Katibu mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Profesa Sifuni Mchome amesema Serikali haijapata taarifa hiyo, na kueleza kuwa watu hao wamekamatwa kwa mujibu wa sheria.
Taarifa iliyotolewa jana katika tovuti ya shirika la Umoja wa Mataifa na Kamishina wa Shirika la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Bi. Michelle Bachelet inadai kuwa viongozi wa upinzani na wafuasi wao 150 wa Bara na Zanzibar wamekamatwa tangu Oktoba 27, siku moja kabla ya wananchi kupiga kura. Bachelet alieleza kusikitishwa na taarifa za kukamatwa kwa viongozi wa vyama vya upinzani.
Hata hivyo serikali kupitia Profesa Mchome imesema bado haijapata taarifa hiyo na kama ni madai ya watu kukamatwa ni kwa mujibu wa sheria.
“Inawezekana kweli wanaongelea Watanzania, lakini inaweza kuwa ni umbea,” alisema Profesa Mchome.
“Kama watu wamekamatwa ni kwa kuvunja sheria na kama amekamatwa kutakuwa na kitu wametuhumiwa na kama ni hivyo wana nafasi ya kujieleza, waliomkamata wakiridhika wanamwachia. Huo ndio utaratibu wa kisheria.”
Taarifa ya Umoja wa Mataifa hii hapa.
www.jamiiforums.com
Taarifa iliyotolewa jana katika tovuti ya shirika la Umoja wa Mataifa na Kamishina wa Shirika la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Bi. Michelle Bachelet inadai kuwa viongozi wa upinzani na wafuasi wao 150 wa Bara na Zanzibar wamekamatwa tangu Oktoba 27, siku moja kabla ya wananchi kupiga kura. Bachelet alieleza kusikitishwa na taarifa za kukamatwa kwa viongozi wa vyama vya upinzani.
Hata hivyo serikali kupitia Profesa Mchome imesema bado haijapata taarifa hiyo na kama ni madai ya watu kukamatwa ni kwa mujibu wa sheria.
“Inawezekana kweli wanaongelea Watanzania, lakini inaweza kuwa ni umbea,” alisema Profesa Mchome.
“Kama watu wamekamatwa ni kwa kuvunja sheria na kama amekamatwa kutakuwa na kitu wametuhumiwa na kama ni hivyo wana nafasi ya kujieleza, waliomkamata wakiridhika wanamwachia. Huo ndio utaratibu wa kisheria.”
Taarifa ya Umoja wa Mataifa hii hapa.
Uchaguzi 2020 - Geneva: UN Rights Chief disturbed by harassment of opposition following Tanzania elections
OHCHR | UN rights chief disturbed by harassment of opposition following Tanzania elections GENEVA (10 November 2020) – UN High Commissioner for Human Rights Michelle Bachelet on Tuesday said she was disturbed by reports of continued intimidation and harassment against opposition leaders and...