Sheikh Yahya: Mengi kuingia kwenye siasa, Kikwete Kushinda kwa Kishindo

Sheikh Yahya: Mengi kuingia kwenye siasa, Kikwete Kushinda kwa Kishindo

Hapa ni suala la imani kwa kila mmoja wetu nisingependa kumlaumu kitu. Kwa mengi zaidi wenye kupenda hii burudani ya Mnadhimu Shekh Yahaya Hussein endelea na tovuti hii.
Astrosheikh TZ - Home
 
Huyu Sheikh ni wa ajabu sana anatumia TV kufundiha uchawi na ushirikina jamabo ambalo ni hatari sana kwa Taifa.

Anachodai utabiri kilishawahi kuandikwa na Magazeti mengi miaka ya nyuma kuwa Mengi anataka kugombea urais kwa hiyo Sheikh hana jipaya bali kutaka kutangaza biashara zake tu ikiwa Mengi atajitosa.
 
Kikwete kushinda kwa kishindo 2010

Gloria Tesha

Daily News; Thursday, January 08, 2009 @21:15

Mtabiri maarufu nchini, Shehe Yahya Hussein, amemtabiria ushindi wa kishindo Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu mwakani na kwamba Serikali yake itakuwa ya Muungano wa Vyama vya Siasa.

Shehe Yahya amesema pia kuwa ushindi wa Kikwete utatokana na mwendelezo wake wa kufichua mafisadi na kuwafikisha katika vyombo vya sheria bila woga na kwamba katika uchaguzi huo, hakutakuwa na wizi wa kura, bali watu watashughulikia kutafuta fedha na mtandao wa mafuta.

Mtabiri huyo alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akitoa taarifa ya utabiri wake kwa mwaka huu kwa waandishi wa habari. Kuhusu ushindi wa Kikwete na hali ya kisiasa kuelekea mwaka wa uchaguzi, alisema utabiri wa mwaka huu uliopewa baraka zote na Umoja wa Mataifa, kuwa mwaka wa kuongozwa na nyota duniani, unaonyesha kuwa kiongozi mwenye jina lenye herufi J na K nchini, ndiye anayeongoza nchi.

“Pamoja na kuwa na herufi hizo, pia mwenye bahati kuwa katika uongozi wa awamu ya pili, ya tatu na sasa ya nne, awe mwenye kichwa cha bapa, uso wa meza na rangi ya maji ya kunde … mwenye nyota hiyo ni Kikwete na hivyo namtabiria kuendelea kuongoza nchi 2010,” alisema Shehe Yahya.

Alisema pamoja na kuwa na nyota hiyo inayoonyesha ushindi, endapo ataacha kuwatetea wanyonge kwa kupingana na baadhi ya matakwa ya watu wa chama chake, atashindwa vibaya katika uchaguzi na akakionya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuacha kiburi na kutambua kuwa hakitaongoza nchi peke yake mwaka huo.

Akifafanua kuhusu Serikali ya Muungano wa Vyama, alisema dalili zilizopo zinaonyesha Serikali ya Mseto na kuzitaja dalili hizo kuwa ni kampeni za kinyang’anyiro cha ubunge Mbeya Vijijini, ambako vyama vya upinzani vinaangushana na kuiunga mkono CCM.

Hata hivyo, alisisitiza hakutakuwa na wizi wa kura katika uchaguzi ujao na badala yake itaundwa Serikali ya Mseto na kwamba viongozi wakiwamo wabunge walioko madarakani watakaoendelea kufanya ufisadi na kutotenda haki kwa wanyonge, watashindwa vibaya katika uchaguzi huo.

“Mwaka huu vifo vya watu mashuhuri vitaongezeka sana na kutakuwa na kukwama kwa viongozi wapenda rushwa na wale watakaosema ukweli bungeni bila kuficha kitu, watachanua katika uongozi na maisha kifedha,” alisema.

Shehe huyo alimzungumzia pia Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, kuwa atajiunga na siasa mwakani na pia mgogoro wake na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, hauwezi kuendelea kwa kuwa herufi za majina yao ya pili ni M zikifuatiwa na herufi E na A ambazo kinajimu ni ndugu wa baba mmoja. Pia mnajimu huyo alimtabiria Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, kuwa kati ya sasa na Aprili mwaka huu, atapata kazi kubwa duniani ambayo itaiacha Dunia ikishangaa, hasa Watanzania.

Kuamini mambo ya UTABIRI hakuna tofauti na yule anayeamini akipata mkono wa albino atatajirika!!

Serikali makini haina muda wa kudangaya watu wake kwa kutumia watabiri kama navyofanya huyu mzee.

Mambo ya utabiri ni ya kishetani, ni imani za kipumbavu!!!

Huyu mzee kuna wakati anajibu maswali kwa wanaomuuliza yanayojenga utatanishi, mfano, mtu anauliza afanyeje ili ampate mpenzi anayemtaka? majibu ya huyu mzee anasema apate damu ya njiwa na vitu vingine nk na nk, anatofauti gani na mganga anayemwelekeza mteja wake atafute mkono wa albino???? inawezekana kwenye mahojiano ya TV anasema dmu ya njiwa lakini wakiwa wawili na mteja anasema damu ya albino!!!

Nini connection ya damu ya njiwa na kumpenda mtu awe mpenzi????

Kama kweli tumedhamilia kupambana na IMANI hizi potofu huyu mzee AZUILIWE kufanya mambo ya utabiri wake

Lakini na media zetu ni za ajbu kabisa, habari ya utabiri imeandikwa karibu na magazeti yote, huu ni UPUMBAVU!!!! kama media ni wajinga kiasi hicho kuamini mambo ya utabiri, vp raia wengine??
 
Mkuu YY,

Huwa SINA imani kabisa na ubashiri, siamini kama ubashiri wa Sheikh ni sahihi mpaka niyaone haya. From then nitamwamini.

Kuhusu suala la JK kuchukua nchi kiulaini sina wasiwasi sana na hilo litawezekana ENDAPO wapinzani (vyama vya Upinzani) watabakia kama tunavyowaona.

Kuhusu Mkapa I doubt amechemka, huenda yuko sahihi lakini binafsi siamini kuna jukumu KUBWA kwa kiwango hicho... Labda awe Katibu mkuu wa UN!

Let's wait n see

Asante Invisible

1.Mda ukifika akaulizwa vipi mbona havijawa, atapindisha oh Si umuoni Mkapa kapewa jukumu la usuruhishi nchini Kongo, Somalia n.k. Ni majukumu makubwa hayo, ni ya kimataifa!! Nilimanisha hivyo!!!

Ebu fuatilia utabiri aliokwishatoa huko nyuma na kama ilitokea kweli, ni vichekesho!

Utabiri wa Tanzania kuongozwa na mwanamke, alipoulizwa mbona ni JK, alisema huyo huyo Angalia tabasamu lake!!!,

2. Utabiri wake nauona kama wakati fulani una mkono wa kisiasa, angalieni utabiri wake wa jana. Wajanja wanajua wafuasi na waumini wa utabiri wa nyota ni wengi sana. Wengine kwao ni zaidi ya Yesu na Mtume SAW!!!, Ikibidi mtu yuko radhi kuwa mfuasi wa sehemu mbili. Wanajua impact yake kisiasa.
 
Huyu jamaa kweli haaminki, alishawahi kusema kuwa Zanzibar itaongozwa serikali ya mseto (CCM na CUF), nadhani siku, miezi hata miaka sasa imeshapita HAKUNA hata DALILI za kuwepo serikali ya mseto..........Naona mambo yake ya utabiri ni wizi wizi, tena ni wizi mtupu! Mbona Enzi za Mwalimu hakuwahi kutabiri UTUMBO kama huo???
 
Mnajimu maarufu wa Tanzania leo ametabiri kuwa mwaka 2009 utakuwa mwaka mgumu kiuchumi (mwaka wa matatizo); pia akadai kuwa mwaka 2010 uchaguzi hautakuwa na kuibiwa kwa kura kama chaguzi zilizopita.

The most interesting thing ni kuwa alibashiri kuwa mfanyabiashara mkubwa nchini kwa jina la Reginald Mengi ataingia kwenye siasa kabla ya 2011!

Je ubashiri wake utakuwa sahihi?

Mkuu...
Sijaona ubashiri wowote kwa huyu babu.Ameona mambo yanavyokwenda akaamua kuwafurahisha watu.Kuhusu Mkapa nani asiyejua kuwa anakubalika in international communities kutokana na alivyowapendelea alivyokuwa in power? Huu ni ujanja wakutafuta umaarufu..
 
Niliwahi kusoma katika makala moja katika gazeti la rai enzi hizo ikimtuhuumu sheikh yahya kuwa ni usalama wa taifa,hivyo huwa anapewa hint ya what will happen in the next few days hili hata kama litatokea watu wasishituke hasa kama suala lenyewe ni la kushitua.Hivyo kuweni makini na utabiri wa sheikh yahya.Jamaa alitoa ushahidi aliosema unapatikana katika kitabu kiitwacho THE DARKNESS SIDE OF MWALIMU,binafsi sijawahi kukiona ingawa sijafanya juhudi ya kukitafuta.

Dalili zote zinaonyesha dhahiri kuwa idara ya usalama wa taifa inamtumia mzee huyu kupre-empty mambo, kwa kutoa utabiri ili watu waamini kitakachojiri!! walengwa wakubwa wa ujinga huu ni watu wa IMANI fulani hapa nchini waaoamini mambo ya UTABIRI!

UTABIRI NI IMANI POTOFU!!! na kama usalama wa taifa wanamtumia mzee huyu kutrigger mind nzr za watu, basi HATUNA usalama wa taifa na mwelekeo wa taifa hili ni kuanguka!!!

Kwa dunia ya leo huwezi kuendesha nchi kwa kuwaaminisha watu mambo ya UTABIRI! ndio maana idadi kubwa ya watanzania ingali maskini kwa kuaminishwa ujinga! hata watu wengine hapa jamvini km Invisible,kibunango,gembe nk ukisoma maoni yao wangali bado kwenye UJINGA huu!

Halafu huyu mzee ni sheikh, sijui anawezaje kuunganisha mambo ya kishetani na ya Mungu halafu bado akawa anasema KWELI! kwa sababu GIZA(shetani) na nuru(Mungu) haviwezi kuwa pamoja!!!

Inawezekana mwandishi salman rushdie ktk kitabu chake cha SATANIC VERSES yuko sahihi!!!

Haiwezekani kuwa Mtabiri halafu ukawa kiongozi wa dini kwa wakati mmoja, nilitarajia kuona MAANDAMANO ya watu wa imani hii kupinga upotofu huu!!!!
 
HUYU MZEE APUUZWE!!!!!!!!! na MEDIA SHOULD STOP HIS "UTABIRI."...circulating on their media!!!
 
HUYU MZEE APUUZWE!!!!!!!!! na MEDIA SHOULD STOP HIS "UTABIRI."...circulating on their media!!!

Huh! Well, should this really be happening in a free society?
 
wakuu, hakuna usalama wa taifa wala usalama wa nini.huyu sheih mswalishaji wa waislam, ni mchawi tu. kwanza anapita akiuza uchawi tanzania nzima. hakuna aisiyemjua. ametembelea mikoa yote, na channel ten wanampenda sana huyu jamaa ndio maana huwa wanamwonyesha akisoma nyota. huwa nashindwa kuelewa kwanini wenzetu waislam wanamuona huyu mtu ni kiongozi wao wa dini, kwasababu ni mchawi kabisa.

alishawai kusema osama atakamatwa mwezi wa saba wa miaka ile, lakini hadi leo osama hatujamwona. marekani kwa ujanja wake wote, haijamkamata osama. sasa atuambie, osama aliyekamatwa ni osama gani? mbona hatujamwona akikamatwa? si ajabu huyu jamaa ni mmoja wa watu wanaofanya biashara ya viungo vya albino huyu. amelaaniwa kama shetani, ndio maana anatukuza uchawi. Mungu anakataza uchawi.
 
Ati, hivi kwanini watz bado tunashikilia uchawi? kwanini bado tunatoa vibali kwa waganga wa kienyeji, kwanini bado tunawaruhusu wapiga ramli, hivi tunajua kuwa haya ni mambo yanayoleta laana kwenye nchi?

Juzi hapa mtu aliyewahi kutabiri kuwa OSAMA ATAKAMATWA MWEZI WA SABA wa mwaka ule wa vita ya taliban, hadi leo hatujaona kichwa cha osama. na vyombo vya habari bado vinaonyesha mambo hayo, hivy vinakuwa encouraged. viongozi wa selikali kule mwanza na sumbawanga wameweka mikutano ati na waganga wa kienyeji, wakifikiria kuwa ndio watakaolimaliza tatizo la albino. Leo albino, kesho watasema mmasai, siku ingine watu warefu, siku ingine watu wafupi, siku ingine watataka kichwa cha rais au mbunge....nini uchafu huu? kwanini? kwanini hatuandamani kuamrisha selikali ifute vibali vya waganga wa kienyeji na wabashiri kama kina shehe yahya? .
 
Wachina, Wajapani, Wahindi, Wazungu..wote wana imani zao!

Ni sisi tunaelekea kuiga 100% toka kwa wengine!
 
Sijaelewa mkuu. wana imani gani, na je, sisi nasi tumwache Mungu wa kweli tuabudu na ku encourage utabiri wa nyota, ubashiri, uganga na ramli? nchi yetu itabarikiwa? No.
 
MUNGU ANACHUKIA UCHAWI NA WACHAWI
Uchawi ni imani zinazotokana na kazi ya shetani ndani ya ufalme wa shetani. Shetani anatumia wanadamu kwa nguvu zake(ambazo si kubwa kuliko nguvu za Mungu), kufanya vitu mbalimbali ili wanadamu wadanganyike na kujiunga kwenye ,yeye akiwa mkuu wao katika ufalme wake wa giza. Wanadamu wengi hizi ni wachawi tangu enzi za agano la kale. Watu wengi wanafanya kazi kwa kutumia uchawi maofisini, mahirizi yamefungwa viunoni, watoto wao wanawachanjia uchawi, watu wanatoa kafara hata watoto wao, na vitu vingi. Mambo haya yalikuwepo hata enzi za zamani hata kabla ya Yesu. Hivyo, katika Biblia, imani ya kichawi imetajwa na inatambuliwa kama ni imani ambayo ni ya kishetani, ni kinyume na mapenzi ya Mungu, na Neno la Mungu litawataka watu waikimbie kwa mioyo yao yote, na katu wasijaribu kufanya au kufuata mambo ya kichawi. Shetani anafanya mazingaombwe tu, ili kuwadaka watu, awaweke kwenye ufalme wake wa giza. Mwivi haji ila kuua, kuchinja na kuharibu, mwisho wa siku lazima atawaua na kuwachinja kama kuku tu vile apendavyo, pasipo na msaada wowote kwasababu upo chini yake. Shetani haji ili kuleta mafanikio kwa wanadamu, ila anakuja ili kuua kuchinja na kuharibu. Hata kama unaweza ukaona kama anakupatia mafanikio, ni kiini macho tu cha kukufanya uje kwake ili akuue na mkawe wote kule jehanamu. Kuna siku atakuua kabisa kusudi ukose hata nafasi ya kubadilisha maisha na kumfuata Mungu upone. Hebu tuangalie maeneo mbalimbali ambayo biblia inataja uchawi na nini Mungu anaongelea kuhusu hilo. Kuna maeneo mengi, lakini maeneo machache tu yataongelewa hapa.

Kumbukumbu la Torati 18:10, asionekane kwako mtu ampitishaye mwanae au binti yake kati ya moto wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kwamaana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana. (There shall not be found among you any one that maketh his son or his daughter to pass through the fire, or that useth divination, or an observer of times, or an enchanter, or a witch, Or a charmer, or a consulter with familiar spirits, or a wizard, or a necromancer. For all that do these things are an abomination unto the LORD: and because of these abominations the LORD thy God doth drive them out from before thee. Thou shalt be perfect with the LORD thy God.) Kwa maelezo ya kiingereza cha kisasa ni: Don't sacrifice your son or daughter. And don't try to use any kind of magic or witchcraft to tell fortunes or to cast spells or to talk with spirits of the dead. The LORD is disgusted with anyone who does these things, and that's why he will help you destroy the nations that are in the land. Never be guilty of doing any of these disgusting things! Hivyo tunaona kuwa, Mungu anakataza kabisa mambo ya kiuchawi, kutafuta bahati kwa kuangalia nyota,kuagua, kusoma nyota na majira kwa kutumia wachawi,kufuga uchawi na mambo yote ya kiuchawi ni chukizo kwa Mungu. Mtu anayetumia uchawi, anamaanisha kuwa uchawi ambao ni shetani, ni bora kuliko Mungu, na Mungu lazima atawahukumu watu hao.

Kitabu cha 2Wafalme 1:3,4, 17 (mlango wa kwanza wote), Mfalme Ahazia aliyemrithi babaye mfalme Ahabu wa Israel, alianguka kutoka kwenye dirisha la gorofa, akawa anaumwa. Badala ya kumwomba Mungu, yeye alituma wajumbe wande kuuliza kwa miungu ya Ekroni(waganga wa kienyeji, yaani kuagua) Baal Zebubu ili miungu hiyo itambue kama atapona au la. Mungu alikasirika sana, akatuma ujumbe kuuliza kuwa, Je, hakuna Mungu katika Israel hata mnaenda kuagua?basi kwakuwa umefanya hivyo, utakufa. Na kweli, mfalme alikufa kwasababu badala ya kumtegemea Mungu wa Ibrahim Isaka na Yakobo, yeye alitegemea miungu mingine ya kichawi. Mungu anachukia uchawi na atawahukumu wachawi wote.

Toka enzi ya zamani ya uasi wa mwanadamu, ni kawaida watu kutumia hirizi na madawa ili kulinda kazi zao, biashara n.k. yaani wako kwenye system ya mfumo wa utawala na utendaji wa shetani, wao ni maajenti wa shetani kwasababu wako kweye system yake. Watu wanatumia waganga wa kienyeji kama ndo solution ya matatizo yao. Watu wanasoma nyota, watu wanabashiri, wanaagua, wanaloga, wanatoa kafara watoto wao, wanawadhuru watu wengine n.k. pia wapo watu wanaofanya mazingaombwe, na watu wanawakusanyikia ili kuona maajabu, wanachukua utukufu kuwa wao ni wakubwa kumbe Mungu wetu ni mkuu kuliko vimazingaombwe vyao. Hata kama mtu atapata tatizo gani, ni bora akamsubiria Bwana kuliko kufanya uchawi. Mungu anachukia uchawi.

Katika Matendo ya mitume 8:9, Na mtu mmoja Jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa. Wote wakamsiiliza tangu mdogo hata mkubwa wakisema mtu huyu ni uweza wa Mungu ule mkuu. Wakamsikiliza kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake. Laikini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa wanaume na wanawake. Na yeye Simoni mwenyewew aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo. Hivyo hapa tunaona mtu mmoja wa mazingaombwe aitwaye simon, aliacha uchawi wake na akaamua kumfuata Yesu kwasababu Yesu ni mkuu kuliko uchawi.

Matendo 13:6, pia inasema kuwa, kulikuwa na mtu mmoja mchawi aliyejiita jina la Bar-yesu, alikuwa pamoja na Liwali. Watu walimtukuza mtu huyu kuwa ni mtu mkuu kwasababu ya uchawi wake. Sasa Paulo na Barnaba walipotaka kumshuhudia liwali habari za Yesu, yule mchawi alishindana na watumishi wa Mungu akitaka wasimshuhudie yule liwali. Paulo akampiga upofu kwa nguvu ya Jina la Yesu, akawa kipofu. Hivyo, tunaona hapa kuwa, nguvu ya Mungu, ndani ya Jina la Yesu tulilopewa wanadamu tupate kuokolewa kwalo, ina nguvu kuliko nguvu ya uchawi iwayo yote ile. Kwa Jina la Yesu, hakuna nguvu yoyote ile ya giza itakayoshinda. Na uchawi ni dhambi. Kama mchawi anazuia mambo ya kimungu, hata leo watu wa Mungu tunao uwezo kuwapiga upofu na itatokea.

Kutoka 22:18, Mungu alitoa amri ya hukumu ya kifo(kwa waisrael walipokuwa wanasafiri kipindi kile), kuwauwa watu wachawi. Hizi ni sheria ambazo Mungu aliziweka ili ziwaongoze wana wa Israel. "Usimwache mwanamke mchawi kuishi", "death is the punishment for witchcraft". Hata leo hii, kama kuna mchawi anayejaribu kusumbua maisha yako, usimwache kuishi. Isipokuwa, usitumie nguvu za mwili kwasasa kwasababu kupigana kwetu katika agano hili jipya si kwa damu na nyama, ni kwa kiroho kuzipiga falme na mamlaka, wakuu wa giza hili na majeshi ya pepo wabaya. Unachotakiwa ni kupigana naye katika ulimwengu wa roho, na unaweza ukamtamkia chochote kile kama Paulo alivyofanya, na kitatendeka kwa Jina la Yesu. Uchawi na kuabudu miungu mingine, ni chukizo kwa Bwana. Kusoma nyota, kubashiri, kuagua n.k, ni chukizo.

Mambo ya Walawi 19:29, Msile kitu chochote pamoja na damu yake(yaani kibudu) wala msifanye kuloga wala kutumia utambuzi. Don't eat the blood of any animal. Don't practice any kind of witchcraft. Kibudu ni kitu ambacho kimeuawa bila kumwagika damu ardhini. Mfano ni kuua wanyama kwa kunyonga etc. kinachotakiwa, ni kuwachinja ili damu imwagike na kutoka, ndio nyama safi hiyo. Pia Mungu anasema tusifanye uchawi wa aina yoyote ile. Remember, kama kuna shetani na uchawi, basi kuna Mungu, kama kuna nuru, basi kuna giza pia, kama kuna mchana basi kuna usiku pia, na kama kuna uzima wa milele basi kuna na jehanam. Ufalme wa Mungu ni dhahiri tofauti na ufalme wa shetani. Hakuna maswali. Ni vibaya sana kuacha ufalme wa Mungu na kufuata ufalme wa shetani. Ni hatari kwa mwanadamu. Ni hatari kwako kwenda kuchanja kwa mganga, kuloga,kuagua,kuomba utajiri kwa shetani/waganga,kutafsiri nyota n.k.

2Wafalme 17:17, wakawapitisha watoto wao waume na wake motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha. (And they caused their sons and their daughters to pass through the fire, and used divination and enchantments, and sold themselves to do evil in the sight of the LORD, to provoke him to anger.) They used magic and witchcraft and even sacrificed their own children. The Israelites were determined to do whatever the LORD hated.

Pia 2Wafalme 21:6, akampitisha mwanae motoni, akatazama bao, akafanya uganga, akajishughulisha na hao wenye pepo wa utambuzi, na wachawi; akafanya mabaya mengi machoni pa Bwana, hata kumkasirisha. (And he made his son pass through the fire, and observed times, and used enchantments, and dealt with familiar spirits and wizards: he wrought much wickedness in the sight of the LORD, to provoke him to anger) (and even set up the pole for Asherah there. Manasseh practiced magic and witchcraft; he asked fortunetellers for advice and sacrificed his own son. He did many sinful things and made the LORD very angry). Siku hizi kuna ma fortune tellers wengi tu, wengine tunawaona kwenye televisions, wasoma nyota, waganga, wengine wa mitishamba wengi tu wanaoamini nguvu za kiuchawi. Mungu ameandaa siku atakayowahukumu watu wote wa aina hii.


Zekaria 10:1,2, Neno la Mungu linasema; mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni. Kwa maana vinyago vimenena maneno ya ubatili, nao waaguzi wameona uongo, nao wameleta habari za ndoto za uongo, wafariju bure; (You can't believe idols and fortunetellers, or depend on the hope you receive from witchcraft and interpreters of dreams. But you have tried all of these, and now you are like sheep without a shepherd).

Malaki 3:5, The LORD All-Powerful said: I'm now on my way to judge you. And I will quickly condemn all who practice witchcraft or cheat in marriage or tell lies in court or rob workers of their pay or mistreat widows and orphans or steal the property of foreigners or refuse to respect me. (And I will come near to you to judgment; and I will be a swift witness against the sorcerers, and against the adulterers, and against false swearers, and against those that oppress the hireling in his wages, the widow, and the fatherless, and that turn aside the stranger from his right, and fear not me, saith the LORD of hosts) nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo, na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwaajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi asema Bwana wa Majeshi.

Wagalatia 5:20, inasema, basi matendo ya mwili ndio haya; uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo; katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.(Now the works of the flesh are manifest, which are these; Adultery, fornication, uncleanness, lasciviousness, Idolatry, witchcraft, hatred, variance, emulations, wrath, strife, seditions, heresies, Envyings, murders, drunkenness, revellings, and such like: of the which I tell you before, as I have also told you in time past, that they which do such things shall not inherit the kingdom of God) matendo ya mwili ambayo Neno la Mungu linasema ya kuwa wayatendayo hayo, hawataurithi ufalme wa Mungu. Wachawi wote hawataurithi ufalme wa Mungu, wataungua moto pamoja na shetani milele na milele. Hata wale wanaofanya ushirikina na mambo ya kienyeji, wote wako kwenye kapu moja la uchawi.

Wengi wetu ni wafanyakazi maofisini, aither ofisi za selikali au ofisi za makampuni ya watu binafsi. Wengine vilevile ni wafanya biashara kwenye ulimwengu wa ushindani mkubwa sana huu. Kwa macho yetu, au hata sisi wenyewe pengine tulishaona watu wanatumia, au tumetumia uchawi katika maofisi yetu, tumeenda kwa waganga ili kuzindika nyumba, magari, watoto au kazi zetu. Tumefunga mihirizi viunoni pamoja na kwamba tunaonekana tumevaa suti, tunapeleka pesa kwa waganga wa kienyeji ili watupatie uchawi wa kazi n.k. mambo haya hayajaanza leo, yamekuwapo muda mwingi na Mungu ameyakemea siku zote. Mambo yote ya jinsi hii ni chukizo kwa Mungu.

Ole wao wanaofanya uchawi, kwasababu ni chukizo kwa Mungu, na Mungu atawahukumu. Uchawi huo huo utawageuka na kuwatafuna wao wenyewe. Kwa kutumia uchawi mmewadhurumu watu wengi sana, mmewatia watu vilema, magonjwa, mmewaibia mali na kuwapiga chuma ulete, mmerudisha maendeleo ya watu nyuma, mmeua na kufanya watu misukule, mmesababisha ajali nyingi ili damu inapomwagika iwe kafara kwenu, mmewafarakanisha watu wasifanikiwe katika maisha yao, mmewaibia watu nyota zao, mmefunga mahirizi viunoni, badala ya kumtegemea Mungu, mnategemea uchawi, waganga, waaguzi, watabiri, wasoma nyota na watambuzi wa kishetani. Je, mnamdharau Mungu aliyewaumba kwa kutegemea vitu hivyo badala ya kumtegemea yeye, ina maana Mungu ameshindwa kukulinda na kukubariki hata ukamdharau kiasi hiki kwa kutegemea uchawi? Je hivyo ndivyo unavyomfikiria Mungu aliyekuumba? Unajua kuwa Mungu ndiye aliyeshikilia hata pumzi yako hata leo hivi? Unajua kwanini upo hai hadi leo: je ni kwasababu ya uchawi wako au Mungu amekuneemia akupe uhai ili pengine utageuka na kuiacha njia yako mbaya upate kupona? Mungu na akusaidie ewe uliye na mambo haya.

Enyi wabunge, mawaziri, wanasiasa na watu wote, ninani kati yenu sio mchawi? Ni nani, anyoshe mkono, ambaye wakati wa kampeni haendi kwa waganga wa kienyeji ili kujizindika na kupata uchawi? Kazi hizo mnamfanyia nani?mko kwenye system ya Mungu ya shetani? Ndio maana hata leo hivi hadi viungo vya binadamu vinauzwa, kwasababu wateja ni watu wa heshima tu. Yaani wafanya biashara, na maofisa mbalimbali. Tumetia laana kwenye nchi yetu, tumemwaga damu isiyokuwa na hatia kwenye nchi yetu.

Hakuna nchi yoyote duniani inayouza viungo vya binadamu wenzao, isipokuwa Tanzania. Hii ni nchi ya kwanza kwa kuuza viungo vya binadamu kama vile vya albino, ngozi za binadamu, matiti, sehemu za siri, vipara vya watu, n.k. Tanzania itajibu nini mbele za Mungu, ndio maana hata hatuendelei kwasababu laana imekalia nchi. Mafisadi ndio wanakula nchi na hakuna mtetezi kwasababu tumetegemea akili zetu sisi wenyewe na kuacha Kumfuata Mungu wa Ibrahim Isaka na Yakobo, Mafisadi ndio wanakula nchi na hakuna mtetezi kwasababu tumetegemea akili zetu sisi wenyewe na kuacha Kumfuata Mungu wa Ibrahim Isaka na Yakobo ambaye ndiye Mungu pekee wa kweli ambaye ulimwengu wote unatakiwa kumwabudu na kumheshimu. Ni heri yeye abadilikaye na kugeuka asikiapo sauti ya Bwana,kwasababu yeye aikazaye shingo yake asisikie maonyo, itavunjika na hatapata dawa. Mungu atusaidie watanzania.

Itakufaidi nini ewe mwanadamu ukifanya uchawi, ukaupata ulimwengu wote na faida zote, na kila kitu, halafu nafsi yako mwisho wa siku ikaishia kwenye ziwa la moto ambalo ni la milele? Inakufaa nini kumwasi Mungu wako kwasababu ya kazi tu, ukaipata hiyo kazi na kwenda motoni ukifa? What is your destiny after death, au hautakufa?utaishi milele? Dunia yenyewe si ya milele, itaisha,na Mungu atakuja kuhukumu walio hai na watu, wengine makao mapya ya miele na wengine moto wa milele. Jehanamu ipo,na ni dhahiri, Yesu aliitabiria, na kuonyesha kuwa moto na mateso yake hayaongeleki, ni heri kama hata kidole chako kikiwa ndicho kinachokukusesha, kikate, bora ukaingie mbinguni bila hicho kidole au kiungo chochote kuliko kuingia motoni navyo vyote. Hii ina maana kuwa, mateso ya huko ni makuu mno. Sio ya siku moja, au sio ya miaka hata mia tu ambayo wanadamu wengi wanamwasi mungu wakitengeneza maisha yao ya hapa duniani, ni zaidi ya hapo, ni miele na milele. Amina.
 
....nini uchafu huu? kwanini? kwanini hatuandamani kuamrisha selikali ifute vibali vya waganga wa kienyeji na wabashiri kama kina shehe yahya? .

...yote inatokana na triumph of hope over common sense and General experiences, sawasawa na waliosema Kikwete ni chaguo la mungu.
 
...yote inatokana na triumph of hope over common sense and General experiences, sawasawa na waliosema Kikwete ni chaguo la mungu.

Mbu
JK mwenyewe nilidhani kaacha, kumbe bado anaendelea. Kuna mtu alipost hapa JF sasa hivi ana import waganga toka Nigeria. Tusishangae tukiona anaweweseka madarakani kufanya mambo ya ajabu kila kukicha, sio yeye ni tunguli!
 
Sheikh Yahya Hussein:

Kuna tabiri ambazo naweza kumpa credit.

(a) Mwishoni mwa mwaka 2002 alisema kuwa Saadam Huessin atatolewa madarakani kwa nguvu mwezi Machi mwaka 2003. Ni kweli ilitokea hivyo

(b) Mwaka huo huo alisema kuwa kungetokea ajali ya chombo kikubwa sana cha anga; ni kweli Space Shuttle Columbia ilipasukia angani mwezi Januari mwaka huo wa 2003.


Lakini tabiri zake nyingi hazina ukweli.

(a) Wakati anasem Saddam atatolewa madarakani, alisema pia kuwa Osama bin Laden angeshikwa, kufariki au kuuwawa; lakini Bin Laden amekuwa anatoa kanda zake kila kukicha.

(b) Alisema kuwa rais wa Tanzania baada ya Mkapa angekuwa mwanamke. Sielewi kama huyu Kikwete (ambaye huko mitaani akina mama hawapumui) kweli ni mwanamke,

(c) Nadhani mwaka 1973 au 74 hivi alitabiri kuwa timu ya Yanga ingekuwa bingwa lakini ubingwa huo ulichukuliwa na Simba (au kinyume chake)

Hee,kulikoni tena?Hewa yote anatwaa yeye ama?Hii kali mkulu....
 
Huyu mganga wa kienyeji nae aacha kuwadanga Watanzania. Imani za kipumbavu kama hizi ndio zinaendelezwa na vyombo vya habari na mwishowe tunakuta Maalbino wanauwa kwa upuuzi kama huu. Huu ni utabiri gani .. eti watu mashuhuri watakufa.. hali ya uchumi itakuwa mbaya.. mbona haya mambo hayahitaji hata utabiri? Huyu ni tapeli anayeganga mlo wake wa kila siku na hakuna cha utabiri wala nini... upuuzi mtupu...

Supported sir!

Sijuia hata kama inaingia akilini, huyu mtu kutabiri katika mwanvuli wa dini fulani.

Hawa ni moja ya watu wanaochangia umaskini TANZANIA, wanaowaambia watu vaa nguo ya kijani utapata hela.

Ni ujinga sana, upumbavu usiosemeka,uzuzu wa ajabu.

Dunia ya sasa hawa watu wasiruhusiwe, lakini kuna jamii au kundi la watu bado wako karne ya 17, wanavienzi na kuvitukuza hivi vitu vinavyopromote ujinga!

Huyu naye aanzwe kumulikwa na kurunzi

Tapeli-UWIZI MTUPU-HUU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
mungu anachukia uchawi na wachawi
uchawi ni imani zinazotokana na kazi ya shetani ndani ya ufalme wa shetani. Shetani anatumia wanadamu kwa nguvu zake(ambazo si kubwa kuliko nguvu za mungu), kufanya vitu mbalimbali ili wanadamu wadanganyike na kujiunga kwenye ,yeye akiwa mkuu wao katika ufalme wake wa giza. Wanadamu wengi hizi ni wachawi tangu enzi za agano la kale. Watu wengi wanafanya kazi kwa kutumia uchawi maofisini, mahirizi yamefungwa viunoni, watoto wao wanawachanjia uchawi, watu wanatoa kafara hata watoto wao, na vitu vingi. Mambo haya yalikuwepo hata enzi za zamani hata kabla ya yesu. Hivyo, katika biblia, imani ya kichawi imetajwa na inatambuliwa kama ni imani ambayo ni ya kishetani, ni kinyume na mapenzi ya mungu, na neno la mungu litawataka watu waikimbie kwa mioyo yao yote, na katu wasijaribu kufanya au kufuata mambo ya kichawi. Shetani anafanya mazingaombwe tu, ili kuwadaka watu, awaweke kwenye ufalme wake wa giza. Mwivi haji ila kuua, kuchinja na kuharibu, mwisho wa siku lazima atawaua na kuwachinja kama kuku tu vile apendavyo, pasipo na msaada wowote kwasababu upo chini yake. Shetani haji ili kuleta mafanikio kwa wanadamu, ila anakuja ili kuua kuchinja na kuharibu. Hata kama unaweza ukaona kama anakupatia mafanikio, ni kiini macho tu cha kukufanya uje kwake ili akuue na mkawe wote kule jehanamu. Kuna siku atakuua kabisa kusudi ukose hata nafasi ya kubadilisha maisha na kumfuata mungu upone. Hebu tuangalie maeneo mbalimbali ambayo biblia inataja uchawi na nini mungu anaongelea kuhusu hilo. Kuna maeneo mengi, lakini maeneo machache tu yataongelewa hapa.

kumbukumbu la torati 18:10, asionekane kwako mtu ampitishaye mwanae au binti yake kati ya moto wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kwamaana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa bwana. (there shall not be found among you any one that maketh his son or his daughter to pass through the fire, or that useth divination, or an observer of times, or an enchanter, or a witch, or a charmer, or a consulter with familiar spirits, or a wizard, or a necromancer. For all that do these things are an abomination unto the lord: And because of these abominations the lord thy god doth drive them out from before thee. Thou shalt be perfect with the lord thy god.) kwa maelezo ya kiingereza cha kisasa ni: Don't sacrifice your son or daughter. And don't try to use any kind of magic or witchcraft to tell fortunes or to cast spells or to talk with spirits of the dead. The lord is disgusted with anyone who does these things, and that's why he will help you destroy the nations that are in the land. Never be guilty of doing any of these disgusting things! Hivyo tunaona kuwa, mungu anakataza kabisa mambo ya kiuchawi, kutafuta bahati kwa kuangalia nyota,kuagua, kusoma nyota na majira kwa kutumia wachawi,kufuga uchawi na mambo yote ya kiuchawi ni chukizo kwa mungu. Mtu anayetumia uchawi, anamaanisha kuwa uchawi ambao ni shetani, ni bora kuliko mungu, na mungu lazima atawahukumu watu hao.

kitabu cha 2wafalme 1:3,4, 17 (mlango wa kwanza wote), mfalme ahazia aliyemrithi babaye mfalme ahabu wa israel, alianguka kutoka kwenye dirisha la gorofa, akawa anaumwa. Badala ya kumwomba mungu, yeye alituma wajumbe wande kuuliza kwa miungu ya ekroni(waganga wa kienyeji, yaani kuagua) baal zebubu ili miungu hiyo itambue kama atapona au la. Mungu alikasirika sana, akatuma ujumbe kuuliza kuwa, je, hakuna mungu katika israel hata mnaenda kuagua?basi kwakuwa umefanya hivyo, utakufa. Na kweli, mfalme alikufa kwasababu badala ya kumtegemea mungu wa ibrahim isaka na yakobo, yeye alitegemea miungu mingine ya kichawi. Mungu anachukia uchawi na atawahukumu wachawi wote.

Toka enzi ya zamani ya uasi wa mwanadamu, ni kawaida watu kutumia hirizi na madawa ili kulinda kazi zao, biashara n.k. Yaani wako kwenye system ya mfumo wa utawala na utendaji wa shetani, wao ni maajenti wa shetani kwasababu wako kweye system yake. Watu wanatumia waganga wa kienyeji kama ndo solution ya matatizo yao. Watu wanasoma nyota, watu wanabashiri, wanaagua, wanaloga, wanatoa kafara watoto wao, wanawadhuru watu wengine n.k. Pia wapo watu wanaofanya mazingaombwe, na watu wanawakusanyikia ili kuona maajabu, wanachukua utukufu kuwa wao ni wakubwa kumbe mungu wetu ni mkuu kuliko vimazingaombwe vyao. Hata kama mtu atapata tatizo gani, ni bora akamsubiria bwana kuliko kufanya uchawi. Mungu anachukia uchawi.

Katika matendo ya mitume 8:9, na mtu mmoja jina lake simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa. Wote wakamsiiliza tangu mdogo hata mkubwa wakisema mtu huyu ni uweza wa mungu ule mkuu. Wakamsikiliza kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake. Laikini walipomwamini filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa mungu na jina lake yesu kristo, wakabatizwa wanaume na wanawake. Na yeye simoni mwenyewew aliamini akabatizwa, akashikamana na filipo. Hivyo hapa tunaona mtu mmoja wa mazingaombwe aitwaye simon, aliacha uchawi wake na akaamua kumfuata yesu kwasababu yesu ni mkuu kuliko uchawi.

matendo 13:6, pia inasema kuwa, kulikuwa na mtu mmoja mchawi aliyejiita jina la bar-yesu, alikuwa pamoja na liwali. Watu walimtukuza mtu huyu kuwa ni mtu mkuu kwasababu ya uchawi wake. Sasa paulo na barnaba walipotaka kumshuhudia liwali habari za yesu, yule mchawi alishindana na watumishi wa mungu akitaka wasimshuhudie yule liwali. Paulo akampiga upofu kwa nguvu ya jina la yesu, akawa kipofu. Hivyo, tunaona hapa kuwa, nguvu ya mungu, ndani ya jina la yesu tulilopewa wanadamu tupate kuokolewa kwalo, ina nguvu kuliko nguvu ya uchawi iwayo yote ile. Kwa jina la yesu, hakuna nguvu yoyote ile ya giza itakayoshinda. Na uchawi ni dhambi. Kama mchawi anazuia mambo ya kimungu, hata leo watu wa mungu tunao uwezo kuwapiga upofu na itatokea.

kutoka 22:18, mungu alitoa amri ya hukumu ya kifo(kwa waisrael walipokuwa wanasafiri kipindi kile), kuwauwa watu wachawi. Hizi ni sheria ambazo mungu aliziweka ili ziwaongoze wana wa israel. “usimwache mwanamke mchawi kuishi”, “death is the punishment for witchcraft”. Hata leo hii, kama kuna mchawi anayejaribu kusumbua maisha yako, usimwache kuishi. Isipokuwa, usitumie nguvu za mwili kwasasa kwasababu kupigana kwetu katika agano hili jipya si kwa damu na nyama, ni kwa kiroho kuzipiga falme na mamlaka, wakuu wa giza hili na majeshi ya pepo wabaya. Unachotakiwa ni kupigana naye katika ulimwengu wa roho, na unaweza ukamtamkia chochote kile kama paulo alivyofanya, na kitatendeka kwa jina la yesu. Uchawi na kuabudu miungu mingine, ni chukizo kwa bwana. Kusoma nyota, kubashiri, kuagua n.k, ni chukizo.

mambo ya walawi 19:29, msile kitu chochote pamoja na damu yake(yaani kibudu) wala msifanye kuloga wala kutumia utambuzi. Don't eat the blood of any animal. Don't practice any kind of witchcraft. Kibudu ni kitu ambacho kimeuawa bila kumwagika damu ardhini. Mfano ni kuua wanyama kwa kunyonga etc. Kinachotakiwa, ni kuwachinja ili damu imwagike na kutoka, ndio nyama safi hiyo. Pia mungu anasema tusifanye uchawi wa aina yoyote ile. Remember, kama kuna shetani na uchawi, basi kuna mungu, kama kuna nuru, basi kuna giza pia, kama kuna mchana basi kuna usiku pia, na kama kuna uzima wa milele basi kuna na jehanam. Ufalme wa mungu ni dhahiri tofauti na ufalme wa shetani. Hakuna maswali. Ni vibaya sana kuacha ufalme wa mungu na kufuata ufalme wa shetani. Ni hatari kwa mwanadamu. Ni hatari kwako kwenda kuchanja kwa mganga, kuloga,kuagua,kuomba utajiri kwa shetani/waganga,kutafsiri nyota n.k.

2wafalme 17:17, wakawapitisha watoto wao waume na wake motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa bwana, hata kumkasirisha. (and they caused their sons and their daughters to pass through the fire, and used divination and enchantments, and sold themselves to do evil in the sight of the lord, to provoke him to anger.) they used magic and witchcraft and even sacrificed their own children. The israelites were determined to do whatever the lord hated.

Pia 2wafalme 21:6, akampitisha mwanae motoni, akatazama bao, akafanya uganga, akajishughulisha na hao wenye pepo wa utambuzi, na wachawi; akafanya mabaya mengi machoni pa bwana, hata kumkasirisha. (and he made his son pass through the fire, and observed times, and used enchantments, and dealt with familiar spirits and wizards: He wrought much wickedness in the sight of the lord, to provoke him to anger) (and even set up the pole for asherah there. Manasseh practiced magic and witchcraft; he asked fortunetellers for advice and sacrificed his own son. He did many sinful things and made the lord very angry). Siku hizi kuna ma fortune tellers wengi tu, wengine tunawaona kwenye televisions, wasoma nyota, waganga, wengine wa mitishamba wengi tu wanaoamini nguvu za kiuchawi. Mungu ameandaa siku atakayowahukumu watu wote wa aina hii.


zekaria 10:1,2, neno la mungu linasema; mwombeni bwana mvua wakati wa masika, naam, bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni. Kwa maana vinyago vimenena maneno ya ubatili, nao waaguzi wameona uongo, nao wameleta habari za ndoto za uongo, wafariju bure; (you can't believe idols and fortunetellers, or depend on the hope you receive from witchcraft and interpreters of dreams. But you have tried all of these, and now you are like sheep without a shepherd).

malaki 3:5, the lord all-powerful said: I'm now on my way to judge you. And i will quickly condemn all who practice witchcraft or cheat in marriage or tell lies in court or rob workers of their pay or mistreat widows and orphans or steal the property of foreigners or refuse to respect me. (and i will come near to you to judgment; and i will be a swift witness against the sorcerers, and against the adulterers, and against false swearers, and against those that oppress the hireling in his wages, the widow, and the fatherless, and that turn aside the stranger from his right, and fear not me, saith the lord of hosts) nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo, na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwaajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi asema bwana wa majeshi.

wagalatia 5:20, inasema, basi matendo ya mwili ndio haya; uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo; katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa mungu.(now the works of the flesh are manifest, which are these; adultery, fornication, uncleanness, lasciviousness, idolatry, witchcraft, hatred, variance, emulations, wrath, strife, seditions, heresies, envyings, murders, drunkenness, revellings, and such like: Of the which i tell you before, as i have also told you in time past, that they which do such things shall not inherit the kingdom of god) matendo ya mwili ambayo neno la mungu linasema ya kuwa wayatendayo hayo, hawataurithi ufalme wa mungu. Wachawi wote hawataurithi ufalme wa mungu, wataungua moto pamoja na shetani milele na milele. Hata wale wanaofanya ushirikina na mambo ya kienyeji, wote wako kwenye kapu moja la uchawi.

Wengi wetu ni wafanyakazi maofisini, aither ofisi za selikali au ofisi za makampuni ya watu binafsi. Wengine vilevile ni wafanya biashara kwenye ulimwengu wa ushindani mkubwa sana huu. Kwa macho yetu, au hata sisi wenyewe pengine tulishaona watu wanatumia, au tumetumia uchawi katika maofisi yetu, tumeenda kwa waganga ili kuzindika nyumba, magari, watoto au kazi zetu. Tumefunga mihirizi viunoni pamoja na kwamba tunaonekana tumevaa suti, tunapeleka pesa kwa waganga wa kienyeji ili watupatie uchawi wa kazi n.k. Mambo haya hayajaanza leo, yamekuwapo muda mwingi na mungu ameyakemea siku zote. Mambo yote ya jinsi hii ni chukizo kwa mungu.

ole wao wanaofanya uchawi, kwasababu ni chukizo kwa mungu, na mungu atawahukumu. Uchawi huo huo utawageuka na kuwatafuna wao wenyewe. Kwa kutumia uchawi mmewadhurumu watu wengi sana, mmewatia watu vilema, magonjwa, mmewaibia mali na kuwapiga chuma ulete, mmerudisha maendeleo ya watu nyuma, mmeua na kufanya watu misukule, mmesababisha ajali nyingi ili damu inapomwagika iwe kafara kwenu, mmewafarakanisha watu wasifanikiwe katika maisha yao, mmewaibia watu nyota zao, mmefunga mahirizi viunoni, badala ya kumtegemea mungu, mnategemea uchawi, waganga, waaguzi, watabiri, wasoma nyota na watambuzi wa kishetani. Je, mnamdharau mungu aliyewaumba kwa kutegemea vitu hivyo badala ya kumtegemea yeye, ina maana mungu ameshindwa kukulinda na kukubariki hata ukamdharau kiasi hiki kwa kutegemea uchawi? Je hivyo ndivyo unavyomfikiria mungu aliyekuumba? Unajua kuwa mungu ndiye aliyeshikilia hata pumzi yako hata leo hivi? Unajua kwanini upo hai hadi leo: Je ni kwasababu ya uchawi wako au mungu amekuneemia akupe uhai ili pengine utageuka na kuiacha njia yako mbaya upate kupona? Mungu na akusaidie ewe uliye na mambo haya.

Enyi wabunge, mawaziri, wanasiasa na watu wote, ninani kati yenu sio mchawi? Ni nani, anyoshe mkono, ambaye wakati wa kampeni haendi kwa waganga wa kienyeji ili kujizindika na kupata uchawi? Kazi hizo mnamfanyia nani?mko kwenye system ya mungu ya shetani? Ndio maana hata leo hivi hadi viungo vya binadamu vinauzwa, kwasababu wateja ni watu wa heshima tu. Yaani wafanya biashara, na maofisa mbalimbali. Tumetia laana kwenye nchi yetu, tumemwaga damu isiyokuwa na hatia kwenye nchi yetu.

Hakuna nchi yoyote duniani inayouza viungo vya binadamu wenzao, isipokuwa tanzania. Hii ni nchi ya kwanza kwa kuuza viungo vya binadamu kama vile vya albino, ngozi za binadamu, matiti, sehemu za siri, vipara vya watu, n.k. Tanzania itajibu nini mbele za mungu, ndio maana hata hatuendelei kwasababu laana imekalia nchi. Mafisadi ndio wanakula nchi na hakuna mtetezi kwasababu tumetegemea akili zetu sisi wenyewe na kuacha kumfuata mungu wa ibrahim isaka na yakobo, mafisadi ndio wanakula nchi na hakuna mtetezi kwasababu tumetegemea akili zetu sisi wenyewe na kuacha kumfuata mungu wa ibrahim isaka na yakobo ambaye ndiye mungu pekee wa kweli ambaye ulimwengu wote unatakiwa kumwabudu na kumheshimu. Ni heri yeye abadilikaye na kugeuka asikiapo sauti ya bwana,kwasababu yeye aikazaye shingo yake asisikie maonyo, itavunjika na hatapata dawa. Mungu atusaidie watanzania.

Itakufaidi nini ewe mwanadamu ukifanya uchawi, ukaupata ulimwengu wote na faida zote, na kila kitu, halafu nafsi yako mwisho wa siku ikaishia kwenye ziwa la moto ambalo ni la milele? Inakufaa nini kumwasi mungu wako kwasababu ya kazi tu, ukaipata hiyo kazi na kwenda motoni ukifa? What is your destiny after death, au hautakufa?utaishi milele? Dunia yenyewe si ya milele, itaisha,na mungu atakuja kuhukumu walio hai na watu, wengine makao mapya ya miele na wengine moto wa milele. Jehanamu ipo,na ni dhahiri, yesu aliitabiria, na kuonyesha kuwa moto na mateso yake hayaongeleki, ni heri kama hata kidole chako kikiwa ndicho kinachokukusesha, kikate, bora ukaingie mbinguni bila hicho kidole au kiungo chochote kuliko kuingia motoni navyo vyote. Hii ina maana kuwa, mateso ya huko ni makuu mno. Sio ya siku moja, au sio ya miaka hata mia tu ambayo wanadamu wengi wanamwasi mungu wakitengeneza maisha yao ya hapa duniani, ni zaidi ya hapo, ni miele na milele. Amina.

asante sana kwa mchango mahiri uwasaidie watu hawa!!
Kwa mtu anayefikiri sawa sawa na kufanya tathmini pana juu ya mustakabali wa tanzania, zipo dalili kuonyesha tuendako si kuzuri!! Matukio kama ya mtoto mdogo (rama) kukutwa na kichwa cha binadamu ni ishara kuwa tumeruhusu shetani aonyeshe nguvu za milki yake!!!

Kinachosaidia nchi hii angalau iwe hivi ilivyo ni kwa ajili ya watenda haki wachache, wanaomsihi mungu muumba wa vitu vyote, asitupatilize kwa dhambi hizi mbaya tena zinazofanywa na viongozi!!! Huruma hiyo ina kikomo!!

Nilitegemea mjadala kama huu wote tunaoitakia mema nchi hii tungeungana kukataa mambo ya uaguzi,uchawi,utambuzi wa nyota nk, lakini hata wale wachangiaji wazuri kwenye mada zingine ambazo wakati mwingine ni za kipuuzi kabisa wako mbele kutoa maoni, watu km invisible,masatu,field marshal,kibunango na wengine, hawa ni wanafiki wakubwa! Hakuna hata chembe ya kulitakia taifa hili mema, ni wanafiki tu,

ni yapi hayo ya maana zaidi yanayolitia hasara taifa hili na kulipeleka gizani kama siyo imani hizi za kishetani??

ee muumba wa taifa hili tuhurumie na utusamehe na dhambi hii!! Tuonyeshe kujua nguvu na uwezo wako juu yetu, vile wengi kati yetu hawafahamu!
 
Back
Top Bottom