Serikali yaagiza Mabasi ya Shule yawe na 'Makondakta' wa kike

Serikali yaagiza Mabasi ya Shule yawe na 'Makondakta' wa kike

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
SERIKALI imeagiza mabasi yote yanayobeba wanafunzi kuwa na kondakta wa kike na mabasi yote yafungwe Camera maalum.

Waziri wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maaalum, Dk. Dorothy Gwajima ametoa agizo hilo alipokuwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe katika Shule ya Star Light Pre and Primary School, ambapo mtoto wa miaka sita wa darasa la kwanza anadaiwa kubakwa na kondakta wa gari hilo.

Dk. Gwajima amesema “Watuhumiwa kwa sasa wapo ndani na wameshapanda mahakamani, pongezi wote waliowajibika haraka kesi inaendelea,” amesema Gwajima.

“Na hapa hakuna cha gharama kuongezeka maana jinsia tu ndio inabadilika. Hii itawezesha ulinzi imara kwa mtoto wa kwanza kuchukuliwa na wa mwisho kurejeshwa,” amesema na kuongeza.

“Huko mbele kuna haja ya kufunga camera kwenye mabasi ya shule tunaangalia uwezekano. Lazima wateja walindwe yaani mtoto ni mteja jamani inakuwaje analipia huduma halafu anafanyiwa vitendo vya kikatili?” amehoji.

Tamko hilo la Serikali linakuja ikiwa ni siku chache baada ya kusambaa kwa taarifa katika mitandao ya kijamii inayosema ‘Dereva na anko wabaka mtoto wa miaka sita’
 
Feza schools ukienda pale unakuta private zipo zawasubiri watoto ziwarudishe makwao.
Wazazi tusomeshe watoto karibu na makazi yetu, watoto huteseka kuamka mapema na kuzungushwa kupitia wengine au kushusha wengine. Mtoto wa kwanza kuchukuliwa ndo wa mwisho kushushwa, na yeye ndo huathirika zaidi
 
Hiyo ni nchi ya zima mito hakuna utaratibu kabisa kila mtu anaropoka kutokana na tukio, waalimu wangapi wana baka watoto jinsia zote kwa hilo tutafanyaje?
 
Feza schools ukienda pale unakuta private zipo zawasubiri watoto ziwarudishe makwao.
Wazazi tusomeshe watoto karibu na makazi yetu, watoto huteseka kuamka mapema na kuzungushwa kupitia wengine au kushusha wengine. Mtoto wa kwanza kuchukuliwa ndo wa mwisho kushushwa, na yeye ndo huathirika zaidi
Sawa . Hivi Emanuel Macron wa Ufaransa alimpataje mkewe? Nasikia Wazazi walipinga sana lakini wapi.
 
Sio makondakta tu hata madereva wa school bus wawe wanawake itaondoa hayo mambo ya kishenzi
 
Aje atoe tamko hatima ya watoto waliofutiwa matokeo sababu ya makosa ya shule.
Kwanini watoto wadogo wa miaka 12 hadi 14 waadhibiwe kwa kosa la waalimu na wamiliki wa shule?
Hivi wanajua watoto wameumia kiasi gani?
 
Serikali iende mbali zaidi.
Watu wanaojihusisha na watoto kama hao madereva wa school buses, nannies, wapishi n.k wapate training kuwasaidia kuwaelewa watoto. Angalau basic child development psychology.
Hao Malinda wa kike wanaweza wasiwaharibu watoto physically ila wakawadamage kihisia kwa maneno yao ya shombo.
 
Unaangalia takwimu? Wewe kweli pimbi, hata hivyo huwa si argue na idiots. Tafuta wa level yako.
Takwimu naamini ndizo zinatoa muongozo kundi lipi lizingatiwe. Kama hauangalii takwimu unasemaje mwenzako ni pimbi ujuaji mwingi muda mwingine unafanya uonekane zuzu usiejielewa
 
Mabasi Yanatakiwa yawe na security cameras na vinasa sauti vilivyounganishwa polisi na kwa mwenye Shule na mwenye mtoto akitaka. Hapo mchezo huo muovu utapunguzwa kwa asilimia kubwa. Ninawaza hivyo.
 
Back
Top Bottom