Kuna rafiki yangu dada yao alipata matatizo kama hayo na alikuwa anakula vitasa si vya kitoto, siku moja anakwenda kumsalimia sister anamkuta na sun glasses kumbe macho yamevilia damu hataki aonekane. Ndugu waliamua kumtafutia nyumba ahame, walipata nyumba Kinondoni walilipa pango la mwaka. Dada alikuwa na kibarua chake, shost ananiambia baada ya miezi sita wanamuona dada na mimba kama ya miezi mitatu hivi, kumbe wameongea na shemeji na wameyamaliza na alikuwa anakwenda Kino kupiga mbonji. Ongeeni na dada yenu mjue anataka nini kwanza.