Serikali ma waajiri wengine wangetoa mshahara hata mara mbili kwa mwezi ili shughuli za kiuchumi zisiwe zinadorora

Serikali ma waajiri wengine wangetoa mshahara hata mara mbili kwa mwezi ili shughuli za kiuchumi zisiwe zinadorora

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Mada hii imawahi zungumzwa humu. Naomba kukazia zaidi. Kama wewe ni mfanyabiashara utaona kuwa biashara inachanganya mwisho wa mwezi. Baada ya wiki hivi inakata kabisa. Unakuwa unadunduliza tu.

Ili walau biashara na mzunguko wa pesa uwe mzuri mwezi wote serikali na waajiri wengine wangefanya mpango huo mshahara ulipwe mara mbili kwa mwezi. Katikati na mwisho wa mwezi. Hii itasaidia kuchangamsha mzunguko wa pesa. Katikati ya mwezi kunakuwa kukavu sana vibarua na business za hapa na pale zinadorora.

Mtu anaweza kusema mbona kiasi cha pesa kwa mwezi ni kilekile, ni kweli lakini masuala ya kiuchumi huwa yanakuwa ya kimahesabu na ya kisaikolojia.

Zamani haikuwezekana sababu mishahara ilitolewa benki mkononi. Leo mtandao umerahisisha sana utumaji na upokeaji pesa.

Hebu serikali icheki hili. Mshahara utolewe kila baada ya wiki mbili. Hata kila wiki ikiwezekana. Mzunguko wa pesa ambao ni endelevu ni muhimu sana.
 
Nchi zilizoendelea nyingi malipo ya mshahara hutoka kila mwisho wa wiki hii husaidia sana mtumishi kutoadhirika lakini pia katikati ya mwezi ni lazima watumishi wetu wapate posho kidogo, ya kujikimu
 
Nchi zilizoendelea nyingi malipo ya mshahara hutoka kila mwisho wa wiki hii husaidia sana mtumishi kutoadhirika lakini pia katikati ya mwezi ni lazima watumishi wetu wapate posho kidogo, ya kujikimu
Kwa wiki safi sana. Mtu haishi kwa mawazo. Na hata akienda kukopa mchele mwenye duka anajua kuwa mwisho wa wiki si mbali. Mtu anayetake home 600k akipewa zake 150k kila wiki anafanya uchimi uchangamke. Hii habari ya mabucha kujaw watu mwisho wa mwezi tu si nzuri. Hata watoto watapigwa na udumavu.
 
Hata hivyo tungeingia mfumo wa masaa, na mishahara iwe inalipwa kila baada ya wiki mbili hio ingesaidia sana hata kwenye suala zima la uchumi. Maana mfumo uliopo ni ule wa mkoloni hadi leo haujawahi badilika.
 
Mimi nasema mwanafunzi bora yule anae kopia mwenzake, serikali ikopi kutoka kwa wenzake walio endelea.🤣
 
Back
Top Bottom