Ilikua jumamosi asubui natoa gari getini, mara naskia mke wa jirai yangu ananiuliza Shemeji utapita pale Petrol satation?
Kwa sababu nilikua narudi njuma nilikua sijamuona ila yeye alikua kasimama pembeni ya geti kwa nje.
Nikajibu-Oooh za asubui shem...Hapana shemeji nilishaweka jana ila kwani kuna kitu unaitaji... akajibu Ndio shem naitaji Luku.
Nikamwambia haina shida ila mimi nitachelewa kurudi.. akanijibu hamna tatizo bado iko kidogo.
Kwenye mida ya saa mbili na nusu napiga honi ili geti lifunguliwe....mara naona simu inaita, napokea ni shem ananiambia umenipita hapa nyuma..nikamwabia ok ngoja nimpe Masai akuletee luku yako.
Ilipofika kwenye saa nne na nusu ivi bado niko naangalia TV , msg inaingia... ''shem naomba uje uniingizie, mimi nimeshindwa, na baba...... amewapeleka watoto shule Arusha niko mwenyewe, samahani kama nakusumbua''
Nikazima TV fasta nikaingia chumbani nikampigia wife simu nikamwambia nampenda na kumkiss good night,, mke wangu yuko Mbeya alienda kwenye msiba wa bibi yake. Nikazima simu nikasali , nikalala.