TrioNeTwork
JF-Expert Member
- Aug 7, 2022
- 444
- 382
SHAKA ANAANZA KWA KUSEMA KUWA, RAIS SAMIA NI KIOO KINACHOAKISI THAMANI YA TANZANIA NA WATANZANIA,
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, amesema Rais Samia Suluhu Hassan ni kioo kinachoakisi utu na thamani ya Watanzania.
Shaka ameyasema hayo leo mjini Babati, mkoani Manyara wakati akisalimia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hasaan ambae alikuwa katika ziara ya siku ya mwisho ya ziara yake ya siku mbili mkoani humo.
"Samia Suluhu Hassan ni kioo kinachoakisi utu na thamani ya Watanzania kipaji chake cha siasa, kipaji chake katika uongozi ni chachu ya maendeleo endelevu, lakini ubunifu wake umeleta ari mpya ya kusukuma kasi ya maendeleo ndani ya taifa letu," amesema Shaka.
Shaka anaendelea kwa kusema kuwa Rais Samia kwa Uchapakazi wake tayari ameshaua ndoto nyingi za Wasaka Urais ifikapo Mwaka 2025 kwani kwa Umoja na Mshikamano wetu kama CCM kamwe hatuwezi kumwacha mtu anayefanya mambo makubwa kama Rais Samia Suluhu Hassan.
Shaka anasmea "imekwisha hiyo Tukutane 2030 ishallah kwa Majaliwa ya Mwenyezi Mungu,
Sikiliza hiyo video Mpaka Mwisho