Shaka: Ni marufuku kwa hospitali za Serikali kumtoza Mama mjamzito kiasi chochote cha fedha wakati, kabla na baada ya kujifungua

Shaka: Ni marufuku kwa hospitali za Serikali kumtoza Mama mjamzito kiasi chochote cha fedha wakati, kabla na baada ya kujifungua

Hu

Huyo ndio msemaji wa CCm Taifa chama kilichounda serikali na kuikabidhi serikali ili isimamie ilani, Sasa wewe puuza maagizo yake Ndio utajuwa Ni nani
Kwani wameanza kusema hivo leo?

Au leo ndio limekua agizo jipya?😂😂😂
 
Kama mke wako atadaiwa mpigie ndio utajua yeye ni nani?
Na wewe umeingizwa mkenge?

TOZO za miamala ni kubwa kuliko Tozo za uzazi.

Achana na wanasiasa , fanya yako mwenyewe. Na huyo ni msemaji tu wa chama , atasema chochote
 
Nitachangia bila kuweka porojo za siasa. Hii sera utekelezaji wake ni mgumu sana.

Kundi la wajawazito, watoto chini ya umri wa miaka 5 na wazee ndilo linalohudhuria zaidi katika vituo vya huduma za afya na ndilo linapaswa kupewa msamaha kwa mujibu wa sera.

Hii hupelekea mzigo mkubwa wa gharama za uendeshaji kwa vituo hivi, na kuingia kwenye madeni (umeme, maji, dawa, taka nk).

Ushauri wangu:
1. Ujauzito sio dharula, wazazi wa mtoto wana muda wa miezi 9 kujipanga hivyo wachangie gharama kidogo za huduma isipokuwa kwa huduma za dharula.

2. Kila mtanzania awe na Bima ya Afya, itungwe sheria ya kuwezesha utekelezaji wa hili.

Mwisho: "Afya ni ghali, na hakuna matibabu ya bure, ukiona umepatiwa huduma bila malipo jua kuna mtu/taasisi/nk imetoa gharama kwa ajili yako."
 
View attachment 2328846
SHAKA "TUSIWATOZE FEDHA WAJAWAZITO"

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka amewataka watoa huduma kote nchini kuacha kuwatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua.

Shaka ametoa maelekezo hayo akiwa Jimbo la Bukene wilaya ya Nzega mkoa wa Tabora alipopokea kilio cha wakina mama wakati alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wakati wa ziara yake.
View attachment 2328851
"Naomba nitumie jukwa hili kuweka msisitizo kwenye maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa wizara ya afya pamoja na TAMISEMI juu ya kusimamia takwa la kisera la kutaka watoa huduma za afya kote nchini kutowatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua. Hapa Bukene DC na Mkurugenzi mmesikia kilio hiki naomba tusitishe tabia hiyo" Amesema Shaka
View attachment 2328849
Shaka amewaeleza wananchi hao kuwa tayari Rais Samia ameshatoa maelekezo kwa wizara ya afya nchini kufanya mapitio ya gharama za matibabu ili kuja na muongozo utakaowapunguzia mzigo wananchi. Hivyo waendelee kumuunga mkono kwa kumuombea dua na sala pamoja na kutoa ushirikiano kwa serikali anayoiongoza kwa kuchapakazi na kulipa kodi.
View attachment 2328852
Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wazazi Tanzania Ndg Gilbert Kalima ambaye ameambatana na Shaka katika ziara hiyo amewataka wananchi kujitokeza kuhesabiwa na kutoa ushirikiano kwa makarani siku ya sensa Agosti 23, 2022.
View attachment 2328850
'CCM Imara, Shiriki Uchaguzi Kwa Uadilifu na Jiandae Kuhesabiwa Agosti 23, 2022'

#CCMIMara
#KaziIendelee

Aache utapeli wa kijinga, hiyo porojo inapigwa kila siku na bado wa mama wanatozwa pesa.
 
Nitachangia bila kuweka porojo za siasa. Hii sera utekelezaji wake ni mgumu sana.

Kundi la wajawazito, watoto chini ya umri wa miaka 5 na wazee ndilo linalohudhuria zaidi katika vituo vya huduma za afya na ndilo linapaswa kupewa msamaha kwa mujibu wa sera.

Hii hupelekea mzigo mkubwa wa gharama za uendeshaji kwa vituo hivi, na kuingia kwenye madeni (umeme, maji, dawa, taka nk).

Ushauri wangu:
1. Ujauzito sio dharula, wazazi wa mtoto wana muda wa miezi 9 kujipanga hivyo wachangie gharama kidogo za huduma isipokuwa kwa huduma za dharula.

2. Kila mtanzania awe na Bima ya Afya, itungwe sheria ya kuwezesha utekelezaji wa hili.

Mwisho: "Afya ni ghali, na hakuna matibabu ya bure, ukiona umepatiwa huduma bila malipo jua kuna mtu/taasisi/nk imetoa gharama kwa ajili yako."
Mkuu uko sahihi 1000%

Ujauzito si dharula.

Ukiacha hata miezi 9 ya kusubiri kujifungua, kupata mimba tu huwa ni mipango. Kama uko kwenye reproductive age, na unafanya ngono zembe, huwezi sema umepata mimba kwa bahati mbaya. Unakuwa umejipanga 100%.

Tusifanye siasa kwenye mambo ya msingi.
 
Hivi kwani tatizo ni kutozwa tozo au huduma?

Mwambie zile Hospitali wanazotumia wao waheshimiwa wetu kuna sio tozo tu bali ni mitozo tena waifuata wenyewe hiyo mitozo.

Hivyo badala ya kurudia chorus zile zile miaka nenda rudi nendeni huo Hospitalu muhakikishe tunapata huduma kama mnazopata kule mnapozifuata tozo za hiari.
 
👏👏👏👏👏👏👏👏👏
Safi sana! Ila tutakoma zile nyodo za manesi
 
Hii itachangia watu kuzidi kuzaa kwa kasi,ilitakiwa watu wawezeshwe kiuchumi wachague hospital wanazotaka kwenda.
 
Ukiwa hujawahi kuitumikia serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania unaweza kuamini hiyo tozo itaondolewa. Wewe uliyeandika Rudi Bukene baadaye uje utwambie kama hawatozwi. Shaka aliwaambia wananchi wa Bukene wanachotoka kukisikia na wakashangalia. Waulize watumishi walitaka kusikia mshahara umepanda walichoambulia hakijulikani. Matamko kama haya yanawapa watumishi wa umma ugumu wa kufanya kazi zao. Serikali imeweka hizo tozo na si daktari Wala nesi na hazifutwi kwa kusherehesha kama Shaka anavyofanya.
 
👏👏👏👏👏👏👏👏👏
Safi sana! Ila tutakoma zile nyodo za manesi
Na upo hapo unaamini tozo zimefutwa. Pata ujauzito kajifungulie Bukene mahali tamko lilipotolewa halafu uje useme kama tozo zimefutwa. Bahati mbaya kubwa ni kuamini matamko ya wanasisa
 
Rais Samia ni jembe kwelikweli,tumuunge mkono
 
Rais Samia Suluhu anaupendo sana aliahidi kupunguza vifo vya mama na mtoto na ametimiza na sasa watatibiwa bure hili ni jambo jema sana
 
View attachment 2328846
SHAKA "TUSIWATOZE FEDHA WAJAWAZITO"

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka amewataka watoa huduma kote nchini kuacha kuwatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua.

Shaka ametoa maelekezo hayo akiwa Jimbo la Bukene wilaya ya Nzega mkoa wa Tabora alipopokea kilio cha wakina mama wakati alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wakati wa ziara yake.
View attachment 2328851
"Naomba nitumie jukwa hili kuweka msisitizo kwenye maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa wizara ya afya pamoja na TAMISEMI juu ya kusimamia takwa la kisera la kutaka watoa huduma za afya kote nchini kutowatoza fedha wanawake wajawazito wakati wa kliniki na wanapofika kujifungua. Hapa Bukene DC na Mkurugenzi mmesikia kilio hiki naomba tusitishe tabia hiyo" Amesema Shaka
View attachment 2328849
Shaka amewaeleza wananchi hao kuwa tayari Rais Samia ameshatoa maelekezo kwa wizara ya afya nchini kufanya mapitio ya gharama za matibabu ili kuja na muongozo utakaowapunguzia mzigo wananchi. Hivyo waendelee kumuunga mkono kwa kumuombea dua na sala pamoja na kutoa ushirikiano kwa serikali anayoiongoza kwa kuchapakazi na kulipa kodi.
View attachment 2328852
Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wazazi Tanzania Ndg Gilbert Kalima ambaye ameambatana na Shaka katika ziara hiyo amewataka wananchi kujitokeza kuhesabiwa na kutoa ushirikiano kwa makarani siku ya sensa Agosti 23, 2022.
View attachment 2328850
'CCM Imara, Shiriki Uchaguzi Kwa Uadilifu na Jiandae Kuhesabiwa Agosti 23, 2022'

#CCMIMara
#KaziIendelee
Huyu mjomba ni jembe kwelikweli
 
Mbona maneno hayo yapo miaka mingi na hatekelezeki. Alishindwa MAGU ?
 
Back
Top Bottom