Mkuu pamoja na kwamba upo Uhuru sana, siyo kila jambo la Mwajiri wako upeleke Mitandaoni hasa nyaraka za malipo serikalini. Imagine wewe jalada lako binafsi pia serikali au Afisa mmoja akachapisha hapa taarifa zako utajiskiaje? Kanuni Na.8 ya ajira yako imekusisitiza Kamwe taarifa za Mwajiri wako usizitoe kwa mtu yeyote yule lkn wewe hapo umenakili maneno ya Waraka wa SIRI mtandaoni ambao hata Rais hakuutaja wakati wa MEI MOSI. Sio tu kwamba unaleta usumbufu kwa Wafanyakazi wenzako lkn inakuweka kwenye wakati mgumu sana ikitokea bahati mbaya ukabainika. Jiepusha sana na haya makitu Mkuu. Ni ushauri tuu mkuu otherwise nyongeza tunaisubir huku Mtaani iongeze mzunguko wa pesa.