Service Levy ya halmashauri ya jiji Temeke sasa ni kodi ya ujenzi wa madarasa na barabara

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Mimi ni mfanyabiashara, nwishoni mwa mwaka jana niliwekwa mahabusu kwa kukataa kulipa tozo ya kuzoa takataka za wamachinga!

Kukataa kwangu kulitokana na kuamini kodi hiyo ya huduma ni kwa ajili ya uzoaji takataka na huduma nyingine, hatahivyo niliambiwa kwa sasa kodi hiyo ni kwa ujenzi wa barabara na madarasa tu ndiyo sababu wameanzisha tozo za usafi, tozo hii hutozwa wenye fremu za maduka huku wazalishaji wa taka ambao ni wamachinga wakisamehewa kama ambavyo wanavyosamehewa kushiriki siku za usafi.

Swali langu ni nani mwenye jukumu la kukusanya pesa za ujenzi wa barabara na madarasa na utitiri wa kodi kwa wafanyabiashara nini sulihisho lake?
 
Hii nchi uhuni ni mwingi ndio maana huwa sitoi lawama kwa mtu anayejitahidi kukwepa kodi
 
Mzee ulishaambiwa ukiona yamekushinda hamia Burundi
 
Jina kamili kampuni ni JTM ENTERPRISES with no fixed abode!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…