Serikali ya Awamu ya Sita inajali Wananchi wake

Serikali ya Awamu ya Sita inajali Wananchi wake

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Waswahili wanasema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni ukweli ni kwamba serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu inawajali sana wananchi wake kupitia utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa Bomba la mafuta la Tanzania na Uganda Serikali ya Rais Samia Suluhu imetoa Kiasi cha shilingi Bilioni 27 kwa Wananchi watakaopitiwa na mradi wa bomba la mafuta ghafi kuanzia Kagera hadi Tanga.

Sasa Wakazi wa kata ya Kalambi na Kasharuga Wilayani Muleba mkoani Kagera waliopitiwa na mradi huo wamepewa nyumba kama fidia. Serikali ya awamu ya sita inatekeleza miradi ya maendeleo lakini inazingatia utu wa wananchi wake haya mambo kwa miaka kadhaa huko nyuma tuliyasahau kabisa serikali ilikua ikichukua maeneo ya wananchi na wananchi walikua wakifatilia fidia kwa muda mrefu sana lakini kipindi hiki cha uongozi wa Rais Samia Suluhu wananchi wamepewa fidia zao kwa wakati.

Lakini naona kujali ni hurka ya Rais Samia Suluhu maana tukiangalia hata kwa wamasai walijengewa nyumba nzuri Msomera pamoja na huduma za kijamii kuliko hata walipokua Ngorongoro tunaona dhamira ya Rais Samia Suluhu kuboresha maisha ya wananchi wake na sio kuwadidimizi Mungu amtunze Rais wetu.

HUU NI MUONEKANO WA NYUMBA WALIZOPEWA FIDIA WAKAZI WA MULEBA BEFORE AND AFTER
FqWpvxzWcAEuo9j (1).png
 
Sitaki nikuvunje moyo lakini hayo ni makubaliano baina ya wananchi na mradi wa EACOP (bomba la mafuta). Kisheria za kimataifa wanatakiwa pale watapowaondoa wananchi kwa kupitisha mradi basi wawalipe (iwe makazi, fedha au watakavyokubaliana). Hawa wamelipwa fedha na nyumba za makazi.

Huu mradi ulianza awamu ya JPM.
 
Back
Top Bottom