Bunsen Burner
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 909
- 1,101
Tz nchi ya maagizo, na kila mtu ni kambale kutoa maagizo kwa kwenda mbele, kaazi kwelikweli...Nchiiii ngumu saana hakuna kinachoeleweka.Sasa huyu anaongea kama nani??kweli katiba inamruhusu kutoa maagizo au Sisi ni nchiiii ya kusadikika.
Kwani wameanza kusema hivo leo?Hu
Huyo ndio msemaji wa CCm Taifa chama kilichounda serikali na kuikabidhi serikali ili isimamie ilani, Sasa wewe puuza maagizo yake Ndio utajuwa Ni nani
Na wewe umeingizwa mkenge?Kama mke wako atadaiwa mpigie ndio utajua yeye ni nani?
View attachment 2328846
SHAKA "TUSIWATOZE FEDHA WAJAWAZITO"
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka amewataka watoa huduma kote nchini kuacha kuwatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua.
Shaka ametoa maelekezo hayo akiwa Jimbo la Bukene wilaya ya Nzega mkoa wa Tabora alipopokea kilio cha wakina mama wakati alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wakati wa ziara yake.
View attachment 2328851
"Naomba nitumie jukwa hili kuweka msisitizo kwenye maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa wizara ya afya pamoja na TAMISEMI juu ya kusimamia takwa la kisera la kutaka watoa huduma za afya kote nchini kutowatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua. Hapa Bukene DC na Mkurugenzi mmesikia kilio hiki naomba tusitishe tabia hiyo" Amesema Shaka
View attachment 2328849
Shaka amewaeleza wananchi hao kuwa tayari Rais Samia ameshatoa maelekezo kwa wizara ya afya nchini kufanya mapitio ya gharama za matibabu ili kuja na muongozo utakaowapunguzia mzigo wananchi. Hivyo waendelee kumuunga mkono kwa kumuombea dua na sala pamoja na kutoa ushirikiano kwa serikali anayoiongoza kwa kuchapakazi na kulipa kodi.
View attachment 2328852
Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wazazi Tanzania Ndg Gilbert Kalima ambaye ameambatana na Shaka katika ziara hiyo amewataka wananchi kujitokeza kuhesabiwa na kutoa ushirikiano kwa makarani siku ya sensa Agosti 23, 2022.
View attachment 2328850
'CCM Imara, Shiriki Uchaguzi Kwa Uadilifu na Jiandae Kuhesabiwa Agosti 23, 2022'
#CCMIMara
#KaziIendelee
Mkuu uko sahihi 1000%Nitachangia bila kuweka porojo za siasa. Hii sera utekelezaji wake ni mgumu sana.
Kundi la wajawazito, watoto chini ya umri wa miaka 5 na wazee ndilo linalohudhuria zaidi katika vituo vya huduma za afya na ndilo linapaswa kupewa msamaha kwa mujibu wa sera.
Hii hupelekea mzigo mkubwa wa gharama za uendeshaji kwa vituo hivi, na kuingia kwenye madeni (umeme, maji, dawa, taka nk).
Ushauri wangu:
1. Ujauzito sio dharula, wazazi wa mtoto wana muda wa miezi 9 kujipanga hivyo wachangie gharama kidogo za huduma isipokuwa kwa huduma za dharula.
2. Kila mtanzania awe na Bima ya Afya, itungwe sheria ya kuwezesha utekelezaji wa hili.
Mwisho: "Afya ni ghali, na hakuna matibabu ya bure, ukiona umepatiwa huduma bila malipo jua kuna mtu/taasisi/nk imetoa gharama kwa ajili yako."
Na upo hapo unaamini tozo zimefutwa. Pata ujauzito kajifungulie Bukene mahali tamko lilipotolewa halafu uje useme kama tozo zimefutwa. Bahati mbaya kubwa ni kuamini matamko ya wanasisaπππππππππ
Safi sana! Ila tutakoma zile nyodo za manesi
Huyu mjomba ni jembe kwelikweliView attachment 2328846
SHAKA "TUSIWATOZE FEDHA WAJAWAZITO"
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka amewataka watoa huduma kote nchini kuacha kuwatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua.
Shaka ametoa maelekezo hayo akiwa Jimbo la Bukene wilaya ya Nzega mkoa wa Tabora alipopokea kilio cha wakina mama wakati alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wakati wa ziara yake.
View attachment 2328851
"Naomba nitumie jukwa hili kuweka msisitizo kwenye maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa wizara ya afya pamoja na TAMISEMI juu ya kusimamia takwa la kisera la kutaka watoa huduma za afya kote nchini kutowatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua. Hapa Bukene DC na Mkurugenzi mmesikia kilio hiki naomba tusitishe tabia hiyo" Amesema Shaka
View attachment 2328849
Shaka amewaeleza wananchi hao kuwa tayari Rais Samia ameshatoa maelekezo kwa wizara ya afya nchini kufanya mapitio ya gharama za matibabu ili kuja na muongozo utakaowapunguzia mzigo wananchi. Hivyo waendelee kumuunga mkono kwa kumuombea dua na sala pamoja na kutoa ushirikiano kwa serikali anayoiongoza kwa kuchapakazi na kulipa kodi.
View attachment 2328852
Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wazazi Tanzania Ndg Gilbert Kalima ambaye ameambatana na Shaka katika ziara hiyo amewataka wananchi kujitokeza kuhesabiwa na kutoa ushirikiano kwa makarani siku ya sensa Agosti 23, 2022.
View attachment 2328850
'CCM Imara, Shiriki Uchaguzi Kwa Uadilifu na Jiandae Kuhesabiwa Agosti 23, 2022'
#CCMIMara
#KaziIendelee
Unafahamu kati chama na serikali nani zaidi?Tz nchi ya maagizo, na kila mtu ni kambale kutoa maagizo kwa kwenda mbele, kaazi kwelikweli...