Serikali: Ugonjwa ulioambukiza watu 8 na kuua 5 Mkoani Kagera ni Marburg

Serikali: Ugonjwa ulioambukiza watu 8 na kuua 5 Mkoani Kagera ni Marburg

imhotep

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
55,997
Reaction score
88,219
Ugonjwa wa ajabu uliosababisha vifo vya watu watano kati ya wanane waliougua wilayani Bukoba Vijijini mkoani Kagera umetambuliwa kuwa ni Marburg. Soma: Ugonjwa wa Virusi vya Marburg: Historia, Uambukizwaji, Dalili na Matibabu

Imesema ugonjwa huo huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine au kutoka kwa mnyama kwenda kwa binadamu.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 21, 2023 jijini Dar es Salaam.

Waziri Ummy amesema ugonjwa huo hauna tiba mahususi bali hutibiwa kwa dalili husika anazokuwa nazo mtu. “Hadi kufikiwa leo siku tano tangu kuripotiwa ni watu nane ndio wameambukizwa na vifo ni vitano na watatu bado wanaendelea na matibabu,

“Tumefanikiwa kudhibiti ugonjwa huu haujatoka nje ya eneo lililolumbwa na ugonjwa huu,” amesema.

Machi 16, 2023 na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Tumaini Nagu siku chache baada ya ugonjwa huo kuripotiwa amesema umetokea katika vijiji vya Bulinda na Butayaibega vilivyopo katika kata za Marua Kanyangereko wilayani Bukoba. Leo Profesa Nagu amesema watu hao walipata dalili za homa, kutapika, kutokwa na damu maeneo mbalimbali ya mwili na figo kushindwa kufanya kazi.

Hivyo ili kudhibiti ugonjwa huo usisambae, amewataka watu kuepuka kumgusa mgonjwa au majimaji ya mwili mfano mate, machozi, damu, mkojo na kinyesi yatokayo kwa mgonjwa ama mtu mwenye dalili hizo.

Amesema iwapo mtu atalazimika kumhudumia mgonjwa kwa dharura, achukue tahadhari ya kujikinga majimaji yoyote kabla ya kumhudumia.

Chanzo: Mwananchi

Ripoti ya kuzuka kwa ugonjwa huo, soma: Kagera kuna hali ya hatari, kumezuka ugonjwa wa kutokwa damu puani na mdomoni. Watu 5 wafariki dunia 2 wako hospitali. Serikali ichukue hatua haraka

===

Nimekuwa nikiangalia Ayo TV Wazili wa Afya anasema Ugonjwa ulioua watu huko Kagera ni Marburg, nimefurahishwa na uwazi sijui ingekuwaje kama gonjwa hili ilingeingia walati wa ile Awamu ya laana?.

Huenda lingeitwa "Changamoto ya kuzimia".

============

UGONJWA WA MARBURG UNAWEZA KUSAMBAA KWA WATU NA WANYAMA
Serikali ya #Tanzania imebainisha ugonjwa ulioibuka Mkoani Kagera na kusababisha vifo vya watu kadhaa, Machi 2023 unaitwa Marburg ambao unasababishwa na Virusi vya Marburg (Marburg Viral Disease).

Unaweza kuambukizwa kwa njia ya kugusa majimaji kama mate, mkojo, damu, machozi au kinyesi yatokayo kwenye maiti au mgonjwa mwenye dalili.

Pia, maambukizi yanaweza kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu kwa kula au kugusa wanyama walioambukizwa.
 
Asante Uganda kwa kuendelea kutuambukiza na kutuletea Wahaya magonjwa ya ajabu.
 
Marburg hemorrhagic fever is a severe and highly fatal disease caused by a virus from the same family as the one that causes Ebola hemorrhagic fever.

Both diseases are rare, but can cause dramatic outbreaks with high fatality.
 
Hii kitu isichukuliwe Poa. Umakini mkubwa saaaana unatakiwa.

Yasifanyike masihara kabisa 62.5% Mortality rate sio Mchezo.
 
Waziri wa Afya ametaja ugonjwa ulioua watu 5 huko Bukoba kuwa ni Marbug disease ambao ni jamii ya Ebola

Marburg virus disease (MVD) is a rare but severe hemorrhagic fever which affects both people and non-human primates. MVD is caused by the Marburg virus, a genetically unique zoonotic (or, animal-borne) RNA virus of the filovirus family. The six species of Ebola virus are the only other known members of the filovirus family.

Marburg virus was first recognized in 1967, when outbreaks of hemorrhagic fever occurred simultaneously in laboratories in Marburg and Frankfurt, Germany and in Belgrade, Yugoslavia (now Serbia). Thirty-one people became ill, initially laboratory workers followed by several medical personnel and family members who had cared for them. Seven deaths were reported. The first people infected had been exposed to Ugandan imported African green monkeys or their tissues while conducting research. One additional case was diagnosed retrospectively.

The reservoir host of Marburg virus is the African fruit bat, Rousettus aegyptiacus. Fruit bats infected with Marburg virus do not show obvious signs of illness. Primates (including people) can become infected with Marburg virus, and may develop serious disease with high mortality. Further study is needed to determine if other species may also host the virus.
 
Hiyo ndiyo ile mi vijana ya hovyo isiyokuwa na mchango wowote kwa taifa hili.
Nilisema serikali itoe tamko kuwa kwa dalili hizi let us take precaution maana dalili hizi zinashabihiana na ebola. Wakati tunajiridhisha ni ugnjwa gani take precautions hiz na hizi
 
Duuh Marbug tena Dunia imekua na majanga juu ya majanga kweli kazi tunayo kwa kweli Mnyeezi Mungu atupiganie...
 
Marburg virus ni waliopo kwenye kundi la hemorrhagic fever viruses.

Huyu bwana mkubwa yupo na kamanda Ebola virus ,lassa virus na yellow fever virus.

Ni hatari, tujikinge na tumtangulize Mungu.
 
Nilisema serikali itoe tamko kuwa kwa dalili hizi let us take precaution maana dalili hizi zinashabihiana na ebola. Wakati tunajiridhisha ni ugnjwa gani take precautions hiz na hizi

nIliandika uzi huu hapa:

Ugonjwa wa ajabu Kagera uchunguzi siku ngapi?

Tokea tarehe 16/3/23 walishajua kuna taabu.

Hata sasa hatua zipi za maana zimechukuliwa?

Wilaya ya Mudende Uganda ugonjwa huu ulitesa sana kwa sababu za kizembe kama hizi.
 
Back
Top Bottom