Serikali yakiri Umeme hautoshi, TANESCO ina upungufu wa Megawati 190

Serikali yakiri Umeme hautoshi, TANESCO ina upungufu wa Megawati 190

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Serikali imekiri kuwa na upungufu wa umeme kwa megawati 190 na ndiyo sababu za kukatika au kuwa na mgawo wa mara kwa mara. Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 2, 2022 bungeni na Naibu Waziri wa Nishati, Stephen Byabato wakati akitoa maelezo kama alivyotakiwa na Spika wa bunge Dk Tulia Akson.

Dk Tulia alimtaka Naibu Waziri kutoa majibu ya jumla kuhusu kukatika umeme kwani jambo hilo limekuwa kero. Katika swali la msingi Mbunge wa Ndanda (CCM), Cecil Mwambe ametaka kujua mkakati wa Serikali kumaliza kero ya kukatika kwa umeme mara Kwa mara ikiwemo mikoa ya kusini.

"Tatizo tulilonalo ni upungufu katika vyanzo vya kuzalisha umeme, mheshimiwa Spika, kwa sasa tuna upungufu wa megawati 190 katika vyanzo vya kuzalisha umeme nchini," amesema Byabato. Hata hivyo ameliambia Bunge kuwa mwezi ujao mradi wa Kinyelezi One utakamilika na kuingiza megawati 185 ambazo zitapunguza makali ya mgawo wa umeme.

Kingine ni mpango wa Serikali wa kutenga Sh500 bilioni kwa ajili ya kusaidia kwenye ukarabati wa miundombinu. Hata hivyo Spika ameagiza suala la mgawo wa umeme litazame vipaumbele kwa baadhi ya maeneo ambayo yanahitaji umeme kwa shughuli za viwanda na huduma muhimu ikiwemo Afya
 
Makamba alisema tuna ziada alipokuwa akifanya mahojiano na 360 Clouds, huyu naibu Byabato anasema tuna upungufu, nani mkweli?

"RAIS SAMIA FUMUA TANESCO,HII NI DHIHAKA, LABDA KAMA NA WEWE NI MNUFAIKA WA YANAYOENDELEA NISHATI,"

Makamba umembeba habebeki, kwahiyo ilifumuliwa Tanesco kutuletea hii dhahama?
 
Serikali imekiri kuwa na upungufu wa umeme kwa megawati 190 na ndiyo sababu za kukatika au kuwa na mgawo wa mara kwa mara. Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 2, 2022 bungeni na Naibu Waziri wa Nishati, Stephen Byabato wakati akitoa maelezo kama alivyotakiwa na Spika wa bunge Dk Tulia Akson.
Hiyo mijitu ya Sisiem, ni kila siku kutupiga saundi waTZ.

Hii Hali itaisha pale tu tutakapowang'oa madarakani Hawa wanaojifanya Wana hati miliki ya kutawala nchi hii milele🥺
 
Tunaotegemea ma freezer ku survive tunaisoma namba. Tutafika 2025 tumechoka sana
 
Nunua

Generator
😂 Nacheka kwasababu umenikumbusha uzi niliusoma jana jamaa anauliza mauzo ya 100M kwa mwaka ni haki kuingia VAT? Wakati kumbe faida ni 10k tu kwa siku! Kwa kifupi siwezi kuingia gharama ya generator bora niachane nayo tu. Lakini namba nimezisoma kweri kweri.
 
Upungufu huu unawezekana umesababishwa na madhara ya ukame au sababu nyengine. Hilo lingeeleweka kama NW ametoa ufafanuzi wa nini sababu ya upungufu huu. Lakini kama ni ujanja ujanja wa majibu rahisi kwa mambo muhimu kama hili la umeme na yanayo gusa maisha ya Watanzania moja kwa moja basi wakae wakijua tumepewa Funguo za Ufalme wa Mbinguni. Tukifunga tumefunga na tukifungua tumefungua.
 
Makamba alisema tuna ziada alipokuwa akifanya mahojiano na 360 clouds,huyu naibu Byabato anasema tuna upungufu,nani mkweli,?

"RAIS SAMIA FUMUA TANESCO,HII NI DHIHAKA,LABDA KAMA NA WEWE NI MNUFAIKA WA YANAYOENDELEA NISHATI,"

Makamba umembeba habebeki, kwahiyo ilifumuliwa Tanesco kutuletea hii dhahama?
RWANDES atabisha
 
KAMA sikosei niliisikia kauli ya Mh Makamba kuwa tuna surplus ya umeme leo imekuwaje tunaambiwa tuna nakisi ya umeme.hizi kauli mbona zinapingana na nani sasa ni mkweli naibu au waziri mwenyewe?
 
Back
Top Bottom