Serikali yasitisha tozo ya Tsh 100 kwa kila lita ya mafuta, yasema itapoteza Sh bilioni 30 kwa mwezi

Serikali yasitisha tozo ya Tsh 100 kwa kila lita ya mafuta, yasema itapoteza Sh bilioni 30 kwa mwezi

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia kwa sababu mbalimbali ikiwemo vita ya Urusi na Ukraine, Serikali ya Tanzania imetangaza kuondoa Tozo ya Sh 100 kwa kila lita katika Dizeli, Petroli na Mafuta ya Taa kwa miezi mitatu.

Wizara ya Nishati imetangaza maamuzi hayo ambapo utekelezaji wake unatarajiwa kuanza Machi 2, 2022 huku tathimini ya mwenendo wa soko la dunia ikiendelea.

Maamuzi hayo yataipunguzia Serikali mapato ya Sh bilioni 30 kwa mwezi. Bei mpya zitatangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).

1b36c872-5322-419a-a06d-b9f48e6dff71.jpg

 
Kutokana na kuendelea kupanda kwa Bei za Mafuta katika Soko la Dunia, Serikali imeondoa Tozo ya Tsh. 100 kwa kila Lita ya Dizeli, Petroli na Mafuta ya Taa zilizopaswa kulipwa kwa miezi mitatu zaidi, kuanzia Machi hadi Mei 2022

Kupanda kwa bei kumetokana na sababu mbambali ikiwemo vita kati ya Urusi na Ukraine. Serikali imesema Bei mpya za mafuta zitakazoanza kutumika Machi 02, 2022 zitazingatia marekebisho hayo

9FDFBB60-C331-4E39-A60F-AE8493E88045.jpeg
 
Kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia kwa sababu mbalimbali ikiwemo vita ya Urusi na Ukraine, Serikali ya Tanzania imetangaza kuondoa Tozo ya Sh 100 kwa kila lita katika Dizeli, Petroli na Mafuta ya Taa kwa miezi mitatu.

Wizara ya Nishati imetangaza maamuzi hayo ambapo utekelezaji wake unatarajiwa kuanza Machi 2, 2022 huku tathimini ya mwenendo wa soko la dunia ikiendelea.

Maamuzi hayo yataipunguzia Serikali mapato ya Sh bilioni 30 kwa mwezi. Bei mpya zitatangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).

View attachment 2134065
Serikali imechelewa kuzifuta tozo mbalimbali ilizojiwekea kwani ni kikandamizaji dhidi ya wananchi wake na zilipitishwa na bunge bila kuangalia athari kwa jamii.
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Kakope tena Mama maana haijulikani hivi vita vitaisha lini na baada ya kuisha, mikopo itatolewa kwa mtindo UPI na kwa riba IPI!!
 
Inapotezaje billion 30 wakati hizo ni pesa zetu walikua wanatuibia??????

Walikurupuka kuweka hii tozo kandamizi kisa tu waliona bei za mafuta zimeshuka wakaona tunafaidi sana kumbe punguzo hilo lilitokana na soko la dunia kuporomoka kwasababu ya Korona.
 
Inapotezaje billion 30 wakati hizo ni pesa zetu walikua wanatuibia??????

Walikurupuka kuweka hii tozo kandamizi kisa tu waliona bei za mafuta zimeshuka wakaona tunafaidi sana kumbe punguzo hilo lilitokana na soko la dunia kuporomoka kwasababu ya Korona.

Ni kawaida kwa majizi kuhesabu mali za watu kama zao
 
ivi tz si tunamafuta, hatuwez kuchakata yakwetu au shida iko wapi
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Mwakatozo mwakapuyanga ulaya na Dubai, mwaka huu mwafwaaaaaaaaaaaaaaaaa, ngoja tuendelee kubeba boksi hakuna namna walay
 
Wanasitishiana tozo za matajiri tu za wanyonge zinaachwa palepale
Kuna mnyonge,asiyetumia petrol,disiel na mafuta taa?Kama hana gari,atapanda bodaboda pikipiki,bajaji,daladala,atakula samaki wanaovuliwa kutumia mashine zinazotumia petrol.Atatumia kuni,mkaa bidhaa mbalimbali,bidhaa za sokoni:nyanya,nazi,ndimu,limau,bamia nk vinavyobebwa na magari yanayotumia dizeli.Mafuta ya taa ,atatumia kwenye taa,kutumia jiko la mafuta,kuwasha moto wa kuni au mkaa.
 
  • Thanks
Reactions: MCN
Mimi nikishaona tu naniliu nakuwa nanusa harufu ya upigaji tu🐒
 
Mwenye gari nae ni mnyonge?
Mafuta hayatumiki kwa wenye magari tu,hata asiye na gari anayatumia,ukipanda pikipiki bodaboda,ukipanda bajaji,ukipanda daladala, bus,unatumia mafuta.Ukinunua bidhaa yoyote ujuwe mpaka imekufikia wewe karibu yako,kumetumika mafuta.Ukiona nyanya,kitunguu,nazi,pilipili,mchicha,sembe,ngano nk,vimefika ulipo,ni.mafuta yametumika kwa ajili ya wewe uvipate.jengo lolote,unalotumia kwa makazi,masomo,afya,kumetumika usafiri wa kufanya liwepo hapo ilipo.Mwanao,ndugu,wewe mwenyewe,shule uliyosoma bila mafuta isingekuwapo hapo ulipo.
 
Back
Top Bottom