Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapa kwangu Nina kuku wachacheJe wajua ya kwamba ndoto zaweza kuwa kweli? Wazungu wanasema dreams can come true...
Fanya yote maishani.. Pambana sana lakini usiache kumwomba Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema zote akujaalie mwisho mwema, uzee uliojaa fanaka na baraka.. Tele.. Wanazengo wanasema fainali uzeeni.. Basi Mwombe sana Manani akutunuku fainali ya ushindi.. Sio ya kutoa suluhu wala kufungwa..!
Pamoja na yote utakayojaaliwa pata walau hekari moja ukikosa kabisa basi walau nusu yake .. Kishapo
Jenga kajumba kako kazuri sana.. Huhitaji ghorofa wala nyumba kubwa utafuga majini na mashetani bila
kutaka na bila kujua
Fuga mifugo yako michache
1. Ng'ombe wa maziwa mmoja wakizidi wawili
2. Kuku wawili watatu wa mayai wa kienyeji
3. Ukiweza na ukipenda fuga na bata au sungura
4. Bwawa dogo la samaki
5. Fuga njiwa ukiweza na kasuku na ndege wengine wa leisure
Hii mifugo yote
Hawa wote watakusaidia sana kwenye ishu ya mbole
Kuzunguka nyumba una bustani zako za maua, garden na miti ya vivuli
Huko shambani sasa unatenga eneo la shamba dogo mazao mixer miti ya matunda.. Eneo lililobaki bustani za mbogamboga..
Utahitaji kisima pia
Pengine utahitaji vijana wawili watatu wa kukusaidia
Utahitaji chumba/ghala lenye vitendea kazi vyote...
Eat well.. Eat fresh.. Na kamnywesho kidogo😀😀😀View attachment 3261641View attachment 3261642View attachment 3261643View attachment 3261644
Jaribu kupanda halafu utamuona Areta Lyimo na chopa lake kwenye anga la nyumba yakoShamba bila mimea miwili mitatu ya bangi, sio shamba.
Haya ni matunda gani?Picha ni nyingi sana.. Nilizopost zinatoshaView attachment 3261727
Sawa, hizi hapa:Safi sana brother usinisahau zile mbegu tafadhali
Karibu sana!Natamani sana siku moja nifike huko brother