Shaffih awaita wachezaji wetu kikundi cha wahuni, huu udhalilishaji tumeuchoka sasa

Hivi wewe kwa kilichofanyika leo pale uwanjani, ni mchambuzi gani wa soka amekubaliana nacho?

Labda useme kuhusu ukali wa maneno aliyotumia shafii dauda kuwasilisha ujumbe wake, lakini kiukweli leo mlidevela
 
Kwani waliokuwepo ndani ya box ni wachezaji wa yanga tu?

"Kabla penat haijapigwa kikundi cha wahuni kimeingia" tafsiri kwanza..
Saido yuko sehemu yake kisheria, ila hawa wachezaji wa3, mmoja yanga na wawili namungo, ndio kikundi cha kihuni, yes, wamefanya uhuni, wamevamia sehemu isiyowahusu.

Mwamuzi yupo, mshika kibendera yupo, kifupi bongo soka bado sana, hatuna waamuzi, tuna wavamizi katika fani, hatuna wachambuzi wazuri wa soka, wengi wao ni wachambuzi wa mchele tu, viongozi wasoka letu, kichwani n'duhu, kazi kujiita watu wa mpira, ogopa sana kukutana na watu wanaojiita "watu wa mpira"[emoji23][emoji86]
 
Ati wachezaji wetu wameitwa wahuni.
Hao wetu ndio akina Nani ?
Ndani ya Box kuna Wachezaji WA timu zote mbili
Pamoja na mwamuzi.
Mtoa Mada anasema Shafi kawadhihaki Wachezaji waYanga
Pekee.
Huyo Refa hatutaki kumwona katika kuongoza mchezo wowote wa Ligi kuu Kwa miaka isiyopungua mitano.
Aende akasome upya Sheria za mpira.
 
Refa ndiyo mhuni hasa.Yule Refa zuzu aisee
 
Kwani aliandika Wachezaaji was Yanga ndio wahuni...wote walioingia kwenye kisanduku kabla ya Penati kipigwa ni Wahuni ...na Utopolo!
Huyo Refa na Kibendera wagutiwe leseni!
Kila kitendo kinaweza kileta maafa!
 
Hivi wewe kwa kilichofanyika leo pale uwanjani, ni mchambuzi gani wa soka amekubaliana nacho?

Labda useme kuhusu ukali wa maneno aliyotumia shafii dauda kuwasilisha ujumbe wake, lakini kiukweli leo mlidevela
Makosa tu ya kibinadamu ya refa hata makolo nao hupendelewa sometimes.
 
Makosa tu ya kibinadamu ya refa hata makolo nao hupendelewa sometimes.
Yale maamuzi aliyoyafanya refa hayakufanyika bahati mbaya mpaka itafsirike kwamba ni makosa ya kibinadamu, ilikuwa ni mpango naye alikua anatimiza agizo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…