Serikali: Marufuku Kutumia Ramani ya Tanzania kutoka Google Kufundishia Wanafunzi, Inaonesha Ziwa Nyasa liko Malawi

Kwani Mwalimu Nyerere alisemaje kuhusu huo mpaka?maana ye ndio final say
Nyerere alikuwa amezama kwenye mahaba ya kuunganisha Tanganyika na Zanzibar.
Tena inashangaza kuwa badala ya kukaa meza moja na Kamuzu Banda msomi kutoka Uingeleza kama yeye wakatatua mgogoro huu wa kikoloni, walianza kugombana wenyewe kwa wenyewe kiasi kwamba vita yetu ya kwanza kama nchi ilikuwa iwe na Malawi miaka ya 60/70
 
Ili Nchi Iendelee inatakiwa kuvamia na kufanya annexation ya Nchi nyingine.

Licha ya mipaka mingine ya kikoloni kukubalika ila huu wa Ziwa hapana
 
Kwani wewe unadhani hao wataalamu wa mambo ya nje hawajui kuwa mpaka haupo katikati ya ziwa?
Unafikiri Google wanabahatisha au wanasubiri waambiwe wapi mpaka upo?
Google wametumia facts zinazojulikana na kukubalika kimataifa kusema wapi mpaka ulipo.
Kwa mujibu wa mkoloni wako sahihi ila Kwa mujibu wa Tanzania huo mpaka haikubaliki.

Hiyo ni sawa na Nchi za Maziwa Makuu kukataa makubaliano ya mkoloni kuhusu mti Nile na vyanzo vyake kupendelea Egypt na Sudan.
 
Kwa nini alikuwa na mahaba ya kuunganisha Tanzania na Zanzibar na sio Tanzania na Malawi,alikuwa na manufaa gani kwenye hiko kipengele?
 
For years hakukuaga na hizi choko choko miaka ya 2010's ndipo zikaanza kuibukaaagaaa
Nani anaanzisha hizi chokochoko?kwani mipaka si iliwekwa tangu kwenue Berlin conference kumbe kuna namna inaweza kueditiwa?
 
Kwa nini alikuwa na mahaba ya kuunganisha Tanzania na Zanzibar na sio Tanzania na Malawi,alikuwa na manufaa gani kwenye hiko kipengele?
Ndio maana kizazi kipya kinaanza kuhoji mambo yanayohusu masilahi ya umma yalivyoamuliwa kienyeji kwa kuamini wakati huo kuwa watu wengi walikuwa na elimu duni ya kuhoji na kung'amua ufisadi wa kidola.

Tuendako kadiri watu wanavyozidi kuelimika wataanza kuhoji na kufukua makaburi. Moja ya eneo litakaloleta shida ni huu umiliki wa ardhi unaonadi ardhi kuwa mali ya umma chini ya udhamini wa Rais.
 
Hapo mwisho ndio umeua...hamna kitu kinanishangaza kama ardhi yangu nimenunua,nailipia halafu naambiwa ni mali ya serikali
 
Hili ziwa Kikwetr ilibaki kidogo sana akiwasheee.! Hawa malawi wameanza tena chokochoko.
 
Hapo mwisho ndio umeua...hamna kitu kinanishangaza kama ardhi yangu nimenunua,nailipia halafu naambiwa ni mali ya serikali
Halafu ardhi hiyo hiyo unachimba zako kisima unakutana na mwamba wa dhahabu,ghafla unaambiwa na maafisa wa Serikali kuwa madini ni mali ya Serikali uondoke!?
 
Mpaka wa hapo kwenye ziwa ni KATIKATI ya maji kwa mujibu wa universal law . Kila la heri .
 
Kwani Mwalimu Nyerere alisemaje kuhusu huo mpaka?maana ye ndio final say
Hatuwezi kukubali mipaka yetu ichezewe na watu wasiyoipenda Tanzania,..tutakufa na tutamwaga damu kwa ajili ya ardhi ya watanzania.🇹🇿
 
Nani anaanzisha hizi chokochoko?kwani mipaka si iliwekwa tangu kwenue Berlin conference kumbe kuna namna inaweza kueditiwa?
Malawi ndio hawataki Wana claims kua ZIWA lote ni lao hapo ndipo mzozo unapo anzia/ mtiti..
 
Mipaka sahihi ni ile iliyowekwa kwenye mkutano wa Berlin, mingine ni ubatili. Kwa maana hiyo hata Rwanda na Burundi ni mikoa ya Tanzania
Tuachane na beelin . Tukae kama waafrika tukubaliane tuishi kwa amani. Sema bado wanatutawala hivyo were wanalitaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…