Sheikh wa Wilaya ya Tanga awaomba waumini kutotumia Sanitizer kabla ya swala maana ina kilevi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426


Sheikh Mohamed Kombora amewaasa waumini wa Kiislam wa wilaya ya Tanga kuacha matumizi ya vitakasa mikono (Sanitizer) kabla ya swala maana vina kilevi kwa zaidi ya 60% na kwamba wakitumia watanajisi swala zao.

Chanzo : EATV

Nakala : FaizaFoxy
 
Sheikh hayupo sahihi. Alcohol ni "pure" siyo najisi na haitengui udhu wala swala labda uwe umeinywa kwa kuelewa kuwa unainywa ili ulewe. Hakuna anaekunywa sanitizer, unajipaka au kujipulizia tu na si kwa sababu ya kulewa.

Huyu ndiyo wale wanaoharamisha ambavyo havijaharamishwa na Allah.
 
Unapotea siku hizi!!!!
Na zile perfume je?
Why nchi za kiarabu na waislam wanatumia non-Alcohol/ Alcohol denant?
 
wacha wafu wazike wafu wao! Kuna vitu vingine huwezi kuvitetea, kuvisemea. acha kila mmoja na lwake .. Acha wanaoamini kusali walundikane, wanaoamini social distancing waamini etc
 
wacha wafu wazike wafu wao! Kuna vitu vingine huwezi kuvitetea, kuvisemea. acha kila mmoja na lwake .. Acha wanaoamini kusali walundikane, wanaoamini social distancing waamini etc
Kila mmoja atahukumiwa kivyake. Atakaesalia kwake akiwa na nia ya hucho anacho kifanya Mungu atamlipa kulingana na nia yake over

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je wanazitumia kama kinga au starehe? Vitu vingine vinahitaji simple logic tu mbona?

Jr[emoji769]
 
Tupe mbinu za jinsi ulivyoweza kusoma, kubobea na kuhitimu ujinga huko shuleni.
 
Toeni elimu kwa maustadhi wenu na maulamaa!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…