Serikali yangu tukufu mnayajua magumu wanayopitia Watumishi wa Halmashauri

Serikali yangu tukufu mnayajua magumu wanayopitia Watumishi wa Halmashauri

mkarimani feki

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2023
Posts
302
Reaction score
1,212
Juzi nilimsikia Waziri wa Tamisemi akisisitiza watumishi wapya walipwe stahiki zao ikiwepo pesa ya kujikimu.

Mpaka sasa halmashauri kadhaa hazijafanya hivyo, najiuliza sana hayo matamko ya viongozi wana monitor vipi, kuhakikisha yanatekelezwa?

Imagine unaripoti Halmashauri X kutoka mkoa wako, nayo inakupangia kituo chako cha kazi takribani km 150 kutoka mjini. Nauli yako, hela ya chumba cha kupanga, chakula,mavazi, kusafirisha na kununua vitu vya ndani kama gesi na godoro juu yako mwenyewe!

Vitu viko juu nauli nayo sio mchezo, serikali kuu chunguzeni hali ya watumishi huko halmashauri! wakurugenzi hawatoi hela ya kujikimu, hali ni mbaya tunaishia kulala kwa wanakijiji.
 
Pole sana halmashauri ndivyo zilivyo,wakati huo mkurugenzi hafanyi activity yoyote bila dokezo na linalipwa kwa wakati
 
TAMISEMI kuna wapigaji sana waziri mkuu tu juzi alikuwa analalamika kuna hela zinatoka hazina zinaenda TAMISEMI hazina melekezo kiufupi ni mchwa wanalitafuna taifa .
 
TAMISEMI kuna wapigaji sana waziri mkuu tu juzi alikuwa analalamika kuna hela zinatoka hazina zinaenda TAMISEMI hazina melekezo kiufupi ni mchwa wanalitafuna taifa .
itakua ni watu wa mifumo sana
 
"Serikali yangu tukufu"

Acha kuwapa Utukufu watu ambao ripoti ya CAG inawashuku wameiba.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Juzi nilimsikia Waziri wa Tamisemi akisisitiza watumishi wapya walipwe stahiki zao ikiwepo pesa ya kujikimu.

Mpaka sasa halmashauri kadhaa hazijafanya hivyo, najiuliza sana hayo matamko ya viongozi wana monitor vipi, kuhakikisha yanatekelezwa?

Imagine unaripoti Halmashauri X kutoka mkoa wako, nayo inakupangia kituo chako cha kazi takribani km 150 kutoka mjini. Nauli yako, hela ya chumba cha kupanga, chakula,mavazi, kusafirisha na kununua vitu vya ndani kama gesi na godoro juu yako mwenyewe!

Vitu viko juu nauli nayo sio mchezo, serikali kuu chunguzeni hali ya watumishi huko halmashauri! wakurugenzi hawatoi hela ya kujikimu, hali ni mbaya tunaishia kulala kwa wanakijiji.
Mm mwenyewe niliripoti kazini mwezi wa 5 mwaka huu lakini mpaka sasa sjalipwa hela ya kujikimu
 
Back
Top Bottom