Sheikh wa Dar es Salaam aliyetenguliwa asema hana mpango wa kukata rufaa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Baada ya Alhad Mussa Salim kutenguliwa nafasi ya kuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam huku nafasi yake ikichukuliwa na Sheikh Walid Omary ambaye amekainishwa nafasi hiyo, Alhad Mussa Salim amesema ataendelea kuwa ndani ya baraza katika nafasi nyingine.

Amesema “Sijapewa taarifa rasmi lakini sina sababu ya kukata rufaa, ni maamuzi ya Baraza, ni chombo chetu tumekiweka na kina mamlaka ya kufanya hivyo, maamuzi ya wao kunitengua sijui wataitaja wao lakini haina shida.”


Chanzo: Clouds FM
 
Huyu Shehe ubwabwa alikua Ni chawa pro max[emoji1787]
 
Duuuh [emoji23][emoji23][emoji23] yy na kadinary Pengo walikuwa watiifu wa chama cha mapinduzi... Kweli maisha ni sawa na gwaride

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
Kutokana na Tabia zake Chafu na zisizompendeza hata Mwenyezi Mungu ( Allah ) huku Kutenguliwa Kwake Kumechelewa mno japo najua Mbinguni Kuni zake za Kuchomwa Moto vibaya zimeshahifadhiwa na zinamsubiri.
 
Huwa wanalipwa sh ngapi kwa mwezi
 
Kutokana na Tabia zake Chafu na zisizompendeza hata Mwenyezi Mungu ( Allah ) huku Kutenguliwa Kwake Kumechelewa mno japo najua Mbinguni Kuni zake za Kuchomwa Moto vibaya zimeshahifadhiwa na zinamsubiri.
Dah watu mna chuki sanaa ila kma kafanya dhambi anaweza akatubia na akasamehewa vizuri tu na Muumba wake
 
Dah watu mna chuki sanaa ila kma kafanya dhambi anaweza akatubia na akasamehewa vizuri tu na Muumba wake
Kumbe kuzijua Dhambi za Mtu na Kuzikemea au Kusikitika nazo ni Chuki Kwake / Kumchukia? Nilikuwa sijui hili Kiongozi wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…