Serikali yafuta vijiji na vitongoji vyote vya wamasai wa Ngorongoro kupitia Amri ya tangazo la Serikali namba 673

Serikali yafuta vijiji na vitongoji vyote vya wamasai wa Ngorongoro kupitia Amri ya tangazo la Serikali namba 673

AMRI YA MAREKEBISHO YA AMRI YA MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA KATIKA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA) YA MWAKA 2024

1. Amri hii itajulikana kama Amri ya Marekebisho ya Amri ya Mgawanyo wa Maeneo ya Utawala katika Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) ya Mwaka 2024 na itasomwa pamoja na Amri ya Mgawanyo wa Maeneo ya Utawala katika Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) ya Mwaka 2019 ambayo hapa imerejewa kama "Amri kuu".

2. Amri kuu inarekebishwa katika Jedwali kwa kufuta kata, vijiji na vitongoji katika Halmashauri za Wilaya ya Ngorongoro, Bahi, Chemba, Kasulu, Kakonko, Hai na Rombo kama ilivyoainishwa katika Jedwali.

Hili ni Tangazo la Serikali namba 673 la Agosti 2, 2024.

View attachment 3074381

Pia soma>> Wamasai wa Ngorongoro watoa tamko kunyang'anywa haki ya kupiga kura 2024 na 2025
Fear of defeat
 
Ni wakati Sasa na wale wenye milli za kimila wakaziacha ili maeneo Yao yapate mchanganyiko wa makabila mbalimbali kuleta maendeleo.

Ni vizuri ukawepo mpango wa muda mrefu wa kupima ardhi bila kurekebisha mara kwa mara matumizi yake,kwa kuwa idadi ya watu nayo inazidi kuongezeka.
 
Mtu anahamishiwa eneo ambalo lina miundombinu yote barabara nzuri umeme maji anapewa nyumba mpya ya room 3 anapewa shamba la hekali 2 anapewa ngombe wa3 anapewa gunia 10 za mahindi kama haitoshi na bado anapata cash tsh 10ml; bado analeta ubishi wa kiduanzi tu,, yaani hawa lolote liwakute tu,,
 
Mtu anahamishiwa eneo ambalo lina miundombinu yote barabara nzuri umeme maji anapewa nyumba mpya ya room 3 anapewa shamba la hekali 2 anapewa ngombe wa3 anapewa gunia 10 za mahindi kama haitoshi na bado anapata cash tsh 10ml; bado analeta ubishi wa kiduanzi tu,, yaani hawa lolote liwakute tu,,
Hawana shida na hizo mali
 
Hivi,kule kisiwani Zanzibar wale binadamu wanafanya nini kule?Kwa nini wasihamishiwe Shinyanga ili watalii wakione kisiwa hicho kwa uzuri zaidi?Wanatukosesha mapato wale.Zanzibar island(s) is for tourism industry!Zanzibar ni kwa ajili ya uchumi wa kibuluu.
Nimekuelewa vizuri, nimependa mawazo yako wanapaswa kuhama ili kuweza kupokea watalii wengi kwa wakati mmoja
 
AMRI YA MAREKEBISHO YA AMRI YA MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA KATIKA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA) YA MWAKA 2024...
Kuna matatizo makubwa sana kwenye suala hili. Serikali naona kama vile inatapatapa vile.

Endapo kama kweli Serikali Ina Nia njema kuhusiana na suala hili la kuwahamisha hao Wamasai kutoka huko Ngorongoro, kwa nini itumike nguvu nyingi na kubwa sana namna hii?? Je, mikutano au vikao vya wazi kati ya Serikali na hao Wananchi kuhusu maandalizi ya suala hili la kuwahamisha viliketi lini na wapi?

Kwa nini kwa upande wa Serikali Kuna usiri mkubwa sana juu ya michakato ya suala hili?

Je, taratibu zote za kisheria zimefuatwa katika Mchakato mzima wa kuwahamisha watu hao? Je, kila mhusika anayepaswa kuhama tayari ameshalipwa haki zake zote kabisa stahili kabla ya kutakiwa kuhama kutoka kwenye maeneo hayo?
 
Back
Top Bottom