Serikali yatenga Shilingi Bilioni 34 kujenga Makumbusho ya Marais Dodoma

Serikali yatenga Shilingi Bilioni 34 kujenga Makumbusho ya Marais Dodoma

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imetenga Tsh. bilioni 34 kwa ajili ya mradi wa makumbusho ya Marais ambao utajengwa Dodoma ili kuweka historia na kumbukumbu za Viongozi hao.

Rais Samia amesema hayo Jijini Dar es salaam leo September 30,2024 wakati akizindua kitabu cha Sokoine (Maisha na Uongozi wake).

"Nataka nizungumzie pendekezo lililotolewa na Balozi Sokoine kwamba kuwe na kituo mahususi cha kuweka historia na kumbukumbu za Viongozi, nataka nitoe taarifa kwamba pendekezo hili limeanza kufanyiwa kazi, kuna mradi wa makumbusho ya Marais, mradi huu ni mradi namba 5221 eneo liko Mumba na tumetenga Tsh. bilioni 34 kwa ajili ya mradi huu na mwaka huu tumeanza kutenga bajeti ndogo kama bilioni 1 na kitu na eneo lile lina ukubwa wa ekari 50 pale Dodoma kwahiyo hili tunalifanyia kazi" — Rais Samia.

Chanzo; Millard Ayo
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imetenga Tsh. bilioni 34 kwa ajili ya mradi wa makumbusho ya Marais ambao utajengwa Dodoma ili kuweka historia na kumbukumbu za Viongozi hao.

Hii habari ipo kwenye ilani ya CCM 2020-2025?
Au ni kipaumbele cha serikali?
 
mh! kuna muda mnatuchanganya sana!..
mnaendaga huko nje kufata mikopo ili mje mfanye mambo yenye kuleta tija maana nchi yetu bado ipo ktk ombwe la umasikini,hatujafika hizo hatua za kuweka makumbusho ya marais kwa gharama za mabillion ya pesa!.
ikiwa bado tunashida lukuki zakutatua kwanini pesa hizo zisipelekwe kwenye miradi yenye tija kwa jamii..?
tukianza kuwasema hovyo mitandaoni mtuteke,mtunyanyase kwa kutubinya kendelelo!.

WTF!
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imetenga Tsh. bilioni 34 kwa ajili ya mradi wa makumbusho ya Marais ambao utajengwa Dodoma ili kuweka historia na kumbukumbu za Viongozi hao.

Rais Samia amesema hayo Jijini Dar es salaam leo September 30,2024 wakati akizindua kitabu cha Sokoine (Maisha na Uongozi wake).

"Nataka nizungumzie pendekezo lililotolewa na Balozi Sokoine kwamba kuwe na kituo mahususi cha kuweka historia na kumbukumbu za Viongozi, nataka nitoe taarifa kwamba pendekezo hili limeanza kufanyiwa kazi, kuna mradi wa makumbusho ya Marais, mradi huu ni mradi namba 5221 eneo liko Mumba na tumetenga Tsh. bilioni 34 kwa ajili ya mradi huu na mwaka huu tumeanza kutenga bajeti ndogo kama bilioni 1 na kitu na eneo lile lina ukubwa wa ekari 50 pale Dodoma kwahiyo hili tunalifanyia kazi" — Rais Samia.

Chanzo; Millard Ayo
Kwanza swali la msingi la kujiuliza, hivi hiyo proposal imepita Bungeni??

Au ndiyo kama kawaida yake Mama, kugawa pesa za walipa Kodi wa nchi hii kama njugu?🙄

Kama anavyofanya wakati huu za kulipa magoli ya Simba na Yanga, milioni 5 Kwa pesa zetu walipa Kodi!😭
 
Kwanza swali la msingi la kujiuliza, hivi hiyo proposal imepita Bungeni??

Au ndiyo kama kawaida yake Mama, kugawa pesa za walipa Kodi wa nchi hii kama njugu!🙄
Hii nchi ni ngumu kwa kweli👋
 
Mchungaji ameona mbali na huu ni ukweli 100%
 
Mchungaji ameona mbali na huu ni ukweli 100%
Hakika hii nchi inakokwenda ni kubaya sana!

Kama wakubwa wanaamua kufuja Kwa hali ya juu kiasi hicho, pesa zetu za walipa Kodi, basi ni hatari sana!😭
 
34B kujenga makumbusho safi sana lakini je, ni kipaumbele chetu kwasasa?
Mahitaji tunayo mengi tena sana ni muhimu kuanza na ya lazima kisha yafuate ya muhimu!
 
Serikali imetenga Shilingi bilioni 34 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Makumbusho ya Marais nchini, unaotarajiwa kujengwa katika eneo la Mtumba, Dodoma. Mradi huo utatekelezwa kwenye eneo lenye ukubwa wa ekari 50 na unalenga kuhifadhi kumbukumbu za viongozi wakuu wa nchi pamoja na historia ya taifa.

Akizindua kitabu cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine (MAISHA NA UONGOZI WAKE) JNICC, Jijini Dar es Salaam Rais Samia amesema kwa kuanza mwaka huu zimetengwa zaidi ya Sh. Bilioni 1 ili kuanza utekelezaji.

Hawa viongozi ni bure wenzao maktaba za maraisi zinatokana na michango na sio pesa za serikali
 
Serikali imetenga Shilingi bilioni 34 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Makumbusho ya Marais nchini, unaotarajiwa kujengwa katika eneo la Mtumba, Dodoma. Mradi huo utatekelezwa kwenye eneo lenye ukubwa wa ekari 50 na unalenga kuhifadhi kumbukumbu za viongozi wakuu wa nchi pamoja na historia ya taifa.

Akizindua kitabu cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine (MAISHA NA UONGOZI WAKE) JNICC, Jijini Dar es Salaam Rais Samia amesema kwa kuanza mwaka huu zimetengwa zaidi ya Sh. Bilioni 1 ili kuanza utekelezaji.
Vimiradi visivyo na maana ndio vinapewa pesa.

Makumbusho ya Taifa ipo Kwa nini hao Marais kumbukumbu zao zisitunzwe kule?
 
Back
Top Bottom