Sheikh Mattaka: BAKWATA ndio wengi kesho misikiti zaidi ya 300 Dar itatumika kwa ajili ya swala ya Idd

Sheikh Mattaka: BAKWATA ndio wengi kesho misikiti zaidi ya 300 Dar itatumika kwa ajili ya swala ya Idd

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Sheikh Mattaka anasema mwandamo wa mwezi Duniani kote hutangazwa na mamlaka husika na hapa Tanzania mamlaka hiyo ni BAKWATA.

Mattaka anasema Mufti hutangaza mfungo au mfunguo baada ya mwezi kuonekana na kamati ya muandamo wa mwezi kujiridhisha.

Sheikh Mattaka, anasema BAKWATA hufuatilia pia muandamo wa mwezi kwa nchi za Zanzibar na Kenya, lakini huko pia mamlaka husika zimesema mwezi haujaandama.

Hata hivyo Sheikh anasema Waislamu watakaoswali Eid kesho ndio wengi na hapa Dar es Salaam waumini watajaa misikiti zaidi ya 300 tofauti na hawa wanaoswalia viwanjani leo ambao hutumia viwanja viwili vitatu tu.

Chanzo: Channel Ten
 
Hoja sio uchache wa watakaoswali Eid, swali la msingi ni je mwezi uliandama jana leo ni Eid mosi au mwezi utaandama leo kesho Eid mosi?

Wanachokifanya BAKWATA wakati mwengine ni kuwalisha watu kwenye mchana wa Ramadhan, wameshindwa kwenda na nyakati tulizopo sahv.

Congo mwezi wa kuanza mfungo uliandama tar 12, tar 13 mfungo ukaanza na jana mwezi umeandama leo ni Eid mosi. Na Afrika Mashariki ni moja kijiografia.

Yaani BAKWATA wameshindwa kuwa na connection ya pamoja na mamufti wote wa Afrika Mashariki?
 
Hao bakwata nao walikua wapambe wa jiwe
Kama ni wachache yeye kinachomuwasha kitu gani?

2772022_1660090_FB_IMG_1514731600839.jpg
 
Back
Top Bottom