Sherehe za kuzima mwenge Tanga - Live

Risala imekwisha, sasa JK anakabidhiwa mwenge
 
sasa rais anatoa zawadi kwa watu na taasisi mbalimbali
 
Pwani kwa kuzindua mbio za mwenge, tanga kwa kuzima mwenge, bagamoyo mshindi wa kitaifa wa kukikmbiza mwenge na umezawadiwa sh mil 1.
Wadau waliopewa zawadi, Unicef, Maji na Uwagiliaji, n.k n.k
 
he! Takukuru nao wanapewa zawadi! TCTS nao wamo, NSSF, PPF, Executive Solutions- Mareale akucheza mbali, Barclays Bank, GTZ, TPA,
 
Pwani kwa kuzindua mbio za mwenge, tanga kwa kuzima mwenge, bagamoyo mshindi wa kitaifa wa kukikmbiza mwenge na umezawadiwa sh mil 1.
Wadau waliopewa zawadi, Unicef, Maji na Uwagiliaji, n.k n.k
...Mkuu Bagamoyo mshindi kitaifa wa kukimbiza mwenge maana yake nini? Huwa wanashindanishwa kwa vigezo gani au kwa kuwa ndio anakotoka JK??
 
Amemaliza, anarudi jukwaani ili kuzungumza, hilo ndilo tukio lililonifanya nianzishe thread hii, tumsikilize
 
Naona mic zinagoma "ebu cheki ile pale inafanya kazi?" anazipiga piga kujaribu, anaona bado hazifanyi kazi :"what is whrong?" (kwenye quotes ni maneno ya Muungwana), imeletwa mic nyingine, anaendelea kuwapongeza wananchiw a tanga kwa kumwalika na maandalizi ya sherehe zilizofana sana. Tumeona mambo makubwa ya chipukizi
 
Ni matumaini yangu kuwa hizo nguo hamtawanyang'anya, na hata mkiwanyang'anya mtazifanye, muwapelee watoto wenu? Nitasikitika sana nikisia baada ya hapa watoto hawa wamenyang'anywa hizi nguo
 
Anamkumbuka Nyerere. Ili kumkumbuka Nyerere ni wajibu wa kila mmoja kuonyesha kwa vitendo aliyoyasimamia Mwalimu. Kuhimiza upendo na kuepuka mambo yanayoleta chuki na utengano katika jamii.
 
Sherehe zimekabidhiwa kwa vijana kwa sababu wao ndio tegemeo la taifa la KESHO na KESHOKUTWA.
 
kaulimbiu-Kutunza vyanzo vya maji, kupambana na rushwa, ukimwi na kupambana na dawa za kulevya.

Kauli mbiu ya ukimwi ni ya kila mwaka kwa sababu tatizo hilo lipo siku zote. Anawashukuru waliojitokeza kupimwa. Kwenye maonyesho aliyoaangalia waliopimwa asilimia 2 tu ndio wana UKIMWI (kama watu 40 out of more than 1400). Arusha mwaka jana waliokutwa na virusi walikuwa asilimia saba.

Si vibaya kujenga utaratibu wa kupima kila mwaka. "Pima kila mwaka hata kama katika kipindi hicho ulikuwa mwaminifu wa kutosha na mwadilifu."

nawahakikishia watanzania kuwa dawa za kurefusha maisha zipo na mtanzania yeyote atakayeathirika na kuhitaji kutumia dawa, serikali itampatia dawa hizo, tena zinatolewa bure. Usikubali mahali popote ukauziwa dawa hizi.

Naamini kuwa atakayeuziwa ni yule atajkayeona haya, atakayefanya kimya na kutaka apewe dawa kwa siri.
 
Rushwa: Kauli mbiu iwe ya kila mwaka kwa sababu ni jambo lililo baya na limetawala sana katika jamii. Hakuna nchi iliyoweza kumaliza rushwa. Hata Marekani, kwenye kampeni za McCain na Obama, wanazungumzia kupambana na rushwa.

Tusiache rushwa ikawa sehemu ya maisha ya kawaida, tutakwisha.
Serikali itaendelea kuongeza uwezo wa kisheria na kitaasisi kupambana na rushwa.

Maji na Mazingira:
Sijambo la hiari kuhifadhi maji na mazingira. Tutunze vyanzo vya maji na mazingira kwa faida yetu na vuizazi vijavyo. Tusipofanya hivyo tutaangamia. hali sasa si nzuri, maeneo mengi maji yamepungua na yanaendelea kupungua kutokana na uharibifu wa mazingira. Mwenye umri kama wangu ajiulize, vile vijito vilivyokuwa vinatirisha maji vipo?
 
Serikali inatambua jukumu lake kuhifadhi mazingira na maji, kuboresha sheria kwa nia njema. Tuliposema watu wasilime mita 60 kutoka kando ya mito, wapo wanaotulaani hadi leo lakini tusiwaendekeze, tukiwaendekeza ndio hatari yetu sote. Tuendelee kuwabana na kuwahimiza kwa sababu tukilima mpaka kwenye mito, itakauka... mito inahifadhiwa na miti.

Tumefanya jitihada za kutambnua vyanzo vya maji na hatua za kuhifadhi zimefanyika.

Mbeya, kote nilikopita nimepata taarifa kuhusu vyanzo walivyotambua na hatua zilizochukuliwa, natamani kila wilaya ingefanya vile
 
Tunapomkumbuka Baba wa Taifa, hatuna budi tukumbuke kuwa alikuwa mtu wa kimataifa. Aliyejihusisha kikamilifu na masuala ya kimataiafa kwa maisha yake, akiwa rauis na hata baada ya kustaafu. Alijihusisha na masuala ya ukombozi wa afrika, ushirikiano wa kanda, pia alijihusisha na ushirikiano wa nchi za afrika na zile zinazoendelea na mataifa yote duniani. Alisisitiza sana ushirikiano kwa kutambua kuwa tanzania si kisiwa, bali ni sehemu ya dunia na kwamba yanayotokea sehemu nyingine yanatuhusu na yatatuathiri.

Aliona umoja ni nguvu miongoni mwa nchi masikini. alipigania ushirikiano w akiuchumi wa kikanda. alifadhaika EAC ilipokua 1977, alifurahi ushirikiano wa AM ulipofufuliwa.
 
Mwenge mwenge. Nimempigia mzee wangu asubuhi ya leo, alichoniambia ni kwamba am late nawai kwenye kuzima mwenge.
Nikamuuliza what is this mwenge staff about? Akawa hana cha kusema, nikajua ni urithi wa CCM ambao hauna maana yoyote zaidi ya kuspend tax payer money.

Nadhani Tanzania inabidi tuwe tuna direct vote za kuchagua mambo ya kiwehu kama haya. Yaani kwenye uchaguzi wa 2010 kuwe na option ya kama unataka mwenye uendelee vote Yes na kama hutaki vote NO. hii itatupa power wananchi kuondoa loophole kama hizi.
 
yanayotokea duniani yanatuhusu, tuna wajibuw a kuyafuatuilia, kuyatambua vizuri na kujihusiaha nayo ili kuona namna ya kutumia manufaa na kukabili athari. tangu 2006 uchumi wa dunia haujatulia, unapita katika misukosuko, mitikisiko mikubwa. Imekuwa na athari kwa ustawi wa uchumi wa nchi yetu na dunia kwa jumla.

Athari kubwa ya kwanza ni kuongezeka kwa bei ya mafuta duniani na kusababisha kuongezeka mfumko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha.

2006, ndio tatizo limeanza, dec 2005 pipa la mafuta dola 50, julai mwaka jana 150 dola.

Matokeo yake ni kupandsa kwa nauli, mahali fulani waliniambia nauli zimepanda, nyie watu wa serikali ni hovyo sana, kazi imewashinda. Nikaaambia kuwa mafuta yanapopanda bei uarabuni tunakoyanunua, hayawezi kushukia bei yakifika Korogwe.
 
mwaka jana likatokea tatizo la kupanda kwa bei za vyakula duniani. kutokana na kupanda kwa bei za mafuta, mataifa yalianza kutafuta namna ya kuopunguza matumizi ya mafuta kwa kupata nishati mbadala. wakapanda mazao ya kuzalisha mafuta badala ya dizeli na petroli. Matiokeo yake ni upungufu mkubwa wa chakula duniani, kulikofuatiwa na kupanda kwa bei za vyakula hivyo kuongeza ukali w amaisha.

Marekani wanatumia mahindi na miwa kupata ethanol, mawese kupata dizeli, wanachokifanya sasa, hawaachi muhindi ukabeba hindi, wanalikata wanatengenez mafuta. wanapunguza sana chakula duniani.

mwaka huu lilipotokea tatizo tukafuta ushuru (VAT) kwa vyakula, tukawaagiza waingize tani wakapata tai 3000 tu. kenya walikuja kwentu tuwauziw wakitaka tani laki 2, sisi akiba yetu tani laki mioja unusu, tukawauzia tani elfu 10
 

..mwenge una maana yake,inayotokana na asili ya lengo lake.

..hivi sasa umetekwa na baadhi ya watu na kufanywa ndio mali yao.

..mwenge ni wa watanzania wote.
 
Sasa limezuka tatizo jingine kubwa zaidi, kuyumba kwa mfumo wa fedha. Limesababisha kuyumba na kufilisika kwa benki kubwa na masoko ya hisa. Wakubwa wameanza harakati za kuokoa kwa kutoa fedha. Uchumi wa dunia unayumba sana.

Haya ndiyo mataifa makubwa yanayotuhusu kwa biashara ya misaada. Kwa hiyo na sisi tutaathirika. Kwa sasa, watalaamu wa uchumi nchini, BOT na wizara, wanafanya tathmini ya jinsi tutakavyoathirika. Wanaendelea kutoa ushauri wa hatua za kuchukua. Tutawataarifu kila hatua zitakazochukuliwa.

Inaelekea kuwa athari zitakuwa kubwa sana kutokana na hali ambayo hatukuisababisha sisi,
kuna kila dalili kwua uchumi wa dunia utaporomoka.

IMF imebashiri kuwa kutokana na msukosuko huu mkubwa, kasi ya ukuaji wa uchumi w adunia itapungua, dunia itaingia kwenye recession, itapungua kutoka asilimia 5 na kufika asilimi 3 mwaka ujao. Tanzania si kisiwa, na katika zama hizi za utandawazi, mtikisiko huu wa uchumi wa dunia una madhara kwetu.

Bahati nzuri athari zake hazijafika kwetu hadi sasa, lakini zipo njiani. Nchi zetu zipo nje ya mtandao wa mifumo ya fedha ya kimataifa, hivyo tupo salama.

Akiba yetu ya fedha za kigeni ipo salama kwa sababu kwa kiasi kikubwa zipo chini ya usimamizi wa serikali yetu. Mabenki yaliyoanguka si mabenki ambayo tumeweka fedha zetu.

BOT inaondoa fedha kwenye mabenki ya biashara kila inapowezekana kila tilipoziweka kwa maana tumeona mabenki yanafilisika. Kuna wasi wasi kuwa iwapo tatizo litaendelea, nchi za afrika pamoja na tz zitaathiriwa, hata imf inatabiri kuwa ukuaji wa uchumi wa Afrika utashuka kutoka asilimia 9.6 kwenda asilimia 6.3 mwakani.

Miskosuko, kupungua kwa mapato kwa nchi tajiri kumepunguza uwezo wao wa kununua bidhaa kwetu-masoko yetu yanapungua. Kuna uwezekano wa kupungua kwa mapato yanayotokana na utalii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…