SGR na uwekezaji mkubwa wa viwanda Tabora, Dodoma, Singida, Morogoro, Shinyanga

SGR na uwekezaji mkubwa wa viwanda Tabora, Dodoma, Singida, Morogoro, Shinyanga

Nakubaliana na kauli hii, lakini pamoja na kuwa swala kuwa letu, serikali haiwezi kamwe kujiondoa katika hatua hiyo ili kufanikisha hizo shughuli za wananchi, kwa mfano ruzuku ya mbolea na maswala mengi mengine katika shughuli hizo.
Sasa labda ungeainisha baada ya Sirikali kuwekeza hivyo vikubwa ambavyo Mimi na wewe hatuwezi, hayo mengine ambayo yamekuwa kikwazo kwako kufungua kiwanda au kulima ni nini.useme Una Ardhi sehemu fulani, na umeshindwa kulima sababu ya mbolea au hayo mengine.
 
Tunaagiza kwa sababu watanzania kwa asili hawapendi kazi na hawapendi kujitumia na wala hawajihangaishi kutafuta fursa. Hizo sekta zote ulizotaja Watanzania wanafanya kazi kimazoea na wanaridhika mapema sana hivyo uzalishaji unakuwa chini ukilinganisha na mahitaji ya soko.

Hadi dunia ya leo wanafuga kwa kuangalia idadi ya mifugo bila kuianzia ubora na hawataki kufuga mifugo michache yenye ubora wa soko.

Ukija kwenye mazao bado tunalima kijadi kabisa. kijishamba kila kina aina ya mazao hadi unashindwa kujua huyu mtu analima zao lipi hasa. Hongera kwa akulima wa Mpunga angalau uzalishaji umepanda ingawa nako tija ni ndogo kutokana na matumizi ya pembejeo yasiyokidhi viwango na matumizi mabaya ya viauatilifu na mbolea.

Hii nchi changamoto inaanzia kwa wananchi wake.
Ndugu yangu inashangaza sana mpaka Karne hii Wenye mitaji bado wanachuana na wajasiliamali wadogo wadogo kununua bidhaa na kuleta kuziuza huku, Badala ya kuimport mashine za kuzalisha bidhaa hizo ili tuzalishie nyumbani wawo wabaki wazalishaji wakubwa ikiwezekana exporter wakubwa, Bado tunaagiza toothpick na mianzi tunayo,embu fikiria muanzi mmoja unazalisha toothpick ngap?, Bado tunaagiza maelf na maelf ya pampas na mali ghafi zipo na inasemekana hivi vitu huzalishwa na Medium mashine kabisa unafikiri huyo Mkulima utamkomboa vipi?
 
Nina hofu kubwa sana na reli hiyo.
Pengine ni kwa kutojuwa yanayo fanyika ndani kwa ndani na mipango ya uendeshaji wa reli yenyewe. Sina taarifa za kunipa matumaini makubwa kwamba maandalizi ya uendeshaji wa reli hiyo yamefanyika ipasavyo na hakutakuwa na matatizo yale yale tuliyo kumbana nayo miaka yote. Tukitazama mfano wa BRT..., . Hivi kutakuwepo na tofauti kubwa kati ya reli hii na huu mpango wa mjini tu hapo Dar?

Mfano wa reli iliyo jengwa na wachina, hapo jirani yetu. Uendeshaji wa reli hiyo umesimamiwa hadi sasa na wachina wenyewe, na ndio wanaowafundisha wenyeji kuendesha mradi huo wakati mkataba wao utakapo kwisha.
Wenyeji sasa wamefuzu na wanashikiria karibu nafasi zaidi ya asili mia 90 kwa sasa, na uendeshaji unakwenda vizuri.
Sisi huu wa kwetu, sijasikia kama watu wetu wamekwenda mafunzo katika uendeshaji wa reli hiyo. Sijui, kwa sababu naona mambo mengi kwetu ni kama siri ya wenyewe.
Tatizo kubwa ninaloliona nikuanzishwa huku tukiwa na malengo yale yale waliyokuwa nayo wakoloni kusafirisha Rasilimali na kuingiza bidhaa kutoka kwa wenzetu, Tujikite na kujiimalishe angalau katika kuongeza thamani Rasilimali zetu ili kuongeza base ya faida za uwepo wa reli hii hapo ndipo itagusa sector nyingi na uchumi wa watanzania wengi.
Pili nakubaliana na wewe tatizo kubwa la nchi yetu ni Management, Plan tunakuwa nazo nzuli na tatizo linakuja kwenye uendeshaji kwenye hili nazilaumu Mamlaka zetu za kuwajibishana tunaleta uswahili wa kuoneana aibu huku watu wengi watanzania wengi wakiumia.
Tatu wananchi wenyewe hakuna mfatiliaji kwanza ufisadi, Wizi, na uhuni uhuni tunauita ni ujanja, mtu mwizi utasikia mswahili anasema jamaa mjanja mjanja sana hii inawafanya hawa watu waone sifa kutuibia, Mwizi aitwe mwizi, Fisadi aitwe Fisadi unajua hata kumita mtu kwa sifa zake mbaya ni hukumu tosha na inaweza changia kumbadilisha mtu na jamii
 
Matumizi yapo hasa mizigo inayopita ndani ya nchi kwenda nchi jirani hususani DRC ambayo inabeba asilimia takribani 41 ya mizigo inayopita ktk bandari zetu.

Katika hili umuhimu wa kupereka SGR bandari ya Kigoma/Kigoma una pana kiuchumi kuliko Burundi ama Rwanda
 
Ndugu yangu inashangaza sana mpaka Karne hii Wenye mitaji bado wanachuana na wajasiliamali wadogo wadogo kununua bidhaa na kuleta kuziuza huku, Badala ya kuimport mashine za kuzalisha bidhaa hizo ili tuzalishie nyumbani wawo wabaki wazalishaji wakubwa ikiwezekana exporter wakubwa, Bado tunaagiza toothpick na mianzi tunayo,embu fikiria muanzi mmoja unazalisha toothpick ngap?, Bado tunaagiza maelf na maelf ya pampas na mali ghafi zipo na inasemekana hivi vitu huzalishwa na Medium mashine kabisa unafikiri huyo Mkulima utamkomboa vipi?

Ni aibu

Vyuo vyetu

Elimu yetu ifinyangwe kuwajenga vijana kuona na kutafsiri fulsa lukuki ktk uzalishaji kupitia viwanda vidogo na vya kati..

Lakini mazingira wezeshi ktk mifumo ya compliance za kisheria-Kodi,Leseni,Vibali etc
 
Nakubaliana na kauli hii, lakini pamoja na kuwa swala kuwa letu, serikali haiwezi kamwe kujiondoa katika hatua hiyo ili kufanikisha hizo shughuli za wananchi, kwa mfano ruzuku ya mbolea na maswala mengi mengine katika shughuli hizo.
Hatuwezi kujikomboa kwa kutegemea kuagiza mbolea toka nje kama ilivyo kwa Sukari..

Tujenge uwezo zaidi kwa wazalishaji wa ndani..Tuwape nafuu na incentives kitita..

Viwanda kama MINJINGU FERTILIZERS vilindwe kwa wivu mkubwa..

Kama ambavyo tunapswa kufuta uhuni unaozuia kuuzwa kwa viuatirifu vinavyozalishwa na kiwanda cha Kibaha chini ya NDC (Kilichojengwa na Wacuba)..Malaria inapaswa kuwa historia ktk nchi
 
Napongeza uwekezaji mkubwa uliofanyika ktk ujenzi wa miundombinu yenye thamani kubwa ktk nchi.

Serikali imetumia zaidi ya Tirioni 8 ktk ujenzi wa SGR..Kilichofanyika ni uwekezaji wa kihistoria ulifanikishwa kwa mapato ya ndani na mikopo ya fedha yenye riba nafuu na isiyo na riba nafuu..

Tuna jukumu la kulipa mikopo na madeni yetu kwa wakati stahiki kuepuka adhabu na malimbikizo kuwa makubwa zaidi..

Ili kufanikisha ulipaji madeni husika lazima tujifunge mikanda haswaa na kuhakikisha uzalishaji na biashara zinashabihiana na mzigo wa madeni tulionayo sasa na baadae..

Treni mpya ya abiria ya kisasa inayofanya kazi ktk miundombinu ya SGR imekuwa gumzo na kivutio kwa watanzania wengi haswa safari za Dar mpaka Dodoma..Mihemuko yetu,Hisia zetu na matamanio hakika yamejaa shauku kubwa..

Nikitafakari kibiashara na ukubwa wa obligations tulizonazo ktk madeni nawiwa kushauri TRC na serikali kwa ujumla kutazama namna ya kufungamanisha maendeleo ya uchumi wa nchi na matumizi yenye tija ya uwekezaji wa SGR.Naamini hatukuwekeza tirions ili tubebe abiria..

Msingi wa uwekezaji ni kufungua collidor kwa kuwezesha usafirishaji wa bidhaa,mazao ya kilimo,Ufugaji,madini kwenda nje ya nchi (Export pia imports kwenda ndani ya nchi (Local Imports) na Transit imports.

Sasa ni wakati wa kupima maeneo ya uwekezaji wa viwanda vikubwa,Mashamba makubwa (Kilimo) kisha vigawiwe bure kwa wawekezaji wa ndani na nje ili kukuza uzalishaji kisha matumizi yenye tija
Hilo la mizigo ni lako, sisi tuko kwenye abiria ambao wanaotushangilia na ndio wapiga kura wetu.
 
Sasa labda ungeainisha baada ya Sirikali kuwekeza hivyo vikubwa ambavyo Mimi na wewe hatuwezi, hayo mengine ambayo yamekuwa kikwazo kwako kufungua kiwanda au kulima ni nini.useme Una Ardhi sehemu fulani, na umeshindwa kulima sababu ya mbolea au hayo mengine.
Nianishe nini wakati inaonyesha tayari umeelewa ninacho zungumzia mkuu 'August'?

Serikali ina wajibu, tena mkubwa sana kwa wananchi wake katika maswala ya shughuli zao. Hata kama si kama hiyo ruzuku ya mbolea iliyo elezwa hapa, kuna mambo mengi sana ambayo serikali ni lazima iwemo; hata kwenye masoko ya bidhaa, sera za kuunga mkono shughuli hizo za wananchi, n.k..
 
Tatizo kubwa ninaloliona nikuanzishwa huku tukiwa na malengo yale yale waliyokuwa nayo wakoloni kusafirisha Rasilimali na kuingiza bidhaa kutoka kwa wenzetu, Tujikite na kujiimalishe angalau katika kuongeza thamani Rasilimali zetu ili kuongeza base ya faida za uwepo wa reli hii hapo ndipo itagusa sector nyingi na uchumi wa watanzania wengi.
Mkuu 'FUTURE PLAN', sijui kama hili uliloweka hapa ni kweli; kwamba reli inajengwa kwa malengo yale yale ya wakoloni. Inawezekana hii ikawa ni hisia zako tu zinazochangiwa na hao hao viongozi kutokuwa na uwezo wa kuyasemea mambo kama haya ili wananchi wajue misingi ya miradi mkakati kama hii ya usafirishaji.
Hata hivyo kumekuwepo na jitihada za muda mrefu tokea tupate uhuru kuyabadili hayo malengo ya kikoloni, hata kama juhudi hizo zimekwama kwa sababu mbalimbali.
Uhitaji wa reli hii siyo swala tena la kuifikiria kuwa na malengo hayo hayo waliyokuwa nayo wakoloni.
Tatu wananchi wenyewe hakuna mfatiliaji
Hili la wananchi wengi kulazwa usingizi na CCM na kuwageuza kuwa washangiliaji wa maovu wanayofanyiwa wenyewe ni jambo la kusikitisha sana kwa nchi yetu.
 
Hatuwezi kujikomboa kwa kutegemea kuagiza mbolea toka nje kama ilivyo kwa Sukari..

Tujenge uwezo zaidi kwa wazalishaji wa ndani..Tuwape nafuu na incentives kitita..

Viwanda kama MINJINGU FERTILIZERS vilindwe kwa wivu mkubwa..

Kama ambavyo tunapswa kufuta uhuni unaozuia kuuzwa kwa viuatirifu vinavyozalishwa na kiwanda cha Kibaha chini ya NDC (Kilichojengwa na Wacuba)..Malaria inapaswa kuwa historia ktk nchi
Sijasema popote pale katika andiko langu kwamba tuwe 'tegemezi' kwa kitu chochote kilicho ndani ya uwezo wetu kukifanya, kama hizo mbolea , sukari na mengi mengine.
Lakini pia ungeweza pia kukumbuka kwamba juhudi zetu za kuzalisha mbolea, sukari na vinginevyo hatujawahi kuzifanya na kwamba hatuwezi kutoendelea kuzifanya. Hili siyo jambo geni hapa kwetu,; tofauti tu inayo jitokeza ni wakati tunapokuwepo na serikali kama hii inayotegemea kuwa maendeleo ya nchi yetu yataletwa hapa toka nje. Hawa ndio wanao tudidimiza zaidi na kuua kabisa moyo wa uthubutu wetu kujifanyia mambo yetu ili nchi yetu ipate maendeleo ya kweli.
 
Hakuna haja ya kupima upya namna ya kuwekeza viwanda; wao wafuate plani alizoasisi Nyerere tu mradi waziboreshe kuendana na wakati tu. Kama hawazijui au hawazikumbuki, mimi nitawajulisha.

Hawa watu wanapenda tuwaone ndio vipanga wetu. Kumbe buana😎😎😎😎
 
Back
Top Bottom