Abdul Najad Faiq
Member
- Jul 13, 2021
- 7
- 5
Na:Abdull Najad Faiq
Zote Tanzania bara na Zanzibar linapokuja jambo ambalo lipo ndani ya orodha ya mambo ya Muungano, huwakilishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndio Serikali mama inayopanga sera na dira ya nchi kimataifa
Uchumi wa Zanzibar na Tanzania bara kamwe hauwezi kuwa sawa kutokana na jeografia ya nchi husika.
Uchumi wa Zanzibar zaid unategemea biashara ya huduma ikiwemo Utalii pamoja na Bandari, Zanzibar haina madini wala kilimo cha kuweza kutosheleza zaid ya zao la biashara la Karafuu pamoja na Mwani.
Pia soma: Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?
Kutokana na kwamba Fedha, Sarafu pamoja na Mabank ni katika mambo ya muungano basi bila ya shaka Uchumi wa Zanzibar utategemea sera za kiuchumi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kupiga hatua kimaendeleo
Upatikanaji wa mikopo kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya kimkakati Zanzibar, kunategemea na dhamana ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Waziri wa Fedha kutokana na kwamba Zanzibar haina uwezo wa kukopa katika taasisi za Kimataifa
Katika njia nyengine ambayo Serikali za nchi duniani huweza kupata mapato kwa ajili ya kuinua uchumi wake ni "misaada na mikopo ya kimataifa" sote tulikua mashahidi jinsi fedha za "Uviko19" zilivyokuja kuibua miradi mbali mbali nchini, ukuaji wa uchumi wa Zanzibar unategemea utashi wa kiongozi wa Tanzania ikiwa ataipatia Zanzibar senti 2 katika kila senti 10 zitakazo kuja kutoka duniani kupitia jina la Tanzania
Uchumi wa Zanzibar unategemea faida inayoweza kupata kupitia majukwaa ya kimataifa mfano Jumuiya ya Afrika Mashariki, Zanzibar nayo pia ni mwanachama wa jumuiya hiyo, kupitia jukwaa hili Zanzibar inaweza kunufaika moja kwa moja kupitia fursa zilizopo ikiwemo masoko ya kibiashara
Zanzibar kama mshirika wa Muungano wa Jamhuri ya Tanzania iliwahi kujiunga na jumuiya ya OIC ili kunufaika kichumi ila iliamuriwa kujitoa na Serikali ya Tanzania na badala yake Serikali ya Jamhuri ikasema itajiunga badala yake sababu Zanzibar si nchi katika nyanja za kimataifa ila hadi leo Tanzania haijajiunga na jumuiya ya OIC
Kuna watu wanasema kwamba jumuiya ya OIC haina maslahi,ipo kisiasa zaid ila kwa maoni yangu wanaotoa hoja za aina hii ndio wapo kisiasa zaid sababu Zanzibar kama ni miongoni mwa mshirika wa Muungano anapaswa kuwa na Uhuru wa kufanya kile anacho kiamini ilimradi anahisi kina maslahi kwake na yeye ndie atakae wajibika kwa kila kitu, kusiwepo na hali ya kuwekeana vikwazo
Sera za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa 70% zinaamua hali ya uchumi wa Zanzibar, sote tunajua kwamba Zanzibar ina idadi ya watu wapatao milioni 2 huku Tanzania bara ikiwa na watu wapatao milioni 59, ikiwa hii leo Mamlaka inayo husiana na "Utoaji wa Leseni za Viwanda Tanzania" ni moja ila muwekezaji aliyewekeza kiwanda Zanzibar akitaka kupeleka bidhaa yake katika soko la Bara inakutana na vikwazo, ila kiwanda hicho hicho kikileta bidhaa katika soko la Zanzibar ni sawa huko ni kuua uchumi wa Zanzibar na kuwaambia wawekezaji kwamba njooni Bara mutakua salama na musiende Zanzibar
Jambo jengine linaloweza kuinua ghafla uchumi wa Zanzibar ni kupatikana kwa usuluhisho kamili juu ya masuala yote ya kifedha baina Zanzibar pamoja na Serikali ya Tanzania bara ikiwemo mgogoro kuhusu hisa za Zanzibar BoT pamoja na Mapato yanayotokana na Account ya Pamoja ya Fedha, mgogoro ambao ni wa muda mrefu, ulioota mizizi na uliobeba Pesa nyingi
Kwahiyo kivyovyote mifumo bora ya ya kiuchumi pamoja na ya Kisera na ya kiutatuzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo pekee inayoweza kuamua "Hatma ya Uchumi wa Zanzibar" iwe na uchumi wa aina gani.
Zote Tanzania bara na Zanzibar linapokuja jambo ambalo lipo ndani ya orodha ya mambo ya Muungano, huwakilishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndio Serikali mama inayopanga sera na dira ya nchi kimataifa
Uchumi wa Zanzibar na Tanzania bara kamwe hauwezi kuwa sawa kutokana na jeografia ya nchi husika.
Uchumi wa Zanzibar zaid unategemea biashara ya huduma ikiwemo Utalii pamoja na Bandari, Zanzibar haina madini wala kilimo cha kuweza kutosheleza zaid ya zao la biashara la Karafuu pamoja na Mwani.
Pia soma: Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?
Kutokana na kwamba Fedha, Sarafu pamoja na Mabank ni katika mambo ya muungano basi bila ya shaka Uchumi wa Zanzibar utategemea sera za kiuchumi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kupiga hatua kimaendeleo
Upatikanaji wa mikopo kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya kimkakati Zanzibar, kunategemea na dhamana ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Waziri wa Fedha kutokana na kwamba Zanzibar haina uwezo wa kukopa katika taasisi za Kimataifa
Katika njia nyengine ambayo Serikali za nchi duniani huweza kupata mapato kwa ajili ya kuinua uchumi wake ni "misaada na mikopo ya kimataifa" sote tulikua mashahidi jinsi fedha za "Uviko19" zilivyokuja kuibua miradi mbali mbali nchini, ukuaji wa uchumi wa Zanzibar unategemea utashi wa kiongozi wa Tanzania ikiwa ataipatia Zanzibar senti 2 katika kila senti 10 zitakazo kuja kutoka duniani kupitia jina la Tanzania
Uchumi wa Zanzibar unategemea faida inayoweza kupata kupitia majukwaa ya kimataifa mfano Jumuiya ya Afrika Mashariki, Zanzibar nayo pia ni mwanachama wa jumuiya hiyo, kupitia jukwaa hili Zanzibar inaweza kunufaika moja kwa moja kupitia fursa zilizopo ikiwemo masoko ya kibiashara
Zanzibar kama mshirika wa Muungano wa Jamhuri ya Tanzania iliwahi kujiunga na jumuiya ya OIC ili kunufaika kichumi ila iliamuriwa kujitoa na Serikali ya Tanzania na badala yake Serikali ya Jamhuri ikasema itajiunga badala yake sababu Zanzibar si nchi katika nyanja za kimataifa ila hadi leo Tanzania haijajiunga na jumuiya ya OIC
Kuna watu wanasema kwamba jumuiya ya OIC haina maslahi,ipo kisiasa zaid ila kwa maoni yangu wanaotoa hoja za aina hii ndio wapo kisiasa zaid sababu Zanzibar kama ni miongoni mwa mshirika wa Muungano anapaswa kuwa na Uhuru wa kufanya kile anacho kiamini ilimradi anahisi kina maslahi kwake na yeye ndie atakae wajibika kwa kila kitu, kusiwepo na hali ya kuwekeana vikwazo
Sera za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa 70% zinaamua hali ya uchumi wa Zanzibar, sote tunajua kwamba Zanzibar ina idadi ya watu wapatao milioni 2 huku Tanzania bara ikiwa na watu wapatao milioni 59, ikiwa hii leo Mamlaka inayo husiana na "Utoaji wa Leseni za Viwanda Tanzania" ni moja ila muwekezaji aliyewekeza kiwanda Zanzibar akitaka kupeleka bidhaa yake katika soko la Bara inakutana na vikwazo, ila kiwanda hicho hicho kikileta bidhaa katika soko la Zanzibar ni sawa huko ni kuua uchumi wa Zanzibar na kuwaambia wawekezaji kwamba njooni Bara mutakua salama na musiende Zanzibar
Jambo jengine linaloweza kuinua ghafla uchumi wa Zanzibar ni kupatikana kwa usuluhisho kamili juu ya masuala yote ya kifedha baina Zanzibar pamoja na Serikali ya Tanzania bara ikiwemo mgogoro kuhusu hisa za Zanzibar BoT pamoja na Mapato yanayotokana na Account ya Pamoja ya Fedha, mgogoro ambao ni wa muda mrefu, ulioota mizizi na uliobeba Pesa nyingi
Kwahiyo kivyovyote mifumo bora ya ya kiuchumi pamoja na ya Kisera na ya kiutatuzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo pekee inayoweza kuamua "Hatma ya Uchumi wa Zanzibar" iwe na uchumi wa aina gani.