Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,677
Kwenye uchumi ambao bei za bidhaa zinapanda kila uchwao, ili mtu uendelee ku survive na maisha, ni budi kipato kipande ili kupunguza ukali wa maisha. Hii kwa wachumi tunaiita 'Cost of living adjustment - COLA'.
Ndo maana utaona salary review zinapaswa kufanyika kila mwaka, na endapo kama haitafanyika lazima kutolewe sababu ni kwanini mwaka husika hakuna salary review na increment. Kipindi cha nyuma salary review ilikuwa inafanyika kote kote Sekta Binafsi na Sekta ya Umma na wafanyakazi kote kote, waliweza kufidiwa na ukali wa maisha kwa kuongezewa mishahara. Ilikuwa ni jambo zuri mno kwa mfanyakazi, maana nao ni binadamu ambao wana mahitaji pia yanayokuwa mwaka hadi mwaka.
Lakini kuanzia mwaka 2015, kumekuwa na kilio kikubwa kwa wafanyakazi wa umma kulikotokana na kutoongezewa mishahara mfululizo kwa miaka 5.
Nimefanya utafiti wangu wa haraka haraka, kwa kuangalia movement ya kupanda kwa bei za bidhaa kwenye matumizi makuu ya mfanyakazi tangu mwaka 2015 mpaka october 2020, na nimegundua kwamba kipato cha mfanyakazi kimenyongwa karibu kwa asilimia 19%. Ikiwa na maana ili mfanyakazi wa sasa as of October 2020, aishi maisha aliyokuwa anaishi mwaka 2015, ilipaswa kipato chake kiwe kimeshaongezeka kwa asilimia 19% au zaidi.
Lakini kwa sababu serikali haijaongeza mshahara kwa kipindi chote hicho, ni sahihi kusema huyu mfanyakazi kipato chake kimenyongwa kwa asilimia 19% ya kipato chake cha 2015, au pato lake limeshuka in real terms kwa asilimia 19% !!!!!!!!!
Huu hapa chini ni mfano wa mtu aliyekuwa analipwa mshahara wa sh 700,000
Ombi langu kwa serikali, kwa haraka na kwa hali ya dharura waangalie namna ya kuokoa jahazi la ubora wa maisha ya mfanyakazi wa umma, hili no bomu na linawaua taratibu.
Wengi sana wame stretch maisha yao na hii imeathiri pakubwa sana quality of life ya hawa ndugu zetu... Humu JF kuna mifano mingi sana wengi wanaleta nyuzi za majuto kila uchwao..
Hali inatisha sana, halafu mbaya zaidi sijahesabia impact ya deni la HESLB kwenye mahesabu yangu, ambayo ndo inafanya hali ya huyu mfanyakazi kuwa worse kuliko hata nilivoandika hapo.
Serikali mtafakari hili, hili bomu likilipuka, msitegemee productivity yoyote kwa hawa wafanyakazi, ni kama wapo wapo tu bora liende, na hii sio nzuri kwenye uchumi.. Ni janga!!!!
Na . N.Mushi
Mtetezi wa wanyonge
Ndo maana utaona salary review zinapaswa kufanyika kila mwaka, na endapo kama haitafanyika lazima kutolewe sababu ni kwanini mwaka husika hakuna salary review na increment. Kipindi cha nyuma salary review ilikuwa inafanyika kote kote Sekta Binafsi na Sekta ya Umma na wafanyakazi kote kote, waliweza kufidiwa na ukali wa maisha kwa kuongezewa mishahara. Ilikuwa ni jambo zuri mno kwa mfanyakazi, maana nao ni binadamu ambao wana mahitaji pia yanayokuwa mwaka hadi mwaka.
Lakini kuanzia mwaka 2015, kumekuwa na kilio kikubwa kwa wafanyakazi wa umma kulikotokana na kutoongezewa mishahara mfululizo kwa miaka 5.
Nimefanya utafiti wangu wa haraka haraka, kwa kuangalia movement ya kupanda kwa bei za bidhaa kwenye matumizi makuu ya mfanyakazi tangu mwaka 2015 mpaka october 2020, na nimegundua kwamba kipato cha mfanyakazi kimenyongwa karibu kwa asilimia 19%. Ikiwa na maana ili mfanyakazi wa sasa as of October 2020, aishi maisha aliyokuwa anaishi mwaka 2015, ilipaswa kipato chake kiwe kimeshaongezeka kwa asilimia 19% au zaidi.
Lakini kwa sababu serikali haijaongeza mshahara kwa kipindi chote hicho, ni sahihi kusema huyu mfanyakazi kipato chake kimenyongwa kwa asilimia 19% ya kipato chake cha 2015, au pato lake limeshuka in real terms kwa asilimia 19% !!!!!!!!!
Huu hapa chini ni mfano wa mtu aliyekuwa analipwa mshahara wa sh 700,000
| % Change in general prices (December 2015 to October 2020) | Wheights in % | |
| Food and Non Alcoholic Beverages | 23.37% | 38 |
| Clothing and Footwear | 14.63% | 8 |
| Housing, Water, Electricity, Gas and Other Fuel | 50.65% | 12 |
| Transport | 7.41% | 13 |
| Others (Average % change) | 8.18% | 29 |
100 | ||
| Allocaion of income of Tzs 700,000 per month in 2015 as per wheights | Needs allocation in 2015 | Amount required for a person to sustain same basket they consumed in 2015 |
| Food and Non Alcoholic Beverages | 266,000.00 | 328,164.20 |
| Clothing and Footwear | 56,000.00 | 64,192.80 |
| Housing, Water, Electricity, Gas and Other Fuel | 84,000.00 | 126,546.00 |
| Transport | 91,000.00 | 97,743.10 |
| Other consumption needs | 203,000.00 | 219,605.40 |
| Total income | 700,000.00 | 836,251.50 |
| Income increase that was required for person to live as they use to be in 2015 | 136,251.50 | |
| Depreciation of income (2015 to 2020) | 19.46% |
Ombi langu kwa serikali, kwa haraka na kwa hali ya dharura waangalie namna ya kuokoa jahazi la ubora wa maisha ya mfanyakazi wa umma, hili no bomu na linawaua taratibu.
Wengi sana wame stretch maisha yao na hii imeathiri pakubwa sana quality of life ya hawa ndugu zetu... Humu JF kuna mifano mingi sana wengi wanaleta nyuzi za majuto kila uchwao..
Hali inatisha sana, halafu mbaya zaidi sijahesabia impact ya deni la HESLB kwenye mahesabu yangu, ambayo ndo inafanya hali ya huyu mfanyakazi kuwa worse kuliko hata nilivoandika hapo.
Serikali mtafakari hili, hili bomu likilipuka, msitegemee productivity yoyote kwa hawa wafanyakazi, ni kama wapo wapo tu bora liende, na hii sio nzuri kwenye uchumi.. Ni janga!!!!
Na . N.Mushi
Mtetezi wa wanyonge