondoka mandarakani stiglers haijafika hata nusu. HEPs are major and extreme project, Kihansi MW 200 imechukua miaka 13. Hiyo stiglers kama una kila kitu resources and time unaweza kukamilisha c chini ya miaka 12. Hapo tu hata mtu wa kufyeka misitu wamekosa, siasa ushenzi na uongo
 
TANZANIA NCHI YA AJABU, WATAALAMU WALIPOWASHAURI KUWA UANZISHAJI WA MRADI HUU UTAHARIBU MAZINGIRA MLIWAJIBU KUWA INYESHE MVUA LIWAKE JUA LAZIMA MRADI UANZISHWE. LEO WAKENYA WANATAKA KUANZISHA MRADI KAMA HUO HUKO KWAO, WAZIRI WA TANZANIA ANALALAMIKA KUWA MRADI UTAHARIBU MAZINGIRA
 
Back
Top Bottom