ramadhani kimweri
Senior Member
- Apr 22, 2016
- 181
- 179
NAJIPA MOYO.
Matatizo niliyo nayo, kuyabeba ni michosho
Lakini hali iwayo, naloa maji ya jasho
Bado ninajipa moyo, kuwa nitapata kesho.
Ninapotazama mbele, giza nene naliona
Lini nitafika kule, moyo tumaini sina
Hata nipige kelele, kila siku kama jana.
Shibe yangu ni njaa, na maji nimeze mate
Naonekana kichaa, natafuta nisipate
Natembea natambaa, niende nijikokote..
Ya jana ndio ya leo, sionagi tofauti
Mie sina kimbilio, na wala sifurukuti
Maisha yangu kilio, kila siku yalaiti..
Ukitegemea waja, ipo siku utalia
Niliposhikwa na haja, wote wakaniambia
Nakuniona kioja, nataabika dunia.
Tumaini langu moja, ndio nalitegemea
Ajuae zangu haja, kwake nimeegemea
Ni yeye mola mmoja, haya kuniondolea.
[emoji2398]Ibn kimweri.
Ramadhani Juma Kimweri
0746328046.
Mashairi mengine soma Shairi: Hakuna siri tena
Matatizo niliyo nayo, kuyabeba ni michosho
Lakini hali iwayo, naloa maji ya jasho
Bado ninajipa moyo, kuwa nitapata kesho.
Ninapotazama mbele, giza nene naliona
Lini nitafika kule, moyo tumaini sina
Hata nipige kelele, kila siku kama jana.
Shibe yangu ni njaa, na maji nimeze mate
Naonekana kichaa, natafuta nisipate
Natembea natambaa, niende nijikokote..
Ya jana ndio ya leo, sionagi tofauti
Mie sina kimbilio, na wala sifurukuti
Maisha yangu kilio, kila siku yalaiti..
Ukitegemea waja, ipo siku utalia
Niliposhikwa na haja, wote wakaniambia
Nakuniona kioja, nataabika dunia.
Tumaini langu moja, ndio nalitegemea
Ajuae zangu haja, kwake nimeegemea
Ni yeye mola mmoja, haya kuniondolea.
[emoji2398]Ibn kimweri.
Ramadhani Juma Kimweri
0746328046.
Mashairi mengine soma Shairi: Hakuna siri tena