Dodoma Demand
Senior Member
- Oct 6, 2021
- 130
- 74
Poleni na majukumu ya kulijenga taifa,
Hapo kabla ya sheria mpya ya madini ya mwaka 2017,haijatungwa na kupitishwa, wakaguzi wa madini migodini walikuwa wanaenda kwenye vituo vya ukaguzi, hasa migodi mikubwa na ya kati kwa utaratibu wa mzunguko/rotations yaani leo upo hapa kesho pale, ili kukwepa mtu mmoja kukaa eneo moja kwa wakati wote kama misingi ya ukaguzi inavyohitaji. Hili lilikuwa linapelekea kuwa na makazi tofauti na sehemu za ukaguzi na kusababisha uthibiti wa biashara ya madini kuwa mgumu.
Baada ya marekebisho ya sheria mpya, mkaguzi anapaswa kukaa eneo la ukaguzi, ikiwa na maana stations kama sheria inavyosema. Hii itapelekea mkaguzi kukaa kituo kimoja aidha mpaka mgodi ufungwe au itokee hali nyingine ya kubalisha. Hili ni jambo jema, inawezekana likasaidia kupunguza matumizi ya wizara kama ilivyoelezwa. Japo pia linaonekana litakuwa na changamoto zake kiukaguzi. Kuanzisha MASOKO YA MADINI KATIKA KILA MKOA AMBAPO KWA SASA, Wizara yenye dhamana na MADINI imejenga masoko 28 katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo.
Dhana inayotumika ni sawa kabisa na DHANA ya MASOKO YA USHIRIKA kipindi cha MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE ambapo kulikuwa na SOKO moja KWENYE ENEO MAALUMU - (MKOA KWA SASA). Ni mtazamo wangu tu na kueleweshana mawili matatu, Je watumishi wa WIZARA HIYO WATATUVUSHA KWENYE MAISHA YA KUKAA KWENYE KITI - BADALA YA KUFUKUZA FUKUZA MACHINGA/ PANGA PANGA MACHINGA KILA SIKU....
Nawasilisha
Hapo kabla ya sheria mpya ya madini ya mwaka 2017,haijatungwa na kupitishwa, wakaguzi wa madini migodini walikuwa wanaenda kwenye vituo vya ukaguzi, hasa migodi mikubwa na ya kati kwa utaratibu wa mzunguko/rotations yaani leo upo hapa kesho pale, ili kukwepa mtu mmoja kukaa eneo moja kwa wakati wote kama misingi ya ukaguzi inavyohitaji. Hili lilikuwa linapelekea kuwa na makazi tofauti na sehemu za ukaguzi na kusababisha uthibiti wa biashara ya madini kuwa mgumu.
Baada ya marekebisho ya sheria mpya, mkaguzi anapaswa kukaa eneo la ukaguzi, ikiwa na maana stations kama sheria inavyosema. Hii itapelekea mkaguzi kukaa kituo kimoja aidha mpaka mgodi ufungwe au itokee hali nyingine ya kubalisha. Hili ni jambo jema, inawezekana likasaidia kupunguza matumizi ya wizara kama ilivyoelezwa. Japo pia linaonekana litakuwa na changamoto zake kiukaguzi. Kuanzisha MASOKO YA MADINI KATIKA KILA MKOA AMBAPO KWA SASA, Wizara yenye dhamana na MADINI imejenga masoko 28 katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo.
| Soko kuu la Dhahabu Geita |
| Soko la Dhahabu Kahama |
| Soko la Dhahabu Singida |
| Soko la Dhahabu Chunya |
| Soko la Dhahabu na Vito Ruvuma |
| Soko la Dhahabu na Almasi Shinyanga |
| Soko la Dhahabu Katavi |
| Soko la Madini Kigoma |
| Soko la Dhahabu Tabora |
| Soko la Dhahabu Mara |
| Soko la Dhahabu Madini Mbeya |
| Soko la Bati Kagera |
| Soko la Dhahabu na Almasi Mwanza |
| Soko la Dhahabu Songwe |
| Soko la Dhahabu na Vito Iringa |
| Soko la Vito Tanga |
| Soko la Dhahabu Singida - Sekenke |
| Soko la Dhahabu Manyara - Mbulu |
| Soko la Dhahabu Morogoro |
| Soko la Dhahabu Dodoma |
| Soko la Dhahabu Manyara - Babati |
| Soko la Vito Tunduru Ruvuma |
| Soko la Dhahabu na Vito Lindi |
| Soko la Madini Mtwara |
| Soko la Vito Mahenge |
| Soko la Vito Arusha |
| Soko la Madini Kilimanjaro – Same |
| Soko la Madini Dar es salaam |
Dhana inayotumika ni sawa kabisa na DHANA ya MASOKO YA USHIRIKA kipindi cha MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE ambapo kulikuwa na SOKO moja KWENYE ENEO MAALUMU - (MKOA KWA SASA). Ni mtazamo wangu tu na kueleweshana mawili matatu, Je watumishi wa WIZARA HIYO WATATUVUSHA KWENYE MAISHA YA KUKAA KWENYE KITI - BADALA YA KUFUKUZA FUKUZA MACHINGA/ PANGA PANGA MACHINGA KILA SIKU....
Nawasilisha