Wakusoma 12
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 4,035
- 11,462
Very painful Karne ya ishirini na moja unaruhusu binadamu mwenziyo kuuawa na kuteswa kwa kisingizio Cha kutekeleza majukumu. Nani asiyejua Kuna bahati mbaya na ndiyo maana kwenye makosa ya mauaji yapo ya kukusudia na Yale ya kutokusudia. Sasa inakuwaje bunge letu, Baraza la mawaziri pamoja na Rais ambao kimsingi wanajukumu la kuhakikisha haki ya Kila mtanzania ya kuishi inalindwa kwa gharama kubwa walikubali kabisa kutunga na kupitisha Sheria ya namna hii????. Kwenye maisha Kuna kukosea lakini makosa hayo yote yanapimwa na chombo chetu Cha mahakama ili kuthibitisha uhalai wa kosa husika. Leo hii tunasema police force hawatekwlezi wajibu wake lakini kiuhalisia Kuna kitu tulijikwaa hapo nyuma kuruhusu Sheria hii kutumiwa na wahuni. Kimsingi idara ya usalama wa taifa haiwajibiki kwa chombo chochote Cha nchi isipokuwa Rais pekee Sasa unajiuliza Hawa wabunge wetu waliamua kuruhusu kikundi kimoja kupewa ruhusa ya kuwaua watanzania kwa kisingizio cha usalama? Civil rights zipo wazi na makosa yake Yana hukumu zake Sasa kwanini tumefika huku? My heart is breeding.