Serikali ya Rais Samia isijisumbue Hayati Magufuli alieleza kila kitu na aliweka wazi matatizo ya nchi hii

Serikali ya Rais Samia isijisumbue Hayati Magufuli alieleza kila kitu na aliweka wazi matatizo ya nchi hii

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Pamoja na mapungufu ya hayati John Magufuli lakini hakupepesa macho wala kumung'unya maneno pale penye ukweli.

Bado Serikali yahangaika kujimwambafwai lakini ukweli wa matatizo yoote yaliyopo nchini kwa sasa uliwekwa wazi na Hayati Magufuli.

Alieleza matatizo ya baadhi ya wahujumu uchumi wa nchi na maisha ya watanzania juu ya upunguzaji maji wa bwawa la Mtera ili maji yauzwe, video zipo na watanzania wamezihifadhi.

Tatizo la umeme pia aliliezea kuhusu ufisadi na biashara ya majenereta ambayo kimazingira si mazuri na pia kwa afya ya binadamu kutokana na moshi, video zake zipo na wananchi wamezihifadhi,.

Uzuri wa watanzania wengi wa sasa ni kwamba wanauwezo wa kununua vifaa vya kidijitali na asilimia kubwa wanatumia mitandao ya kijamii hivyo wana access ya kila alichokisema hayati Magufuli.

Hayati Magufuli alikuwa akizunguka nchi nzima kuwafahamisha watanzania juu ya kujiletea maendeleo na namna jinsi nchi hii ilivyobarikiwa kila kitu na tatizo na namna ya kutumia vyanzo vya maji, ardhi safi ilijaa rutuba na akawa akisisitiza kulima na kuhifadhi chakula.

Sasa, serikali imekwishaharibu kila eneo ambalo angalu lilikuwa limeleta unafuu na kwa miaka mitano hakukuwa na tatizo la umeme wala maji.

Hivyo Serikali hiihii ingetumia mbinu zilezile alozitumia hayati Magufuli kuhakikisha umeme wa uhakika unakuwepo na kila mwananchi anapata maji safi na salama.

Nasema hivyo kwa kuwa wizara ya nishaji ilikuwa ikiongozwa na mtaalam wa sekta ya nishati na pia baadhi ya mawaziri walokuwapo na ambao wapo wengi waliona uendeshaji wa serikali ya awamu ya tano.

CCM itambue kuwa serikali yake inayumba kutokana na kuamua kurudi tulikotoka, hivyo ni kheri ifanye maamuzi magumu ya kuukubali ukweli kuwa imeshindwa kutekeleza kwa makini Ilani yake ya uchuguzi ya mwaka 2015 na pia imeweka rasmi kabatini Dira yake ya maendeleo ya Taifa ya 2025 au imeipoteza.

Kuna tetesi kuwa waziri wa madini huenda nae akaondolewa kwa shinikizo la kwamba ni "hardliner" na alikuwa "inner circle" ya hayati hivyo hawa hardliners ni lazima waondolewe.

Wale welevu wote wapo na waangalia na kuku bado watengeneza uzuri mikakati ya kufanya dua kubwa la kumdondosha mwewe.
 
Hao mafisadi wapiga dili wa majenereta ndio leo wanakuja na namba nyingi ili kuficha wizi wao, wanaleta habari ya umeme wa maji unazalishwa kwa kiasi kidogo leo wakati kiasi hicho kidogo awamu iliyopita hakikuwahi kuleta mgao wa umeme licha ya ukame uliowahi kuwepo.

Watuambie ni kitu gani kilichoongeza matumizi ya nishati ya umeme mpaka kusababisha huu mgao tulionao sasa, ni viwanda vingapi vimejengwa toka Samia aingie ikulu?

Wezi wanaojulikana kwa tabia zao za kijanja janja hawawezi kuleta vijisababu vyovyote vya kitapeli vikaaminiwa na wanaojielewa, wawadanganye mazuzu tu.
 
CCM itambue kuwa serikali yake inayumba kutokana na kuamua kurudi tulikotoka, hivyo ni kheri ifanye maamuzi magumu ya kuukubali ukweli kuwa imeshindwa kutekeleza kwa makini Ilani yake ya uchuguzi ya mwaka 2015 na pia imeweka rasmi kabatini Dira yake ya maendeleo ya Taifa ya 2025 au imeipoteza.
Hata kama serikali inayumba na kushindwa kutekeleza dira na ilani yake bado ccm itashinda tu maana dola itakisaidia chama hiki kubakia madarakani. CCM itafanya ipendavyo wananchi hamna ubavu wa kuiondoa
 
Siku wafuasi wa Marehemu wakikubaliana na ukweli kwamba jamaa yao kafa na harudi tena basi roho zao zitatulia sana!! JPM kafa, na harudi tena, ukweli mchungu, mazuri yake yataendelezwa na upuuzi wake utakemewa hadharani kama wanavyokemewa watangulizi wake, and yeye hawezi kuwa SI Unit ya kuongoza nchi hii
 
Pamoja na mapungufu ya hayati John Magufuli lakini hakupepesa macho wala kumung'unya maneno pale penye ukweli.

Bado Serikali yahangaika kujimwambafwai lakini ukweli wa matatizo yoote yaliyopo nchini kwa sasa uliwekwa wazi na Hayati Magufuli.

Alieleza matatizo ya baadhi ya wahujumu uchumi wa nchi na maisha ya watanzania juu ya upunguzaji maji wa bwawa la Mtera ili maji yauzwe, video zipo na watanzania wamezihifadhi.

Tatizo la umeme pia aliliezea kuhusu ufisadi na biashara ya majenereta ambayo kimazingira si mazuri na pia kwa afya ya binadamu kutokana na moshi, video zake zipo na wananchi wamezihifadhi,.

Uzuri wa watanzania wengi wa sasa ni kwamba wanauwezo wa kununua vifaa vya kidijitali na asilimia kubwa wanatumia mitandao ya kijamii hivyo wana access ya kila alichokisema hayati Magufuli.

Hayati Magufuli alikuwa akizunguka nchi nzima kuwafahamisha watanzania juu ya kujiletea maendeleo na namna jinsi nchi hii ilivyobarikiwa kila kitu na tatizo na namna ya kutumia vyanzo vya maji, ardhi safi ilijaa rutuba na akawa akisisitiza kulima na kuhifadhi chakula.

Sasa, serikali imekwishaharibu kila eneo ambalo angalu lilikuwa limeleta unafuu na kwa miaka mitano hakukuwa na tatizo la umeme wala maji.

Hivyo Serikali hiihii ingetumia mbinu zilezile alozitumia hayati Magufuli kuhakikisha umeme wa uhakika unakuwepo na kila mwananchi anapata maji safi na salama.

Nasema hivyo kwa kuwa wizara ya nishaji ilikuwa ikiongozwa na mtaalam wa sekta ya nishati na pia baadhi ya mawaziri walokuwapo na ambao wapo wengi waliona uendeshaji wa serikali ya awamu ya tano.

CCM itambue kuwa serikali yake inayumba kutokana na kuamua kurudi tulikotoka, hivyo ni kheri ifanye maamuzi magumu ya kuukubali ukweli kuwa imeshindwa kutekeleza kwa makini Ilani yake ya uchuguzi ya mwaka 2015 na pia imeweka rasmi kabatini Dira yake ya maendeleo ya Taifa ya 2025 au imeipoteza.

Kuna tetesi kuwa waziri wa madini huenda nae akaondolewa kwa shinikizo la kwamba ni "hardliner" na alikuwa "inner circle" ya hayati hivyo hawa hardliners ni lazima waondolewe.

Wale welevu wote wapo na waangalia na kuku bado watengeneza uzuri mikakati ya kufanya dua kubwa la kumdondosha mwewe.
Kamfufueni Basi huyo mungu wenu, kenge nyinyi, naona Bado mnaweweseka wapuuz wakubwa
 
Tulie nae hata serikali ya mitaa ni oversize kwake.
 
Hawa Waswahili wa Pwani wakisha takeover, it's a guaranteed downward spiral from day one. Hawa ni wazungumzaji wazuri wa Kiswahili ndiyo lugha yao ya asili Tanzania hii. They will feed us nonsense after nonsense.
 
Hivi ni kweli enzi za utawala wa magu hakukuwa na tatizo la umeme wala maji?
 
Back
Top Bottom