Seti Mbili za Treni ya Umeme na vichwa 8 vya Umeme "Samia Express" vyawasili Nchini

Seti Mbili za Treni ya Umeme na vichwa 8 vya Umeme "Samia Express" vyawasili Nchini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-07-02 at 10.20.23_92845e9b.jpg
SETI MBILI ZA TRENI ZA EMU (ELECTRIC MULTIPLE UNIT) ZAWASILI

Dar es Salaam, Tarehe 02 Julai, 2024

Shirika la Reli Tanzania - TRC linautaarifu umma kuwa Seti mbili (2) za treni ya kisasa inayotumia nishati ya umeme EMU (Electric Multiple Unit) na vichwa nane (8) vya treni vya umeme vimewasili Tanzania kutoka nchini Korea ya Kusini.

Serikali kupitia TRC ilifanya manunuzi ya Seti kumi (10) za treni za EMU zinazotengenezwa na kampuni ya Hyundai Rotem ya nchini Korea Kusini, Seti moja ya EMU ina jumla ya mabehewa nane yakijumuisha kichwa kimoja mbele na kingine nyuma ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 589 na kutembea kwa kasi ya kilomita 160 kwa saa.

Seti mbili (2) za EMU zinafikisha idadi ya seti tatu zilizowasili nchini mpaka sasa, seti ya kwanza iliyowasili mwezi Aprili 2024 inaendelea na majaribio.

Shirika la Reli Tanzania limeshapokea jumla ya mabehewa 65 ya abiria, vichwa 17 vya umeme na Seti tatu za EMU. Upokeaji wa vifaa vya uendeshaji vya reli ya kiwango cha SGR unaendelea kwa awamu tofauti, vifaa vipya vilivyowasili vitaendelea kufanyiwa majaribio kwaajili ya kujiridhisha kabla ya kuanza kutoa huduma.

Shirika linaendelea na uendeshaji wa awali na utoaji huduma ya usafiri wa treni za umeme kupitia reli ya kiwango cha kimataifa kati ya Dar es Salaam na Morogoro, uendeshaji rasmi kati ya Dar es Salaam hadi Dodoma unatarajiwa kuanza Julai 25, 2024.

Jamila Mbarouk Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano

EMU 4.jpeg.jpg

EMU 5.jpeg.jpg

EMU 1.jpeg.jpg
 
Hongera Sana Kwa Serikali , Wizara Husika, Shirika la Reli na Wadau wengine, inatia moyo sana kuona Maendeleo makubwa kama haya katika kipindi hiki Cha mitikisiko ya uchumi Kila Kona ya Dunia.
 
My Take
Kilichonifurahisha no jina la treni hiyo ya haraka yenye kichwa Mchongoko (Electric Multiple Unit) kuitwa "Samia Express "

Kazi iendelee, Samia anaweza na chenji inabaki

20240702_215520.jpg
---
1719939798225.png
Shirika la Reli Tanzania - TRC linautaarifu umma kuwa Seti mbili (2) za treni ya kisasa inayotumia nishati ya umeme EMU (Electric Multiple Unit) na vichwa nane (8) vya treni vya umeme vimewasili Tanzania kutoka nchini Korea ya Kusini.

Serikali kupitia TRC ilifanya manunuzi ya Seti kumi (10) za treni za EMU zinazotengenezwa na kampuni ya Hyundai Rotem ya nchini Korea Kusini, Seti moja ya EMU ina jumla ya mabehewa nane yakijumuisha kichwa kimoja mbele na kingine nyuma ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 589 na kutembea kwa kasi ya kilomita 160 kwa saa.

Seti mbili (2) za EMU zinafikisha idadi ya seti tatu zilizowasili nchini mpaka sasa, seti ya kwanza iliyowasili mwezi Aprili 2024 inaendelea na majaribio.

Shirika la Reli Tanzania limeshapokea jumla ya mabehewa 65 ya abiria, vichwa 17 vya umeme na Seti tatu za EMU. Upokeaji wa vifaa vya uendeshaji vya reli ya kiwango cha SGR unaendelea kwa awamu tofauti, vifaa vipya vilivyowasili vitaendelea kufanyiwa majaribio kwaajili ya kujiridhisha. kabla ya kuanza kutoa huduma.

Shirika linaendelea na uendeshaji wa awali na utoaji huduma ya usafiri wa treni za umeme kupitia
reli ya kiwango cha kimataifa kati ya Dar es Salaam na Morogoro, uendeshaji rasmi kati ya Dar es Salaam hadi Dodoma unatarajiwa kuanza Julai 25, 2024.👇👇

View: https://youtu.be/eHtBXgyF9pA?si=uY6HtxON0Uvmgt_5
 

Attachments

  • 20240702_194645.jpg
    20240702_194645.jpg
    188.6 KB · Views: 7
Back
Top Bottom