benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,533
- 3,187
Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EIB) imeeleza sababu za kurejea Tanzania na kufanya uwekezaji mkubwa wenye thamani ya Euro milioni 540 baada ya kutokuwapo kwa miaka saba nchini.
Moja ya sababu hizo ni maboresho makubwa yaliyofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoiongoza, ikiwamo kuhakikisha mazingira mazuri ya biashara kwa wawekezaji.
Makamu wa Rais wa EIB, Thomas Ostros aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa Kongamano la Biashara Kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya (EU) lililofunguliwa na Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango kwa niaba ya Rais Samia Suluhu.
Ostros alisema maboresho na mazingira mazuri ya biashara ndiyo yaliyowafanya kurejea Tanzania na leo wanatarajia kutia saini hati ya makubaliano ya fedha hizo.
Moja ya sababu hizo ni maboresho makubwa yaliyofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoiongoza, ikiwamo kuhakikisha mazingira mazuri ya biashara kwa wawekezaji.
Makamu wa Rais wa EIB, Thomas Ostros aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa Kongamano la Biashara Kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya (EU) lililofunguliwa na Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango kwa niaba ya Rais Samia Suluhu.
Ostros alisema maboresho na mazingira mazuri ya biashara ndiyo yaliyowafanya kurejea Tanzania na leo wanatarajia kutia saini hati ya makubaliano ya fedha hizo.