sheria ya mirathi msaada please

Joined
Jan 19, 2013
Posts
43
Reaction score
1
wana jf naomba kufahamu kama mtu mwenye umri uliozidi miaka 18 na ni mtoto wa nje ya ndoa ana haki ya kurithi mali za marehemu babake ikiwa babake hakuwahi kumthibitisha kuwa ni mtoto wake na alishathibitisha kwa mandishi kuwa mali zake fulani warithi watoto wake wa ndani ya ndoa ambao ni wadogo na wanaxoma? je kama ana haki ya kurithi ni pasu kwa pasu na mke wa marehemu au kwa kiasi anapaswa kupata huo urithi?plz ndugu zangu naomba mxada wenu.
 
Wewe unawezaje ku prove mbele ya mahakama kwamba huyu bwana alikuwa baba yako?
 
matter z not 2 pruvu wether this child is my fathers or not but what i need is sheria inamtambua mtoto huyu kama mrithi halali au lah?na kama n mrithi halali je ana haki ya kuchukua baadh ya v2 ambavyo babake alshvtoa kwa ndguze tena kwa maandishi?na kama anaruhusiwa je n kwa asilimia ngapi?
 

Nipe contacts zako (pm) then nitakufahamisha sheria inasemaje kuhusu mtoto wa nje ya ndoa. By the way ilishawahi elezewa humu huko nyuma.
 
ataridhije mali zilizochumwakwa ushirikiano na mwanamke mwengine? Hana lake unless kungekuwa na wosia..... au kama kungekuwa na mali ambazo zinajulikana alichuma baba na mamz wa mtoto wa nje ....la asahau
 
Justin your case is very complicated as I have learned few things which will trigger some noise once you raise your concern.

1. The late had never revealed to have a child (Illegitimate)
2. The late wrote the will and allocate all his assets to beneficiaries who are his kids
3. You are not appearing anywhere as a proof that you are also his kid so you deserve your part

Na ndiyo maana nikaulize would you be in the position to prove that he was your dad??? Kinyume na hapo hata mimi ningesubiri tajiri yoyote akifa then natokea nasema mimi ni mtoto wake.
 
go for DNA taste, then nenda mahakaman udai chako kama mtoto wa marehem. huwezi pata pasu, mtagawana kwa ratio/asilimia.
 
itz us who we are distubd by that person because our late dady allocated all his assets to me and my young brother who we are both studyng.on top of that he did all those thngz documentally but still mahakamani wanaendlea kumkandamiza mama ye2 ambaye anakabiliwa na jukumu zito la kutuxomesha sisi.
 
ndo nahtaji ifahamu iyo ratio ikiwa kuna watoto wa4 wa2 n wa nje ya ndoa na wanajitegemea na wa2 n wa ndani ya ndoa na wanaxoma na mke wa marehemu
 

MIRATHI & MFANO WA KUANDIKA WOSIA.


Imeandaliwa na:
Utti. A.Mwang’amba:
Centre for Widows and Children Assistance (CWCA)
S.L.P. 60202, Simu: 0754 693892 or 0787 088513
Barua pepe : childrenwidows@yahoo.co.in or widows.children@gmail.com
Dar es Salaam,
Tanzania.
East Africa



1.0. Mirathi nini?
Ni taratibu mbalimbali za kisheria zinazoongoza uangalizi , usimamizi , umiliki na hatimaye ugawaji wa mali na pengine hata kumaliza madeni ya marehemu pamoja na mazishi.

1.1. Aina za mirathi.
a) Mirathi palipo na wosia .
b) Mirathi pasipo wosia.

2.0. Sheria za mirathi itumikayo Tanzania imegawanyika katika sehemu tatu:-
i) Sheria ya Urithi ya India1865.
ii) Sheria ya Kiislamu.
iii) Sheria ya Kimila.

i)Sheria ya urithi ya India ya 1865 :- Hii ni sheria ya kiserikali na inatumika pale ambapo itaonekana kwamba marehemu alikuwa hafuati sheria za kislamu wala taratibu za kimila na desturi. Na hutumiwa na watu ambao si waislamu , pamoja na watu wengine ambao si wazawa wala waislamu

Warithi katika sheria hii :-
Ø Mke/mume wa marehemu.
Ø Watoto.
Ø Wazazi, kaka na dada za marehemu.

Mgawanyo wa mali kwa mujibu wa Sheria ya Urithi ya India:-

Ø Kama marehemu ameacha mjane na watoto watapata kama ifuatavyo; mjane1/3 na watoto 2/3 ya mali yote ya marehemu ambayo hugawiwa sawasawa.

Ø Kama marehemu hakaucha watoto , mjane atapata ½ na ½ nyingine hugawanywa sawasawa kati ya wazazi , kaka na dada za marehemu.

Zingatia: Kwa mujibu wa sheria hii watoto wa nje ya ndoa hawana haki ya kurithi isipokuwa kama kuna wosia na katika wosia huo wawe wamerithishwa mali.

ii) Sheria ya kiislamu
Hii hutumika kwa wafuasi/waumini wa dini ya kislamu.

Warithi katika sheria hii:-
Ø Mjane.
Ø Watoto.
Ø Wazazi, kaka na dada za marehemu.

Mgawanyo wa mali kwa mujibu wa Sheria ya Kiislamu :-

Ø Mjane /wajane 1/8 ya mali ya marehemu kama marehemu ameacha watoto. Kama hakuacha watoto wajane watapata ¼ ya mali iliyoachwa na marehemu.
Ø Watoto wa kiume 2/3.
Ø Watoto wa kike 1/3.
Ø Wazazi / ndugu 1/6
Zingatia:
Ø Mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa hana haki ya kurithi mali isipokuwa kama kuna wosia.
Ø Pia kwa mujibu wa sheria hii muislamu haruhusiwi kuwosia mali yake yote , anaweza kuwosia 1/3 tu ya mali yake na 2/3 ni lazima igawanywe kwa warithi halali kufuatana na sheria ya kiislamu.
ii) Sheria ya kimila
Hii hutumika pale ambapo marehemu aliishi kwa kufuata mila na desturi za kabila lake.

Warithi katika sheria hii:-
Ø Watoto
Ø Kama marehemu hakuacha watoto mali yake itarithiwa na baba , mama , kaka ,dada ,wajomba na shangazi zake.

Mgawanyo wa mali kwa mujibu wa Sheria ya Kimila :-
Urithi katika sheria za mirathi ya kimila umepangwa katika madaraja matatu.

Ø Daraja la Kwanza : Mtoto wa kwanza wa kiume wa nyumba hupata sehemu kubwa ya mali ya marehemu

Ø Daraja la Plil: watoto wa kiume waliosalia na mwisho

Ø Daraja la Tatu : watoto wa kike ambao hupata kiasi kidogo.

Ø Kwa mujibu wa sheria hii , wajane hawana haki ya kurithi , mjane mwenye watoto sheria inampa haki ya kuishi na kutegemea watoto wake ambao watarithi mali ya marehemu mume wake.

Zingatia:
Ø Watoto wa nje ya ndoa hawaruhusiwi kurithi mali /chochote isipokuwa kama walihalalishwa na marehemu baba yao kufuatana na mila za kabila husika.

Ø Mjane ambaye hana watoto atabaki katika nyumba ya marehemu na kuitumia wakati wa uhai wake , ambapo baada ya kifo chake hugawiwa kwa warithi halali wa mume wake.

3.0. WAJIBU WA MSIMAMIZI WA MIRATHI.
Ø Ndani ya miezi 6 baada ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi , msimamizi anawajibika kutoa orodha na kiasi cha mali alizoacha marehemu, fedha taslimu, madeni pamoja na idadi ya marehemu anaotegemea kuwagawia mali za marehemu.
Ø Kukusanya kwa uaminifu mali za marehemu.
Ø Kuorodhesha madeni yalioachwa na marehemu pamoja na kuyalipa madeni hayo toka kwenye mali alizoacha.
Ø Kulipa gharama za mazishi na gharama za kuendesha mirathi toka kwenye mali za marehemu.
Ø Kugawa mali za marehemu kwa warithi halali kama marehemu atakuwa ameacha wosia msimamizi atagawa kufuatana na wosia aliondika marehemu na kama hakuna wosia atagawa kulinganba na sheria inayotumika kwenye mirtahi9sheria ya kimila, kiislamu, au sheria ya mirtahi ya India.
Ø Kushtaki ambapo marehemu angeshtaki ili kudai haki zake au kujibu mashitaka ya madai pale ambapo kutakuwepo na madai dhidi ya msimamizi.
Ø Kusikiliza maelezo yanayotolewa na mahakama kuhusiana na mirathi anayoendesha.
Ø Kutoa taarifa mahakamani inayoeleza alivyoendesha mirathi na kugawa mali kwa warithi wa marehemu na hatimaye mirathi kufungwa.




WOSIA.
Maana ya Wosia:

Ni tamko au maandishi anayotoa mtu wakati wa uhai wake kueleza jinsi atakavyotaka mwili wake utendewe na mali zake zigawanywe atakapokuwa amefariki.

Umuhimu wa kuandika wosia.

Ø Unaweka mambo yako bayana kuondoa utata kwa familia na jamaa zako.
Ø Unamchagua msimamizi wa mirathi unayemtaka wewe.
Ø Unatoa maelezo juu ya mwili na mali yako kama upendavyo wewe na kwa mujibu wa sheria.


Aina za wosia:-
Ø Wosia wa maandishi.
Ø Wosia wa maneno ya mdomo/matamshi.

Taratibu za kuandika wosia katika sheria za mirathi .

a) Wosia katika Sheria za kimila: Zimo katika jedwali la 3 la sheria iitwayo: The Local Customary Law “(Declaration) No. 4 Order, 1963.
b) Wosia katika sheria za kiserikali.
c) Wosia katika sheria za kiislamu – Mwosia hawezi kuusia mali yake yote. Kisheria anaruhusiwa kuusia 1/3 ya mali yake. 2/3 lazima irithiwe na warithi halali.

Warithi halali ni nani kisheria?

Ø Mke/ mume.
Ø Watoto waliozaliwa ndani ya ndoa.
Ø Watoto waliohalalishwa kisheria.
Ø Wazazi nandugu wa karibu waliokuwa wakimtegemea mtoa wosia wakati wa uhai wake.

Masharti ya uandishi wa Wosia wa maandishi.

Ø Mwosia lazima awe na akili timamu.
Ø Awe ametimiza umri wa miaka 18 na kuendelea.
Ø Uonyeshe tarehe, mwezi na mwaka uliondikwa.
Ø Mwosia ahusiye mali zake binafsi na si za mtu mwingine.
Ø Ushuhudiwe na mashahidi wawili, na kwa yule asiyejua kusoma na kuandika wake lazima wawe wanne na wajue kusoma na kuandika.
Ø Mwosia lazima aweke saini yake, na kama hajui kusoma na kaundika aweke alama ya dole gumba.
Ø Uandikwe kwa kalamu ya wino au kalamu isiyofutika au upigwe chapa.
Ø Mwosia ataje mtu/watu ambao angependa asimamie ugawajki wa mali baada ya kifo chake.





Sifa /masharti ya wosia wa maneno ya mdomo.

Ø Awe mtu ambaye ametimiza umri wa miaka 18 na kuendelea na mwenye akili timamu.
Ø Ushudiwe na mashahidi wasiopungua wanne. Watu wawili kati ya mashahidi hao wawe ni wa ukoo wa mwosia, na wawili wanaweza kuwa watu baki nje ya ukoo wa mwosia.

Kumbuka:

1. Mwosia hawezi kumnyima mrithi wake mali zake isipokuwa tu kama mrithi amefanya mambo yafuatayo :-

Ø Kama amezini na mke na mwosia.
Ø Kama mrithi amejaribu kumuua , kumshambulia , au kumdhuru vibaya mwosia (au kumtendea mama wa mwosia mambo yaliyotajwa )
Ø Mrithi bila sababu na hakumtunza mwosia wakati wa shida na njaa au maradhi.

2. Mtu anaweza kumrithisha rafiki yake vitu au vyombo vyake alivyokuwa akivitumia mwenyewe au sehemu ya mali yake . Lakini fungu la rafiki lisizidi la kila mrithi halali.

3. Wosia ni siri hufichuka wakati mtu aliyeutoa anapokuwa amefariki.

4. Anayeweza kuandika / kutoa wosia wa mdomo ni mtu aliyetimiza umri wa miaka 18 na awe na akili timamu.

Mahali pakutunzia wosia : Benki , kanisani au msikitini , kwa mwanasheria , kwa mtu yeyote ambaye si mrithi katika wosi huo na anaaminika kuwa ana uwezo wa kutuza siri. n.k.


MFANO WA JINSI YA KUANDIKA WOSIA.


  1. Huu ni wosia wangu wa mwisho mimi ………………………………………… wa S.L.P………………………………………………………………………………………


  1. Namchagua ………………………………………………………………………….
wa S.L.P. ……………………………………………………………………………….
Simu………………………………………………………………………………………
ambaye anaishi …………………………………….kuwa msimamizi wa mirathi yangu.


  1. Nitakapokufa mwili wangu ukazikwe……………………………………………..
Wilaya ……………………………………Mkoa……………………………………...


  1. Mali yangu ni:
(a)………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………..

(b) Nina akaunti zifuatazo:…………………………………………………………

………………………………………………………………………………………….

5. Natamka kwmaba mali zangu zote zinazohamishika na zisizohamishika zitamilikiwa
na mke/ mume wangu aitwaye……………………………………iwapo atakuwa hao baadaya kufa kwangu.

6. Iwapo mke/ mume wangu aitwaye ……………………………………..atafariki mapema kuliko mimi , mali zangu zitarithiwa na watoto wangu wafuatao:-

(a)………………………………………………………………………………………….
S.L.P………………………………………………………………………………………
Simu…………………………………………………………………………………………

(b)……………………………………………………………………………………………
S.L.P…………………………………………………………………………………………
Simu………………………………………………………………………………………..


(c)………………………………………………………………………………………….
S.L.P…………………………………………………………………………………………
Simu………………………………………………………………………………………..

(d)……………………………………………………………………………………………
S.L.P………………………………………………………………………………………….
Simu ………………………………………………………………………………………….


Katika mafungu yaliyo sawasawa .

Imetiwa saini hapa………………………………………………………………………….

Siku ya…………………………………………………………………………………………

Mwezi wa……………………………………mwaka………………………………………

Saini ya mwosia………………………………………………………………………………


Shahidi wa Kwanza:

Jina:……………………………………………………………………………………………………….

Saini:………………………………………………………………………………………………………

Anuani:……………………………………………………………………………………………………

Kazi………………………………………………………………………………………………………..






Shahidi wa Pili :

Jina:……………………………………………………………………………………………………….

Saini:………………………………………………………………………………………………………

Anuani:……………………………………………………………………………………………………

Kazi………………………………………………………………………………………………………..

Mbele ya …………………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………………………………...



Mshuhudi viapo/Saini:……………………………………………………………………………………




ANGALIZO: “ Kuandika wosia si uchoro “ , bali ni kujizatiti katika kuhakikisha mambo yako yanakuwa sawa hata usipokuwepo” , ukiwa ni mmojawopo wa wanajamii chukua hatua ya kuandika wosia na uwashawishi wengine kufanya hivyo”


Mwisho.

View attachment mirathi_wosia.doc
 
Nijuavyo mimi kama kuna wosia wa maandishi basi huo huwa haupingwi wala kukiukwa kwa sababu hivyo ndivyo marehemu alivyotaka.

Na mahakama inatakiwa ifuate jinsi ambavyo wosia unasema.

Nimetoka kudili na haya mambo majuzi tu hapa. Hivyo najua walau mawili matatu kuhusiana na haya mambo ya mirathi.
 
Katika mafao ya pensheni kwa sheria ya PSPF mtoto wa nje ya ndoa anahaki kama watoto wengine, natarajia una cheti cha kuzaliwa kinachomtaja babako ni huyo marehemu na mamako anaweza kuthibitisha hivyo
 
Nipe contacts zako (pm) then nitakufahamisha sheria inasemaje kuhusu mtoto wa nje ya ndoa. By the way ilishawahi elezewa humu huko nyuma.
kuna kiapo inaonyesha sipo ila nikija kwenye birth certificate yeye ni my father
 
Sheria as it stands now haimtambui mtoto wa nje ya ndoa. Hivyo birth certificate haina msaada.
Yah ni kweli Sheria haimtambui mtoto wa nje ( illegitimate child) lakini pale panapokua na wosia unaomtaja kurithi mali basi anayo haki juu hizo mali.
 
Yah ni kweli Sheria haimtambui mtoto wa nje ( illegitimate child) lakini pale panapokua na wosia unaomtaja kurithi mali basi anayo haki juu hizo mali.

Pale wosia unapomtaja tu, correct! na sio anampa kama mtoto, bali kama rafiki au mtu baki maana ukiandika neno MTOTO katika wosia, that will be challenged on the locus that mtoto katika tafsiri ya kisheria haimtambui aliyezaliwa nje ya ndoa ( illigitimate child)!. Kwa sasa ndivyo sheria ilivyo.
 
go for DNA taste, then nenda mahakaman udai chako kama mtoto wa marehem. huwezi pata pasu, mtagawana kwa ratio/asilimia.

Baba ameshakufa na hakumtambulisha mtoto halafu leo uje eti kuna DNA test then isema huyu ndiye baba yako! That will be a very contentious case ever on earth. Kumbuka mahakama haiwajibiki kufuata expert evidence under certain circumstances. Mtoto kwa sheria ya sasa hatambulishwi kwa DNA,
 
inategemea na maswala ya dini na kimila mpendwa, kila dini ina taratibu zake na kila ukifuata mila ina taratibu zake haijalishi kama ni mtoto wa halali au si halali.
 

Nyani haya mambo ya mirathi yana technicalities nyingi. kwa mfano kama baba akimnyima mtoto ( a child as defined by law) bila kutoa sababu ya msingi , hiyo wosia hautakubalika. Hivyo matakwa ya wosia yakikiuka sheria inakuwa batili. Lakini kwa case ya muuliza swali, as long as ni bastard, he can not inherit from father's side. Yeye anarithi toka upande wa mama. Asijisumbue kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…