Shairi - kisima nimekiacha

Shairi - kisima nimekiacha

Yakuonea

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
601
Reaction score
277
Mwenzenu ninajongea, taratibu nawajia
Kwa haya yalotokea, ya kisima nawaambia
Hofu menisogelea, na nguvu zimeishia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Kisima nilitumia, na mtu sikuchangia
Usafi lizingatia, kwa ndani nikiingia
Nilionyesha na nia, kufuli kukifungia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Nanikiwa kisimani, mwenzenu ninafurahia
Mengine siyatamani, siwezi wahadithia
Ni raha iso kifani, moyo unavyotulia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Nilikunywa nikaoga, na mengi nikafanyia
Sikuwa hata na woga, madhara sikudhania
Na watu nikawakoga, raha zilivyozidia
kisima nimekiacha, Maji hayanyweki tena

Kwa kweli nilijitamba, ijapo si mmiliki
Nikawaita washamba, hata ndugu marafiki
Nikawa mimi ni mwamba, kejeli nyingi na chuki
kisima nimekiacha, maji hanyweki tena

udhuru ulinipata, kwa mbali kusafiria
Nyuma yaliyofuata, machungu kusimulia
Waovu walikamata, mabaya kukusudia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Kisima liharibiwa, waovu watu wabaya
Tope walivyochimbuwa, kweli walikosa haya
Umbole kahujumiwa, 'saizi' sasa yapwaya
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Kwa sasa kimepoteza, umbole lile asili
Waovu nao wabeza, wasema hakina 'dili'
Usijaribu penyeza, utazama wako mwili
Kisima nimekiacha, maji hanyweki tena

Kisima sasa hatari, wadudu wamejibanza
kutumia kwa hadhari, fikiri kabla kuanza
Nimeacha jivinjari, tamaa sije niponza
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Na nyinyi enyi malenga, tahadhari nawambia
Hakuna sifa kulenga, chini tutawafukia
Mimi nimeshajitenga, na kule sintarudia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena


Wenu
Sindano Mwana wa Ganzi. (SMG)
 
Kwa kweli nilijitamba, ijapo si mmiliki
Nikawaita washamba, hata ndugu marafiki
Nikawa mimi ni mwamba, kejeli nyingi na chuki
kisima nimekiacha, maji hanyweki tena
............................................................

Na nyinyi enyi malenga, tahadhari nawambia
Hakuna sifa kulenga, chini tutawafukia
Mimi nimeshajitenga, na kule sintarudia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Wenu
Sindano Mwana wa Ganzi. (SMG)

Pokea pole mtani:

Pokea pole mtani, kupoteza lako dili
Maji hayo kisimani, nataka tuyajadili
Tena fikiri kichwani, utafahamu dalili
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Nafikiria kichwani, nahisi u m bahili
Ukateka kisimani, halafu huku kijali
Vya watu ukitamani, tafuta yake asili
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Najua ulitamani, vya bure bila kujali
Vina ladha mdomoni, hakika kama asali
Wenyewe ni kina nani? kichwani uliza swali
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Kisima siyo mtoni, uliza kwa wenye mali
Walochimba kisimani, iweje hukuwajali?
Busara yako kichwani, ni vipi hukujadili?
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Vieleavyo majini, nasema vina asili
Mtoni pia ziwani, baharini kuna meli
Asili yake ni nani, uliza bila kejeli
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Pokea pole mtani, ingawa si yako mali
Jifunze tena kichwani, kujua yake asili
Vya watu ni mtihani, usivifanye ni dili
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani
 
Pokea pole mtani:

Pokea pole mtani, kupoteza lako dili
Maji hayo kisimani, nataka tuyajadili
Tena fikiri kichwani, utafahamu dalili
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Nafikiria kichwani, nahisi u m bahili
Ukateka kisimani, halafu huku kijali
Vya watu ukitamani, tafuta yake asili
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Najua ulitamani, vya bure bila kujali
Vina ladha mdomoni, hakika kama asali
Wenyewe ni kina nani? kichwani uliza swali
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Kisima siyo mtoni, uliza kwa wenye mali
Walochimba kisimani, iweje hukuwajali?
Busara yako kichwani, ni vipi hukujadili?
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Vieleavyo majini, nasema vina asili
Mtoni pia ziwani, baharini kuna meli
Asili yake ni nani, uliza bila kejeli
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani

Pokea pole mtani, ingawa si yako mali
Jifunze tena kichwani, kujua yake asili
Vya watu ni mtihani, usivifanye ni dili
Kupoteza lako dili, pokea pole mtani



Hapana sim'bahili, choveki hapa nakana
Mengi nilikifadhili, kuepuka ya vijana
Nikaweka na kufuli, ni tendo la uungwana
Asante ndugu choveki, waovu si wenye mema

Ukweli nilikijali, na nyingi njema dhamira
Nilikiona asali, naramba pasi papara
Sasa ni kama ajali, hakina tena ubora
Asante ndugu choveki, waovu si wenye mema

Ni lipi la kwangu kosa, choveki naomba jibu
kwa huu wote mkasa, nipe busara za babu
kisima nilikinasa, waovu wakaharibu
Asante ndugu choveki, waovu si wenye mema

wabaya wangu waovu, chunguza utanambia
Na sasa nina makovu, moyoni nimeumia
Naomba ya uokovu, kisima nakihofia
Asante ndugu choveki, waovu si wenye mema


Wako
SMG
 
Kiu imenizidia, kisima nakitamani
vipi nitadumbukia, iwe kama zamani
Nipate kufurahia, nijifariji jamani
kisima kuharibiwa, wapi nitakunywa maji ?

mwilini ninazizima, kiu ilivyonishika
Naomba zenu hekima, moyoni nimedhofika
Pumzi zaweza zima, kiu isipo katika
kisima kuharibiwa, maji nitakunywa wapi ?

Maji ya kununua, sipendi yana utata
waweza hata ugua, faida huto ipata
viwango huwezi jua, na kiu hutoikata
kisima kuharibiwa, maji nitakunywa wapi ?

Ya kisima ni matamu, ladha iso kifani
ukinywa hayeshi hamu, hili si laubishani
uyanywe tena kwa zamu, utata hutobaini
kisima kuharibiwa, wapi nitakunywa maji ?

SMG
 

Hati miliki muhimu;

Hati miliki muhimu, na umma kutangazia

Kufuli siyo muhimu, hati ukishikilia

Watakwepa wadhalimu, mwenyewe wakihofia

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu


Kamwe hawata dhulumu, safari ukianzia

Heshima pia nidhamu, kwa kina kuheshimia

Utadhania mwalimu, nidhamu kitapatia

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu


Uianze kwa salamu, wakati wakizengea

Wajuwe siyo dhalimu, mwanzoni ukianzia

Washenga na mabinamu, watume kwa asilia

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu


Ni muungwana wa hamu, na wao watahisia

Wenyewe kukuheshimu, mwanzo mzuri anzia

Wakuone si mgumu, na posa kuwatumia
Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu

Tano zilizo muhimu, ni mwisho ninaishia

Nahisi umefahamu, kosa usije rudia

Utaupata wazimu, wengine wafanyizia!

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu

 

Hati miliki muhimu;

Hati miliki muhimu, na umma kutangazia

Kufuli siyo muhimu, hati ukishikilia

Watakwepa wadhalimu, mwenyewe wakihofia

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu


Kamwe hawata dhulumu, safari ukianzia

Heshima pia nidhamu, kwa kina kuheshimia

Utadhania mwalimu, nidhamu kitapatia

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu


Uianze kwa salamu, wakati wakizengea

Wajuwe siyo dhalimu, mwanzoni ukianzia

Washenga na mabinamu, watume kwa asilia

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu


Ni muungwana wa hamu, na wao watahisia

Wenyewe kukuheshimu, mwanzo mzuri anzia

Wakuone si mgumu, na posa kuwatumia
Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu

Tano zilizo muhimu, ni mwisho ninaishia

Nahisi umefahamu, kosa usije rudia

Utaupata wazimu, wengine wafanyizia!

Sikia kaka sikia, hati miliki muhimu




Nduguyo bado nasita


Mtani nimekupata, hati wasisitizia
Ila ni tabu kupata, kisima kiso kadhia
vingi kwa kweli matata, lengo hutolifikia
Visima viwango duni, nduguyo bado nasita

vingi viwango ni duni, hasa ukisha kipata
vina wingi urubuni, nasita rusha karata
Tageuzwa majinuni, mwishowe waja kudata
Visima viwango duni, nduguyo bado nasita

uma nitatangazia, kisima nikiridhia
Najiepusha kadhia, kwa vile vilo fifia
Nataka chenye vutia, ili nipate tulia
Visima viwango duni, nduguyo bado nasita

Sitaki bora kisima, na maji yamezidia
waweza pata dhahama, kuta zilivyo achia
Hata nikija lalama, nani atanisikia
Visima viwango duni, nduguyo bado nasita

Kipata chenye viwango, choveki nitakwambia
Huu ndo wangu mpango, ubora kuzingatia
Hapa sirushi madongo, mwenzio nasubiria
Visima viwango duni, nduguyo bado nasita


wako

SMG
 
Mwenzenu ninajongea, taratibu nawajia
Kwa haya yalotokea, ya kisima nawaambia
Hofu menisogelea, na nguvu zimeishia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Kisima nilitumia, na mtu sikuchangia
Usafi lizingatia, kwa ndani nikiingia
Nilionyesha na nia, kufuli kukifungia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Nanikiwa kisimani, mwenzenu ninafurahi
Mengine siyatamani, siwezi wahadithia
Ni raha iso kifani, moyo unavyotulia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Nilikunywa nikaoga, na mengi nikafanyia
Sikuwa hata na woga, madhara sikudhania
Na watu nikawakoga, raha zilivyozidia
kisima nimekiacha, Maji hayanyweki tena

Kwa kweli nilijitamba, ijapo si mmiliki
Nikawaita washamba, hata ndugu marafiki
Nikawa mimi ni mwamba, kejeli nyingi na chuki
kisima nimekiacha, maji hanyweki tena

udhuru ulinipata, kwa mbali kusafiria
Nyuma yaliyofuata, machungu kusimulia
Waovu walikamata, mabaya kukusudia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Kisima liharibiwa, waovu watu wabaya
Tope walivyochimbuwa, kweli walikosa haya
Umbole kahujumiwa, 'saizi' sasa yapwaya
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Kwa sasa kimepoteza, umbole lile asili
Waovu nao wabeza, wasema hakina 'dili'
Usijaribu penyeza, utazama wako mwili
Kisima nimekiacha, maji hanyweki tena

Kisima sasa hatari, wadudu wamejibanza
kutumia kwa hadhari, fikiri kabla kuanza
Nimeacha jivinjari, tamaa sije niponza
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena

Na nyinyi enyi malenga, tahadhari nawambia
Hakuna sifa kulenga, chini tutawafukia
Mimi nimeshajitenga, na kule sintarudia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena


Wenu
Sindano Mwana wa Ganzi. (SMG)

Nasema pole sindano; wahenga hukusikia
Maisha ni mashindano, si ajabu kutindikia
Wajinadi kwa maneno, mrembo wajipatia
Kususa uhayawani; ya bahari huyawezi.

Jirani kajihifadhi; maji shinda kajitekea
Kisima hakina maradhi; janga limekutokea
Wamlaumu mahadhi; maji amejinywea
Kususa uhayawani; ya bahari huyawezi


Tuliza akili yako, maji hayana makombo
Jitwalie kata yako, kisimani rudi zako
Kunywa maji yako; ikate kiu yako
Kususa uhayawani, ya bahari huyawezi.

Yakisima yamezidi, utamu hauna mfano
Mahadhi kajirudi, hana shari ya maneno
Sindano nyumbani rudi, jilie raha zako
Kususa uhayawani, ya bahari huyawezi.


Chama
Gongo la Mboto DSM.
 
Nasema pole sindano; wahenga hukusikia
Maisha ni mashindano, si ajabu kutindikia
Wajinadi kwa maneno, mrembo wajipatia
Kususa uhayawani; ya bahari huyawezi.

Jirani kajihifadhi; maji shinda kajitekea
Kisima hakina maradhi; janga limekutokea
Wamlaumu mahadhi; maji amejinywea
Kususa uhayawani; ya bahari huyawezi


Tuliza akili yako, maji hayana makombo
Jitwalie kata yako, kisimani rudi zako
Kunywa maji yako; ikate kiu yako
Kususa uhayawani, ya bahari huyawezi.

Yakisima yamezidi, utamu hauna mfano
Mahadhi kajirudi, hana shari ya maneno
Sindano nyumbani rudi, jilie raha zako
Kususa uhayawani, ya bahari huyawezi.


Chama
Gongo la Mboto DSM.


Uamuzi nilochukua, hakika niwa busara
Jaribu kudadavua, sindano sina papara
Hili ukishalijua, huwezi pata madhara
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Tope zilichimbuliwa, maji sasa karaha
Sipendi kushutumiwa, nasema hayana raha
Kisima lifumiliwa, tena pasi na staha
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Kisima kimechafuka, na tope kila sehemu
Nduguyo nimeshituka, kwa pale sinayo hamu
Siwezi kuwa mzuka, kujitoa ufahamu
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Vipi nikitia kata, tope likang'ang'ania
kipi kitakachofata, kama sio kujutia
Na maradhi nikipata, nani tanihudumia?
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Kisima tadumbukia, cha maji yalo salama
Humo nitafurahia, na wala sintolalama
Mbizi nitazidishia, kwa ndani ninavyozama
Tope lishavurugwa, maji hayanyweki tena

wako

SMG
 
Uamuzi nilochukua, hakika niwa busara
Jaribu kudadavua, sindano sina papara
Hili ukishalijua, huwezi pata madhara
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Tope zilichimbuliwa, maji sasa karaha
Sipendi kushutumiwa, nasema hayana raha
Kisima lifumiliwa, tena pasi na staha
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Kisima kimechafuka, na tope kila sehemu
Nduguyo nimeshituka, kwa pale sinayo hamu
Siwezi kuwa mzuka, kujitoa ufahamu
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Vipi nikitia kata, tope likang'ang'ania
kipi kitakachofata, kama sio kujutia
Na maradhi nikipata, nani tanihudumia?
Tope lishavurugwa, maji hayo sinywi tena

Kisima tadumbukia, cha maji yalo salama
Humo nitafurahia, na wala sintolalama
Mbizi nitazidishia, kwa ndani ninavyozama
Tope lishavurugwa, maji hayanyweki tena

wako

SMG

Kususa si uunngwana, busara kufikiria
kisima chako bayana, hakuna wa kubishia
Hakuna kulaumiana, hilo nakazania
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Makosa uliyatenda, mwenyewe hukusikia
Kisima hazina linda, vingapi utasusia
Nasema njia panda, sindano wajitakia
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Kosa kutendeana, hilo mbona halina shida
Waungwana kusamehana, jambo hilo kawaida
Jitulize na rehana; hata wewe umeranda
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Kisima chako maridhawa, hakina msimu wa maji
Hakika nakuweka sawa, usiwe mropokaji
Waugopa ugonjwa, hali wewe msakaji
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Chama nipo safarini, nikija nitakuona
Usionione hayawani, hilo nimeshaliona
Umepata mtihani, jaribu kushauriana
Mso hili analile, kaa chini fikiria.

Chama
Gongo la Mboto DSM.
 
Nduguyo bado nasita


Mtani nimekupata, hati wasisitizia
Ila ni tabu kupata, kisima kiso kadhia
vingi kwa kweli matata, lengo hutolifikia
Visima viwango duni, nduguyo bado nasita
.......................................................
Kipata chenye viwango, choveki nitakwambia
Huu ndo wangu mpango, ubora kuzingatia
Hapa sirushi madongo, mwenzio nasubiria
Visima viwango duni, nduguyo bado nasita
wako
SMG

Ukiona vyaelea;

Ukiona vyaelea, ujuwe vimeundiwa
Nami nakukumbushia, si kwamba vimejaliwa
Tafuata chako tunzia, mengine ni majaliwa
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Nimeanza na msemo, kukumbusha ya wahenga
Tena kipate kisomo, twakujulisha malenga
Ama waleta mgomo, kufuga wipiga chenga?
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Ni vingi vyenye viwango, machoyo ukifungua
Tumia wako ubongo, kwa dhati utajulia
Wala huhitaji hongo, vinono kujipatia
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Tafuta chako utunze, utashangaa mavuno
Tena kutunza jifunze, utafaidi vinono
Kisima chako kitunze, kwa yako hiyo mikono
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Hapa nasema tamati, nahisi umenipata
Mradi ujizatiti, nasema utakipata
Na tena cha madhubuti, kisima na yake kata
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea
 
Kususa si uunngwana, busara kufikiria
kisima chako bayana, hakuna wa kubishia
Hakuna kulaumiana, hilo nakazania
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Makosa uliyatenda, mwenyewe hukusikia
Kisima hazina linda, vingapi utasusia
Nasema njia panda, sindano wajitakia
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Kosa kutendeana, hilo mbona halina shida
Waungwana kusamehana, jambo hilo kawaida
Jitulize na rehana; hata wewe umeranda
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Kisima chako maridhawa, hakina msimu wa maji
Hakika nakuweka sawa, usiwe mropokaji
Waugopa ugonjwa, hali wewe msakaji
Mso hili analile, kaa chini fikiria

Chama nipo safarini, nikija nitakuona
Usionione hayawani, hilo nimeshaliona
Umepata mtihani, jaribu kushauriana
Mso hili analile, kaa chini fikiria.

Chama
Gongo la Mboto DSM.


SI KAMA NIMESUSIA

Mengi nilifikiria, wala sikukurupuka
Busara nimetumia, ndo kisa cha kufunguka
Na wala sitojutia, hili halina mashaka
si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

Ni vipi wanishutumu, ukweli hutaki ona
Hivi nikilamba sumu, wadhani naweza pona?
Napingana na dhalimu, walojaa kila kona
Si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

Mbona nimeshasamehe, madhila nilofanyiwa
Kwao wao iwe sherehe, kila jambo majaliwa
Nangoja yangu tarehe, kwa lile nilopangiwa
Si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

siwezi jilazimisha, moyo wangu umzito
kisima tabadilisha, nataka umotomoto
Nianze yangu maisha, niachane na majuto
si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

safari nakutakia, ufike huko salama
Na tena ukirudia, sikose kunitazama
Ndio mambo ya dunia, ngoja niache lalama
si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho


SMG
 
Ukiona vyaelea;

Ukiona vyaelea, ujuwe vimeundiwa
Nami nakukumbushia, si kwamba vimejaliwa
Tafuata chako tunzia, mengine ni majaliwa
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Nimeanza na msemo, kukumbusha ya wahenga
Tena kipate kisomo, twakujulisha malenga
Ama waleta mgomo, kufuga wipiga chenga?
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Ni vingi vyenye viwango, machoyo ukifungua
Tumia wako ubongo, kwa dhati utajulia
Wala huhitaji hongo, vinono kujipatia
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Tafuta chako utunze, utashangaa mavuno
Tena kutunza jifunze, utafaidi vinono
Kisima chako kitunze, kwa yako hiyo mikono
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea

Hapa nasema tamati, nahisi umenipata
Mradi ujizatiti, nasema utakipata
Na tena cha madhubuti, kisima na yake kata
Ujuwe vimeundiwa, uonavyo vyaelea


KIPI ZAIDI YA KIPI?

cha kwangu nitatafuta, hili nimedhamiria
Tena nikisha kipata, walahi nitatulia
Vya watu sitafuata, mola tanisaidia
vya pwani na kule bara, kipi zaidi ya kipi?

Kuna visima vya pwani, wengi wavisimulia
vyajua mambo fulani, raha hazitaishia
Hata kiwe cha zamani, mwenyewe utaridhia
Vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Majiye kama nanasi, walonavyo meniambia
Havipatikani nkasi, mombasa ndo asilia
utatulia kwa nafsi, usijute na dunia
vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Na kuna vya kule bara, sifaze sijazipata
Labda navyo imara, Choveki unazo data?
Vipi kikiri kakara, vyaweza kweli kunata?
Vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Visima vya asilia, kwa sasa tabu kupata
mchina kaingilia, soko amelikamata
Na kama hujajulia, kundini waweza fata
vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Mtani usinichoke, nduguyo nahangaika
Naomba nihifadhike, niache kulalamika
salama nisalimike, maisha yenye mashaka
vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?


SMG
 
KIPI ZAIDI YA KIPI?

Kuna visima vya pwani, wengi wavisimulia
vyajua mambo fulani, raha hazitaishia
Hata kiwe cha zamani, mwenyewe utaridhia
Vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?
...........................................
Na kuna vya kule bara, sifaze sijazipata
Labda navyo imara, Choveki unazo data?
Vipi kikiri kakara, vyaweza kweli kunata?
Vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?
SMG

Muhimu Kuridhika nacho tu;

Chongo kuita kengeza, msemo ushasikia?
Si fundi wa kueleza, ni wapi kulobobea

Uzushi sitoeneza, na hilo kaka julia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Nchini kote uliza, majibu siyo sawia

Wa pwani wanidokeza, visima vyao hulea

Sauti utaipaza, kwa ladha ya asilia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Bara ni kama baraza, visima hivyo sikia

Na kiu utamaliza, na mazingira sawia

Kwa macho utaangaza, wakati wakodelea

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Wasema hutopoteza, na bara utarudia
Visima vyao vyajaza, kwa maji yalo sawia

Mchina hajakatiza, vya bara ni asilia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Vya pwani siyo vilaza, mtani hapo julia

Kwa mengi vinashangaza, ufundi wa asilia

Kwa ndugu utaapiza, kisima kutoachia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Ridhika nimeeleza, muhimu hiyo sikia
Chongo kuita kengeza, ishara ilo timia

Utabaki waapiza, na mali ukagawia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Mtani ninamaliza, mwishowe ninaishia

Ni mengi nimeeleza, wajibu kwako kujua

Muhimu maji kujaza, kisima kilo tulia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima

 
SI KAMA NIMESUSIA



Mengi nilifikiria, wala sikukurupuka
Busara nimetumia, ndo kisa cha kufunguka
Na wala sitojutia, hili halina mashaka
si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

Ni vipi wanishutumu, ukweli hutaki ona
Hivi nikilamba sumu, wadhani naweza pona?
Napingana na dhalimu, walojaa kila kona
Si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

Mbona nimeshasamehe, madhila nilofanyiwa
Kwao wao iwe sherehe, kila jambo majaliwa
Nangoja yangu tarehe, kwa lile nilopangiwa
Si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

siwezi jilazimisha, moyo wangu umzito
kisima tabadilisha, nataka umotomoto
Nianze yangu maisha, niachane na majuto
si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho

safari nakutakia, ufike huko salama
Na tena ukirudia, sikose kunitazama
Ndio mambo ya dunia, ngoja niache lalama
si kama nimesusia, lenye mwanzo lina mwisho


SMG

ZAFANANA

Sikiliza kwa makini, hasira ziweke kando
Lako jipe tumaini, kisima safi ni kondo
Utajitia mtoni, utaumudu mkondo
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Bara na visiwani, kote nimepitia
Wamiliki visimani, hakuna asiyejutia
Wamelala malindoni, wajuvi wamepitia
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Usijitie jutoni, rudi zako kisimani
Busara zako sioni, fikiri tena makini
Mapenzi yapo moyoni, hayapotei gharikani
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Visima vina maudhi, na kweli vina madhara
Usiogope maradhi, vitamu vina madhara
Hatima yetu faradhi, nalo si masikhara
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Maji tamu kisimani, sote twakimbilia
Kila mtu atamani, hakuna pakulilia
Asipoyanywa Hassani, chura atakimbilia
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Tamati namalizia, rudisha zako hisani
Tanga nakaribia, nijiendee kisimani
Tuliza zako hisia, waulize makuhani
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
KIPI ZAIDI YA KIPI?

cha kwangu nitatafuta, hili nimedhamiria
Tena nikisha kipata, walahi nitatulia
Vya watu sitafuata, mola tanisaidia
vya pwani na kule bara, kipi zaidi ya kipi?

Kuna visima vya pwani, wengi wavisimulia
vyajua mambo fulani, raha hazitaishia
Hata kiwe cha zamani, mwenyewe utaridhia
Vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Majiye kama nanasi, walonavyo meniambia
Havipatikani nkasi, mombasa ndo asilia
utatulia kwa nafsi, usijute na dunia
vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Na kuna vya kule bara, sifaze sijazipata
Labda navyo imara, Choveki unazo data?
Vipi kikiri kakara, vyaweza kweli kunata?
Vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Visima vya asilia, kwa sasa tabu kupata
mchina kaingilia, soko amelikamata
Na kama hujajulia, kundini waweza fata
vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?

Mtani usinichoke, nduguyo nahangaika
Naomba nihifadhike, niache kulalamika
salama nisalimike, maisha yenye mashaka
vya bara na kule pwani, kipi zaidi ya kipi?


SMG

Mwanangu Yakuonea, sikiza wangu usia
Ni mengi umeongea, yaani karibu kulia
Kobisi nilikulia, nimeshindwa kuvumilia
Nyumba wakaa mwenyewe, Kisima gharama tupu

Hujaona ya kununua, Maji yapo sikia
Kubaki jishebedua, kisima kujichimbia
Umekua ka Ngamia, Maji mengi kujinywea?
Nyumba wakaa mwenyewe, Kisima gharama tupu

Ungeweza jipatia, Kilimanjaro maji sawia
Kwa bei ya kutupia, Uhai wajimwagia
Na ladha ilo sawia, Sayona wajionjea
Nyumba wakaa mwenyewe, Kisima gharama tupu
 
Muhimu Kuridhika nacho tu;

Chongo kuita kengeza, msemo ushasikia?
Si fundi wa kueleza, ni wapi kulobobea

Uzushi sitoeneza, na hilo kaka julia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Nchini kote uliza, majibu siyo sawia

Wa pwani wanidokeza, visima vyao hulea

Sauti utaipaza, kwa ladha ya asilia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Bara ni kama baraza, visima hivyo sikia

Na kiu utamaliza, na mazingira sawia

Kwa macho utaangaza, wakati wakodelea

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Wasema hutopoteza, na bara utarudia
Visima vyao vyajaza, kwa maji yalo sawia

Mchina hajakatiza, vya bara ni asilia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Vya pwani siyo vilaza, mtani hapo julia

Kwa mengi vinashangaza, ufundi wa asilia

Kwa ndugu utaapiza, kisima kutoachia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Ridhika nimeeleza, muhimu hiyo sikia
Chongo kuita kengeza, ishara ilo timia

Utabaki waapiza, na mali ukagawia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima


Mtani ninamaliza, mwishowe ninaishia

Ni mengi nimeeleza, wajibu kwako kujua

Muhimu maji kujaza, kisima kilo tulia

Ridhika nacho kisima, muhimu hiyo lazima



WOSIA NIMEUPATA

kweli nazidi shukuru, mengi wanisaidia
wanipa mwanga na nuru, kwa yale nisojulia
Nisingependa kufuru, na mola takujalia
Wosia nimeupata, nasema tazingatia

kuridhika ni lazima, kama ulivyosema
Hivyo ni vyema kupima, tena kungali mapema
singoji jua kuzama, ndio nije kulalama
Wosia nimeupata, nasema tazingatia

Mchina ajulikana, popote hakosekani
Iweje twaambiana, vya bara hapatikani
si kama twachunguzana, niondoe mashakani
Wosia nimeupata, nasema tazingatia

jibu ukinipatia, bara nitafikiria
Naomba liwe sawia, unionyeshe na njia
Na pwani nafatilia, malindi nitaanzia
wosia nimeupata, nasema tazingatia

Unguja na msambweni, nako pia nitafika
Nimuone bwana Joni, anipe ya uhakika
Mtani nihatarini, kisima nisipo shika
Wosia nimeupata, nasema tazingatia

Mwaka nao wakatika, umri pia waniaga
Yaani nipatashika, hili ni bonge la 'saga'
Naomba kusitirika, mola nipe msaada
wosia nimeupata, nasema tazingatia

SMG
 
ZAFANANA

Sikiliza kwa makini, hasira ziweke kando
Lako jipe tumaini, kisima safi ni kondo
Utajitia mtoni, utaumudu mkondo
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Bara na visiwani, kote nimepitia
Wamiliki visimani, hakuna asiyejutia
Wamelala malindoni, wajuvi wamepitia
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Usijitie jutoni, rudi zako kisimani
Busara zako sioni, fikiri tena makini
Mapenzi yapo moyoni, hayapotei gharikani
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Visima vina maudhi, na kweli vina madhara
Usiogope maradhi, vitamu vina madhara
Hatima yetu faradhi, nalo si masikhara
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Maji tamu kisimani, sote twakimbilia
Kila mtu atamani, hakuna pakulilia
Asipoyanywa Hassani, chura atakimbilia
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Tamati namalizia, rudisha zako hisani
Tanga nakaribia, nijiendee kisimani
Tuliza zako hisia, waulize makuhani
Watanga walinena, hizo zote zafanana

Chama
Gongo la Mboto DSM


SIO ZOTE ZAFANANA

Mgosi nafurahika, kwa wewe kurudi tena
Mwenzio nahangaika, maisha hayajafana
Hujafa hujaumbika, angalizo la rabana
Sio zote zafanana, chunguza utanambia

wembamba sio upana, jaribu kupambanua
Na usiku si mchana, hivi kweli hujajua?
Kikongwe hawi kijana, naomba kufafanua
sio zote zafanana, chunguza utanambia

Na fupi kamwe si ndefu, vipimo vi tofauti
Hata uwe umpofu, gogo huliiti jiti
Mfupa sio mnofu, tuulize watafiti
Sio zote zafanana, chunguza utanambia

Vya mombasa si vya bara, kimaisha na fikira
Na pwani haiwi ngara, mwembe hauwi mpera
Tafiti acha papara, uone kilicho bora
sio zote zafanana, chunguza utanambia

kuna zile za minato, nyingine zimeachia
Na hata kwa manukato, huwezi badilishia
utapatwa machafuko, na mengi yenye kadhia
sio zote zafanana, chunguza utanambia

SMG
 
Mwanangu Yakuonea, sikiza wangu usia
Ni mengi umeongea, yaani karibu kulia
Kobisi nilikulia, nimeshindwa kuvumilia
Nyumba wakaa mwenyewe, Kisima gharama tupu

Hujaona ya kununua, Maji yapo sikia
Kubaki jishebedua, kisima kujichimbia
Umekua ka Ngamia, Maji mengi kujinywea?
Nyumba wakaa mwenyewe, Kisima gharama tupu

Ungeweza jipatia, Kilimanjaro maji sawia
Kwa bei ya kutupia, Uhai wajimwagia
Na ladha ilo sawia, Sayona wajionjea
Nyumba wakaa mwenyewe, Kisima gharama tupu


YA CHUPA SIJAZOEA

Ya chupa nilijaribu, ila kweli yana kifu
Nilikosa na jawabu, sikuona unadhifu
kwa kero na zake tabu, hunywi kwa uadilifu
Ya chupa sijazoea, hayakati kiu yangu

Ijapo wamewekea, kwa ladha za mbalimbali
kuyanywa nayagomea, kwa kuwa ninajijali
sina nayo mazoea, nisije pata ajali
Ya chupa sijazoea, hayakati kiu yangu

Ya chupa yana karaha, na raha hutoipata
utaishia kuhaha, huwezi kunywa kwa kata
Hizi ni zangu nasaha, si kama eti nanata
Ya chupa sijazoea, hayakati kiu yangu

Chunguza haya chupa, ukinywa hautosheki
unywe lita na mapipa, 'kiuyo' haikwepeki
chupa nyingine zi bapa, kwa kweli sishawishiki
Ya chupa sijazoea, hayakati kiu yangu

SMG
 
SIO ZOTE ZAFANANA

Mgosi nafurahika, kwa wewe kurudi tena
Mwenzio nahangaika, maisha hayajafana
Hujafa hujaumbika, angalizo la rabana
Sio zote zafanana, chunguza utanambia

wembamba sio upana, jaribu kupambanua
Na usiku si mchana, hivi kweli hujajua?
Kikongwe hawi kijana, naomba kufafanua
sio zote zafanana, chunguza utanambia

Na fupi kamwe si ndefu, vipimo vi tofauti
Hata uwe umpofu, gogo huliiti jiti
Mfupa sio mnofu, tuulize watafiti
Sio zote zafanana, chunguza utanambia

Vya mombasa si vya bara, kimaisha na fikira
Na pwani haiwi ngara, mwembe hauwi mpera
Tafiti acha papara, uone kilicho bora
sio zote zafanana, chunguza utanambia

kuna zile za minato, nyingine zimeachia
Na hata kwa manukato, huwezi badilishia
utapatwa machafuko, na mengi yenye kadhia
sio zote zafanana, chunguza utanambia

SMG

ZAFANANA


Mimi mchimba mahiri, kazi yangu naijua
Nimetafiti dhahiri, yote nimeyajua
Nimekula vya hariri, hakuna asiyejua
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Visima si tofauti, maumbile nagusia
Utakunywa kwa nyakati, hilo nakumbia
Fanya zako harakati, kiasi utajutia
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Kisima wakiingia, mbizi wajipigia
Hazina wakimwagia, maradhi cha kupatia
Kauli yakuishia, vilinge wavikimbia
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Sadiki yangu maneno, visima vyote ni sawa
usije jitoa meno, utamu wako maridhawa
Umejikunya kiuno, akili za kupagawa
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile


Usijitie kisoi , utamu wako mwenyewe
Kamuulize mtoi, mrukaji kama mwewe
Hata lile goigoi, lawa tamu kama wewe
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Back
Top Bottom