Serikali yaombwa kumchunguza Mrisho Gambo juu ya utata wa Ufisadi wa kutisha alioufanya Arusha

Serikali yaombwa kumchunguza Mrisho Gambo juu ya utata wa Ufisadi wa kutisha alioufanya Arusha

Joined
Jul 19, 2020
Posts
39
Reaction score
128
Mradi wa bodaboda 2017 - 2020 pesa za wadau wa maendeleo gambo na genge lake walikusanya bila kamati pikipiki 200 kila moja 2,100,000. Bila kamati na kwenye kampeni alisema pesa ziko bank kwenye account ya NMB na paka Sasa azipo na hakuna kilicho fanyika mtu uyu aivumiliki na akisema ya watu wengine watu wanaona kinya na kichefu chefu kua iyo haki anatoa wapi uyu tapeli wa kisiasa arusha jiji

Mtu uyu alishawahi hujumu pesa za rambi rambi kwenye msiba wa ajali ya lack visent kuchangishwa bila kamati zaidi ya ml300 tunataka uyu mtu ashunguzwe

Wanawake 600 wa jiji mikopo ya laki 2 kila mmoja chanzo wadau pesa za wadau kwake yeye bila kamati kwa uwazi na paka Sasa uo mradi kauhujumu atujui izo pesa ziko wapi swali je wadau walimchangia yeye au wamama wa jiji la arusha Yani laki 2 Mara 600 ziko wapi atoke adharani aseme ziliko pesa za wamama

Ujenzi wa yumba za polisi bila kamati chanzo za pesa wadau na paka Rais jpm aligoma kukagua na kutoa cheti Cha pongezi kwa wadau

Kituo cha polisi utali chanzo wadau pesa bila kamari yeye na genge lake

Msikiti murueti pesa wadau bila kamati yeye akiwa kiongozi wa serekali na genge lake

Kituo cha polisi murueti pesa za wadau bila kamati yeye na genge lake

Mabati feki 200 murieti bila kamati paka ikaleta ugovi na DC jiji na yeye kama RC kipindi icho

Tunataka uchunguzi wa shule ya mrisho gambo pesa za wadau bila kamati yeye na genge lake paka jina la shule kuletwa bila utaratibu wala kikao cha jiji kupitisha.

Timu ya mpira wamigu ya arusha uneted pesa wadau bila kamati na paka timu imeuzwa kinyamela.

LESENI za wafanya biashara WADOGO wamadini 100 walio changiwa kupata LESENI na mafisadi wamadini bila kamati MUHUSIKA yeye na ndio maana paka sasa anakosa utamu wahoja Ata utetezi wake bungeni kwenye sekta ya MADINI anakosea kutetea UFISADI wake.

SOKO la samunge kuchomwa Moto na ujenzi kufanyika kinyamela pesa wadau bila kamati.

Mwsho ayo yote Akuna ushirikishwaji niyeye na genge lake la ndani ya chama na serekali lawapanga safu ndani ya chama paka Sasa arusha jiji.

Swali langu a napata haki wapi kumlaumu mtu au kiongozi yeyote jiji kwa Sasa kwa lolote tena wazi adharani bila ushaidi wala kufata taratibu na kanuni za vikao vya jiji.

Mtu uyu ni joka kuu kwenye jiji letu tunataka na yeye kwa Sasa achunguzwe kwanza.

Hapo ziko pesa nyingi Sana anatakiwa azitapike ili miradi ya maendeleo kwa wananchi iwe salama.
 
TUNATAKA MRISHO MASHAKA GAMBO ACHUNGUNZWE

Walileta mgogoro wa ujenzi wa stendi kubwa Arusha akiwa yeye na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha Jiji mpanga safu mwenzake wamenunua viwanja kwa siri wakilazimisha Serikali inunue maeneo yao kwa ajili ya kujenga stend ya arusha jiji ambayo paka Leo aipo aijajengwa sababu ni yeye akiwa RC na ndio sababu za kuleta choxhocho za kumfitini mkulugezi maden na DC daqaro apa arusha na kama serekali inataka ushaidi wakaletwe apa CD Madeni na DC Daqaro ushaidi uko wazi mwinzi kiongozi wa jiji ninani paka Sasa tunavyo ongea.

Swali langu au jibu anatoa wapi ujasiri wakuita wengine wezi nakuwafukuza kazi wakati yeye ndio mualifu mkuu paka sasa.

Tunataka kuona Serikali ikiwa makini na mtu huyu na sio vinginevyo kwenye jiji letu la Arusha.

Kusimamia ufisadi wa vibanda 395 vilivyopo stand ndogo Arusha ambavyo ni mali halali ya halimashauri ya Jiji la Arusha. Huku akifahamu vibanda vile vilijengwa kwa makubaliano ya waliovijenga kuvitumia bure kabisa kwa miaka kumi Ili kurejesha gharama zao, aliitisha kikao katika ukumbi wa mkuu wa mkoa na kuwabatiza mafisadi ambao wengi hawakujenga vibanda hivyo kwamba ni "wawekezaji wajenzi" huku akijua si kweli. Kwa hatua hiyo aliikosesha mapato makubwa sana halmashauri ya Jiji la Arusha.

Akiwa mkuu wamkoa wa Arusha huku akijua ni jukumu lake kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama, kuhakikisha wananchi na mali zao ni salama, aliruhusu wawekezaji hao wajanjawajanja KUHARIBU mali za wafanyabiashara, kuvunja na kuiba Mali, kufungia maduka mengi bila sababu za MSINGI na kinyume na utaratibu huku wafanyabiashara hao wakiwa wamelipa kodi. Kuingilia kazi za mkurugenzi wa Jiji, pia wawekezaji wajenzi hao walipuuza amri halali za mahakama.

Swala hili mpaka leo limeendelea kuleta sintofahamu, na kushindikana kufanyika maboresho eneo hilo Kwa maslah mapana ya wakazi wa Arusha. Wakati huo wafanyabiashara halali wamebaki wakiwa na waswas na biashara zao huku wakitishiwa Sana na wajenzi hao FEKI. Serkali ifanye uchunguzi yakinifu kuhusiana na swala hili. Live pls

Sipendi ujinga uyu mtu anatoa wapi ujasiri wakubeza wenzio kwenye jiji la arusha wakati yeye Dunia inajua ni tatizo

Sina hatia kama anajiamini atoke adharani yeye na genge lake la wapanga safu Ccm arusha jiji na wale walioko serekali na kamchezo kao kakulindana tunataka achunguzwe.
 
Mnafeli,

Mpaka awaumbue ndio nanyi mrudishie?

Mlikua wapi kwa ubadhirifu ambao mnadai Gambo aliufanya toka 2017?

Jinai haifi kama mko serious na mnaushahidi wa ubadhirifu mnaodai umefanywa na Gambo mpelekeni mahakamani.
 
Umeamua kumchafua baada ya kuwaumbua na ubadhirifu mnaoufanya hapo Arusha,umechelewa....
 
.....CHEAP POLITICS........

UMMA WA WATANZANIA UMEPATA BAHATI MBAYA SANA KUPATA WANASIASA WA HOVYO SANA....YAANI BAADA YA KUSHUGHULIKIA TAARIFA YA UBADHIRIFU WAO WANASHINDANA KWA UCHAFU......


IMAGINE HAWA NDIO THINK TANK KWENYE VYAMA.....
 
he is too emotional ndo chanzo kikuu cha kushindwa kupresent hoja zake lkn nafikiri anahoja.
Ndo atulize kwanza then aipange upya hoja yake...sijui ana haraka ya nn...
Ht muda wa kutoa tuhuma zake sio sahihi, kila mtu atajua jamaa ana jibu mapigo baada ya kuumbuliwa.
 
Unafiki umezaliwa nchi hii,Kuna watu nawaambia kila siku kuwa unafiki uliumbwa hapa kwenye hii ardhi.
 
Mijizi iuwae tu ndo inayofanya maisha yanakuwa magumu kwasababu ya kuhozi Mali bila kuwa na vyanzo halali
 
Suala la Gambo lije Kama hoja nyingine kwa siku nyingine. Tunataka tujue John Pima hizo milioni moja moja anazogawa hovyo ni za kwake au za Serikali?

Tunataka tujue Kihongosi ni kweli amechukua milioni 2 na kuweka kwenye akaunti yake binafsi ni kweli?

Ikibainika kweli Pima anahonga ili kunyamazisha wanaotaka kumuumbua achukuliwe hatua za kinidhamu na maadili za utumishi wa Umma na ikibainika kweli Kihongosi amekwapua hela za wakinamama basi achukuliwe hatua za kinidhamu na CCM.

Hatuwezi kupuuzia ufisadi kwenye rasilimali za Taifa, yeyote anayefichua ni shujaa wa Taifa. Geita ufisadi wa DED ulipoibuliwa na Musukuma hakukuwa na kelele ,kwa nini iwe Nongwa kwa Gambo?

Mwaka huu Gambo kawashika pabaya ,pale panapoguswa mtu mpaka anashtuka ndo anapapapasa.
 
Back
Top Bottom