Tetesi: Serikali yadaiwa kumvua uraia Padri wa Kanisa Katoliki

Tetesi: Serikali yadaiwa kumvua uraia Padri wa Kanisa Katoliki

Wengine hat kuwa na utaratibu wa jujengea makaburi, yale matuta yamesha titia. Tutainyesha nini?
Mimi hii habari nadhani huenda inapotosha. Kwanini nasema hivyo? Ni siku chache zilizopita maaskofu walifanya kikao na rais na kulingana na mazungumzo yao baada ya kikao inaonyesha wanaridhika kwa kiasi kikubwa na uongozi wa serikali ya awamu hii. Je, kungekuwa na tatizo kubwa kama hili la padri tena aliyekuwa katibu mkuu wa maaskofu kunyang'anywa uraia kwa sababu tu ya ule waraka wangeonyesha furaha namna ile? I mean maaskofu wote wale wangeweza kuwa wanafiki kiasi kile na kuamua kumsaliti mwenzao?
 
Mimi hii habari nadhani huenda inapotosha. Kwanini nasema hivyo? Ni siku chache zilizopita maaskofu walifanya kikao na rais na kulingana na mazungumzo yao baada ya kikao inaonyesha wanaridhika kwa kiasi kikubwa na uongozi wa serikali ya awamu hii. Je, kungekuwa na tatizo kubwa kama hili la padri tena aliyekuwa katibu mkuu wa maaskofu kunyang'anywa uraia kwa sababu tu ya ule waraka wangeonyesha furaha namna ile? I mean maaskofu wote wale wangeweza kuwa wanafiki kiasi kile na kuamua kumsaliti mwenzao?
Petro alimkana Yesu mara tatu, pamoja na kiapo chake kwamba asingefanya hivyo.
 
Hii habari imetiwa chumvi sana. Rev Fr Saba ni mmoja wa watu makini sana, msomi na mtu asiyependa makuu. Ni mwalimu mzuri na mnyenyekevu. Ninachompendea zaidi ni ile self determination aliyonayo daima. He did great work hata alipokuwa Roma.

Kama serikali inahoji uraia wake, basi itakuwa ni moja ya serikali za kizwazwa sana, tena serikali iliyotopea.

The church is greater than this government. Kama walishindwa kumshughurikia Gwajima (kama c mtu wa system), basi kwa mkatoliki huyu wanatafuna chuma cha reli kwa meno ya makaratasi!!
 
Serikali inaendelea kushikilia pasipoti yake (Padri Saba) kama inavyoshikilia pasopoti za wengine inaowachapa “kiboko cha uraia” kwa sababu za kisiasa.
Hii umenishtua kumbe Padri alikuwa anafanya siasa? Sidhani kama hii nikazi ya Padri, ninachojua Padri anatunza imani na kuongeza idadi ya waumini. Na mambo mengine yahusuyo dini. TEC nadhani waliona hoja kumuondoa.
Padri Saba, Askofu Kakobe, Eyakuze, na Nondo ni wazaliwa wa Kigoma. Askofu Niwemugizi ni mzaliwa wa Kagera. Orodha ya wanaoshughulikiwa “kimfumo” ni ndefu.
BlackBold: Hapa ama unania ya kumuaharibia Eyakuze, ama habari yako hii ni ya uongo. Ninachojua Eyakuze alisema yeye ni Muhaya, nadhani rekodi zipo hapa JF wakati akitoa maelezo hayo.
 
Haya mambo ya uraia si mchezo.
Kila mmoja akifuatiliwa uraia wake (Hasa uraia wa mababu/bibi) na wasi wasi karibu watanzania wote si raia wa Tanzania. Maana kabla ya makoloni kugawana bara hili, kunafamilia zilikuwa zinaishi sehemu moja, ila mipaka ilipowekwa na wakoloni, basi familia zile ziligawanywa na kuishi sehemu/nchi karibia tatu.
Hao watu wa uamihaji pia nao yawezekana si raia.
 
Hii habari imetiwa chumvi sana. Rev Fr Saba ni mmoja wa watu makini sana, msomi na mtu asiyependa makuu. Ni mwalimu mzuri na mnyenyekevu. Ninachompendea zaidi ni ile self determination aliyonayo daima. He did great work hata alipokuwa Roma.

Kama serikali inahoji uraia wake, basi itakuwa ni moja ya serikali za kizwazwa sana, tena serikali iliyotopea.

The church is greater than this government. Kama walishindwa kumshughurikia Gwajima (kama c mtu wa system), basi kwa mkatoliki huyu wanatafuna chuma cha reli kwa meno ya makaratasi!!
Huu ni mkwala.
 
nimeona hii trend ya huyu padre inavuma sana, kama ni kweli basi kazi ipo
 
Mimi ni mtanzania original lakini kweli ukiniambia nikuonyeshe kaburi la bibi mzaa baba sijui nitaanzia wapi. Kwa kigezo hichi cha makaburi wengi sii raia.

Criteria zetu ni za karne ya 17
 
Acheni Wafu wazike wafu wenzao. Unamtetea huyo kwani wewe ni askofu? Punguzeni viherehere mtakuja kufa vifo si vyenu
 
Sasa huku tunakokwenda si kuzuri.

Ninakumbuka Namfua alitaka ardhi ya watawa wa kanisa Katoliki Kilacha itolewe kwa vijiji vya ujamaa.

Alisema ”ardhi itolewe kwa watu wanaozaa na kuendeleza taifa kuliko kuwaachia wale matasa”. Watawa walianza Novena, Namfua alipata ajali mbaya iliyosabisha kifo chake.
Duuh...wapi huko na mwaka gani? Mwenyezi Mungu hujibu Maombi
 
Acheni Wafu wazike wafu wenzao. Unamtetea huyo kwani wewe ni askofu? Punguzeni viherehere mtakuja kufa vifo si vyenu
Aisee Mmteule,

VIONGOZI WENGI WA SERIKALI NDIYO VIHEREHERE , WAKIONGOZWA NA JIWE.
 
Jiwe anajionaa wakati kazaliwa Burundi aahaaa...hatutaki kuongozwa na pua ndefu tena..watanzania amkeni ...
 
Kigoma ni lazima iangaliwe kwa jicho pevu kwa sababu ni sehemu muhimu sana kwa usalama wa nchi yetu. Tusilaumu tu kwa sababu za kisiasa. Usalama wa Tanzania ni mihimu kuliko chochote ukijuacho. Tanzania inazungukwa na nchi jirani za Msumbiji, Malawi, Zambia, DR Congo, Burundi, Rwanda, Uganda na Kenya. Lakini kati ya hizo zote Burundi na Congo ziko kwenye hali tete kiusalama na zote hizo ziko karibu sana na mkoa wa Kigoma. Hapo unaweza kuona umuhimu wa kiusalama kwa mkoa wa Kigoma. Lakini pia Kigoma ndo mkoa pekee wenye lango linalounganisha nchi tatu za nje ambazo ni Burundi, Congo na Zambia hivyo kuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa na wageni wengi wasio raia. Hivyo basi kwa kila raia wa Tanzania anayetoka Kigoma lazima uwe nae makini sana kwani anaweza kuwa katoka nje ya nchi akajifanya anatoka Kigoma.

Lakini pia mkoa wa Kigoma unapakana na nchi zenye matatizo ya kiuchumi kiasi kwamba raia wengi wa nchi hizo hupenda sana kukimbilia Kigoma kutafuta kazi na vibarua vya kufanya kukidhi mahitaji yao. Ni kama ilivyo kwa South Africa inavyovutia wahamiaji wengi kutoka nchi zote za kusini mwa Africa.
Mimi ni mzaliwa wa Kigoma nafahamu maisha ya huko. Mara nyingine kumtofautisha muha wa Muyama kwetu na Kayogoro au Makamba Burundi inakuwa vigumu sana. Ama kumtofautisha Mbembe wa Helembe, Sunuka, Sibwesa na Mbembe wa Moba, Baraka na hata Kalemii au Uvira Congo inakuwa vigimu.

Ni kwa misingi hiyo kama nchi huru tunapaswa kuwa waangalifu kwenye uraia wa wananchi wetu.
Watu wa Kigoma sisi kama raia halal wa nchi hii tunao wajibu wa kuilinda mipaka yetu na kuwachunguza watu wasio raia miongoni mwetu.
Hatuna nchi nyingine Tanzania ndo nchi yetu.
Nchi jirani nao wana utaratibu wao wa kuwashughulikia watu wasio raia wa nchi zao.
Kigoma tusigombanishwe na serikali yetu na wajinga wachache kwamba serikali haitupendi. Tuendelee kuipenda na kuilinda nchi yetu kuanzia Mashariki mpaka Mafharibi na kutoka Kusini mpaka Kaskazini.

Karibuni kijijini kwetu Muyama mpakani kabisa na Burundi.
Aksante.
vizuri, sasa nikuulize kwanini mtu ahojiwe uraia wake pindi tu akiongea maneno ya kuikosoa siri kali?
 
Ila Kigoma kz ipo uraia wao huwa una mashaka kwa sababu ya mwingiliano Mkubwa na tamaduni zinazofanana na akina kurunziza.Na wao wapunguze ubishi maana ni wabishi kupita kiasi!
Hili siyo tatizo la Kigoma peke yake, mikoa yote ya mipakani tatizo hilo la mwingiliano lipo, Wamasai wa Kenya vs Wamasai wa Tanzania, Wakurya wa Kenya vs wakurya wa Tanzania, Wangoni, Makonde, wanyasa, wagunya, nk
 
Back
Top Bottom