Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahahaja haya banaa acha wanasiasa sisi tunapasuana bureeStudy gani hapo unaongelea wee kolo???
Umenikumbusha lile swali maarufu kule Dom, " wapi mbali kati ya Dodoma na Tanzania".Wapi mbali, kati ya kutoka stiglazi goji mpaka kasakazini na kutoka Ethiopia hadi kasakazini ?😏
Wanatumia ujinga kama mtaji, kwani mtawafanya niniNaam kama kawa kama dawa, Wazee WA UFAFANUZI wameshatoa UFAFANUZI kuwa umbali wa kutoka Ethiopia Hadi Same ni mfupi kuliko Mwalimu Nyerere Hydro Power pale Rufiji Hadi Same
Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini
View attachment 3264882View attachment 3264881
Boss unamaanisha kuwa Bwawa la Rufiji imeua kabisa uzalishaji wa mabwawa kama Pangani, Hale, Nyumba ya Mungu? Umeme kutoka Ethiopia inafanya nini hapo Kenya mpakani 200km kutoka Tanzania?Kwa heri....unajua gharama kusafirisha 33KV to km 600? Acheni fani zacwatu sio siasa hiii....kwa heriii
Kuna nguzo zinaonekana kati ya Chalinze na Tanga je kwanini hizo zisitumike kusafirisha umeme kutoka chalinze kwenda huko Kasakazini sawa tu na hizo zilizoko Kenya?Gharama za kusafirisha umeme kwa umbali huo ni kubwa mno ukilinganisha na kuuchukulia hapo kenya .
Wanaposema umeme wa Ethiopia haina maana uko huko Ethiopia! Ni uko hapo jilani kenya wastani wa km 250km~300km tu
Hivyo ukichukulia gharama za kuusafirisha umeme kwa wastani 50mil kwa kila span moja ( nguzo moja hadi nyingine) hapa tutazungumzia wastani wa span elf 8000 hadi 9000 endapo utaamua kuutoa mikoa ya rufiji!
Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini
Mbali na gharama hizo mradi mkubwa kama huo unahitaji kulipa watu fidia na kuchepusha miundombinu itayoingiliana hapo katikati ya mradi!
View attachment 3265028
Wakuu pesa tuliyotumia kama taifa kusomesha wasomi imeleta laana kwa taifa. Umbali wa kutoa umeme maeneo ya kusini imeonekena ni kazi Bure kwani katika hatua ya kusafirisha umeme kutoka Mtera ama Bwawa na la Nyerere kuupeleka mikoa ya kasikazini umeme unapotea sana. Sasa sijajua labda kwa sababu ya friction ama heating effects ama drift velocity ama kitu Gani kinafanya voltages zipotee hapo njiani. Nakubali Kuna factors zinapelekea umeme unaozalishwa na unaofika site Huwa unatofautiana lakini si kwa kiwango Cha kuamua kununua umeme kutoka Ethiopia kilomita zaidi ya Elfu 2 na kuacha kuchukua umeme uliopo kilometa 600. Haya ni maajabu. Lazima tuelewe watanzania tuna maisha magumu Sana na haya mambo yanatuumiza sana.
Taarifa yenyewe hii hapa ni ndefu kinyama...
Serikali imetolea ufafanuzi kauli iliyotolewa na Rais Samia leo kwamba Serikali itanunua umeme maalum kwa ajili ya Mikoa ya Kanda Kaskazini ili umeme usikatikekatike ambapo imesema umeme uliopo katika Gridi ya Taifa unazalishwa kutoka ukanda wa Kusini Mashariki na hivyo kulazimika kusafirishwa umbali mrefu kwenda maeneo mbalimbali nchini hali inayosababisha upotevu mkubwa wa umeme.
Taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari Maelezo na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali leo March 09,2025 imesema “Kwa Kanda ya Kaskazini upotevu wa umeme unaosafirishwa umekuwa ukisababisha hasara ya zaidi ya Tsh. bilioni 32 kwa mwaka, kutokana na upotevu huo na usafirishaji mrefu wa umeme, Kanda ya Kaskazini imekuwa ikikabiliwa na changamoto kubwa ya kukatika kwa umeme mara kwa mara hali ambayo inawaathiri Wananchi”
“Ununuzi wa umeme kutoka Ethiopia kupitia Kenya utasaidia kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara na kuokoa upotevu mkubwa wa umeme unaokwenda katika kanda hiyo, gharama za umeme unaonunuliwa kutoka Ethiopia ni nafuu kutokana na Tanzania kuwa mwanachama wa Gridi ya Umeme ya Ukanda wa Kaskazini mwa Afrika ambapo nchi zina makubaliano ya kuuziana umeme kwa gharama nafuu ambayo inalingana ama ni chini ya gharama za uzalishaji umeme zilizopo sasa hapa Tanzania kwa baadhi ya vyanzo vyetu”
“Utaratibu wa Tanzania kununua umeme kutoka nchi jirani umekuwa ukifanyika tangu miaka mingi hususani Mikoa ya pembezoni ambayo ni Rukwa (kutoka Zambia) Kagera (kutoka Uganda) na
Tanga (kutoka Kenya), lengo kuu la kununua umeme kwa ajili ya maeneo ya pembezoni mwa nchi ni kuimarisha Gridi ya Taifa na kuiwezesha nchi kuwa na njia mbadala ya kupata nishati ya umeme pale kunapotokea changamoto katika Gridi ya Taifa.
Upigaji mkubwa sana.🤣🤣 Kuna harufu ya upigaji hapa
Mama yule ni mwi..ziUpigaji mkubwa sana.
Pole sana kwa msiba ndugu.Hii inaitwa hiishi mpaka iishe tena! Ufafanuzi bado unahitaji ufafanuzi, sasa sijui ufafanuzi wa awamu ya pili utakuwaje huu ulikuwa wa maandishi! Labda ujao uwe kwa mahojiano. Aidha, tunayo-pool of Electrical Engineers hapa nchini tena wengine ni PhD holders wabobevu kwenye tafiti. Si kungefanyika project ya uvumbuzi kukabiliana na upotevu mkubwa huo wa umeme angalau upotevu ufikie asilimia 0.0005 ya upotevu wa sasa?
Nimejaribu kuwaza tuu! Au kama vipi tuwaite marafiki zetu wa damu wachina tuwape mchongo huo. Tuone show itakavyokuwa hapo!
Usiku mwema aisee nipo kwenye majonzi, nimepatwa msiba bado hatujazika ila hili nalo linanifanya nigawanye majonzi kidogo ya msiba nilionao.
Sawa watatumia...kama wataona hazina kazi....Kuna nguzo zinaonekana kati ya Chalinze na Tanga je kwanini hizo zisitumike kusafirisha umeme kutoka chalinze kwenda huko Kasakazini sawa tu na hizo zilizoko Kenya?
Shukrani sanaa Mkuu!Pole sana kwa msiba ndugu.
😆😆😆😆😆Nakuona unasoma UFAFANUZI
Yes Hadi kule Mambwe mkoswe HAKUNA upumbavu wa umeme kukatikaMkoa wa Rukwa wasije wakaonganisha umeme Grid ya Taifa. Umeme kutoka Zambia haukatiki wala hakuna mgao wa umeme.
Kama rais Samia angekuwa ndiyo Mungu basi Tanzania ingekuwa ni nchi takatifu iliyobarikiwa sanaNdugu zangu Watanzania,
Serikali yetu tukufu chini ya uongozi mahili,imara ,madhubuti ,shupavu na wenye kuleta matumaini kwa watu wa Dkt Mama Samia Suluhu Hasssan Mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge.
Kupitia msemaji mkuu wa serikali Mheshimiwa Gerson Msigwa Imetoa ufafanuzi wa kina wa sababu ya kununua umeme Nje ya Nchi kwa ajili ya kanda ya kaskazini.
Soma hapa[emoji107]View attachment 3264895View attachment 3264896
Huu ufafanuzi wa serikali unagongelea misumali ya moto kwenye jeneza la ma-ccm.Huu ufafanuzi ni nonsense.Naam kama kawa kama dawa, Wazee WA UFAFANUZI wameshatoa UFAFANUZI kuwa umbali wa kutoka Ethiopia Hadi Same ni mfupi kuliko Mwalimu Nyerere Hydro Power pale Rufiji Hadi Same
Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini
Naaaaaam naaaaaam naaaaaamHuu ufafanuzi wa serikali unagongelea misumali ya moto kwenye jeneza la ma-ccm.Huu ufafanuzi ni nonsense.
Mimi nimesha andaa nyundo, Oktoba 2025 tunagongelea na kuizika ccm.