Serikali lazima mjue matajiri nasi tuna haki kama Watanzania wengine

Serikali lazima mjue matajiri nasi tuna haki kama Watanzania wengine

CreativityCode

Senior Member
Joined
Aug 8, 2020
Posts
158
Reaction score
653
Shalom from Jerusalem.

Mara nyingi viongozi wa serikali mmesikika mkisema na kuona fahari kuwa mko kwa ajili ya kuwatumikia wanyonge kama vile wao pekee ndiyo wenye haki ya kuishi.

Pia mmekuwa mkifanya propaganda kuionesha jamii unyonge wa watu wengi unasababishwa na sisi matajiri.

Mnaanzisha vitendo vya kuhujumu biashara zetu matajiri ili kupata uungwaji mkono na hao wanyonge wenu.


Napenda kuwakumbusha kuwa utajiri wetu unatokana na akili zetu za kubuni biashara zinazotuingizia fedha pia kufanya kazi kwa jasho na damu usiku na mchana.

Tunawekeza nchini. Tunatoa ajira kwa watu wengi na hivyo kustawisha jamii.

Miaka yote mmetubagua sana na kutuumiza kwa kupandisha kodi bila kuzingatia faida tuipatayo na kusababisha wengine tufunge biashara.

Hii si sawa. Badilikeni.

Nasi ni watanzania tunastahili heshima.

Kwa mujibu wa katiba nyie ni viongozi wa watanzania wote, matajiri na masikini, wenye nguvu na wanyonge hivyo tumikieni watu kwa usawa kwa mujibu wa sheria.

Angalizo:

Ni fahari na baraka kuwa tajiri.

Unyonge na umasikini ni laana
 
Una utajiri gani wakuja kupiga kelele hapa JF?
Dogo, sisi matajiri wakubwa tukiwa mtaani au maofisini hatuwezi kujifyatua, kujichomoa akili wala kujitia wazimu. Tuna heshimika na vioo kwa jamii huko mtaani.

Sehemu pekee ya kujifyatua na kujichomoa akili ni humu JamiiForums ili tuweze kuishi kama raia wengine. [emoji3]

Tupo wengi kama kina Zero IQ,Asprin,Kanungila Karim,Mwifwa na Frank Wanjiru

Magonjwa Mtambuka huyu alifilisika hela zake zote kwasababu ya kuendekeza kucheza kamali, wanawake wa kununua, pamoja na siasa. Akaishia kupata msongo wa mawazo na kuingia kwenye ulevi.
 
Dogo, sisi matajiri wakubwa tukiwa mtaani au maofisini hatuwezi kujifyatua wala kujichomoa akili wala kujitia wazimu. Tuna heshimika na vioo kwa jamii huko mtaani.

Sehemu pekee ya kujifyatua na kujichomoa akili ni humu JamiiForums ili tuweze kuishi kama raia wengine. [emoji3]
Hahahahaha yani matajiri wa jf bhana, kwahiyo mnataka haki sawa sawa na wanyonge?
 
Kama nyinyi ni matajiri, basi mnauwezo wa kutumia utajiri wenu kujitetea na kupata haki zenu. Mnyonge hana uwezo wa kujitetea, anabaki kudhulumiwa haki yake na kupoteza utu wake.
 
Tajiri hawezi ku text msahafu wote huo. Yumkini una kibanda CHA kuuzia Vijana wetu pale kona ya UFIPA unapotokea makaburi ya kinondoni.
 
Hayati aliwachukia wafanyabiadhara maarufu kutoka mkoa flani akaamua kuua biashara zao kwa nguvu matokeo yake yeye ndio amekufa.
 
Back
Top Bottom