Mwenzenu ninajongea, taratibu nawajia
Kwa haya yalotokea, ya kisima nawaambia
Hofu menisogelea, na nguvu zimeishia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Kisima nilitumia, na mtu sikuchangia
Usafi lizingatia, kwa ndani nikiingia
Nilionyesha na nia, kufuli kukifungia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Nanikiwa kisimani, mwenzenu ninafurahia
Mengine siyatamani, siwezi wahadithia
Ni raha iso kifani, moyo unavyotulia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Nilikunywa nikaoga, na mengi nikafanyia
Sikuwa hata na woga, madhara sikudhania
Na watu nikawakoga, raha zilivyozidia
kisima nimekiacha, Maji hayanyweki tena
Kwa kweli nilijitamba, ijapo si mmiliki
Nikawaita washamba, hata ndugu marafiki
Nikawa mimi ni mwamba, kejeli nyingi na chuki
kisima nimekiacha, maji hanyweki tena
udhuru ulinipata, kwa mbali kusafiria
Nyuma yaliyofuata, machungu kusimulia
Waovu walikamata, mabaya kukusudia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Kisima liharibiwa, waovu watu wabaya
Tope walivyochimbuwa, kweli walikosa haya
Umbole kahujumiwa, 'saizi' sasa yapwaya
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Kwa sasa kimepoteza, umbole lile asili
Waovu nao wabeza, wasema hakina 'dili'
Usijaribu penyeza, utazama wako mwili
Kisima nimekiacha, maji hanyweki tena
Kisima sasa hatari, wadudu wamejibanza
kutumia kwa hadhari, fikiri kabla kuanza
Nimeacha jivinjari, tamaa sije niponza
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Na nyinyi enyi malenga, tahadhari nawambia
Hakuna sifa kulenga, chini tutawafukia
Mimi nimeshajitenga, na kule sintarudia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Wenu
Sindano Mwana wa Ganzi. (SMG)
Kwa haya yalotokea, ya kisima nawaambia
Hofu menisogelea, na nguvu zimeishia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Kisima nilitumia, na mtu sikuchangia
Usafi lizingatia, kwa ndani nikiingia
Nilionyesha na nia, kufuli kukifungia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Nanikiwa kisimani, mwenzenu ninafurahia
Mengine siyatamani, siwezi wahadithia
Ni raha iso kifani, moyo unavyotulia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Nilikunywa nikaoga, na mengi nikafanyia
Sikuwa hata na woga, madhara sikudhania
Na watu nikawakoga, raha zilivyozidia
kisima nimekiacha, Maji hayanyweki tena
Kwa kweli nilijitamba, ijapo si mmiliki
Nikawaita washamba, hata ndugu marafiki
Nikawa mimi ni mwamba, kejeli nyingi na chuki
kisima nimekiacha, maji hanyweki tena
udhuru ulinipata, kwa mbali kusafiria
Nyuma yaliyofuata, machungu kusimulia
Waovu walikamata, mabaya kukusudia
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Kisima liharibiwa, waovu watu wabaya
Tope walivyochimbuwa, kweli walikosa haya
Umbole kahujumiwa, 'saizi' sasa yapwaya
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Kwa sasa kimepoteza, umbole lile asili
Waovu nao wabeza, wasema hakina 'dili'
Usijaribu penyeza, utazama wako mwili
Kisima nimekiacha, maji hanyweki tena
Kisima sasa hatari, wadudu wamejibanza
kutumia kwa hadhari, fikiri kabla kuanza
Nimeacha jivinjari, tamaa sije niponza
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Na nyinyi enyi malenga, tahadhari nawambia
Hakuna sifa kulenga, chini tutawafukia
Mimi nimeshajitenga, na kule sintarudia
kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena
Wenu
Sindano Mwana wa Ganzi. (SMG)