Tetesi: Sheria ya uchaguzi kuwasilishwa Bungeni, Mgombea urais awe ameishi nchini mfululizo miaka miwili ili akidhi sifa ya Urais

Tetesi: Sheria ya uchaguzi kuwasilishwa Bungeni, Mgombea urais awe ameishi nchini mfululizo miaka miwili ili akidhi sifa ya Urais

Habari JF siasa.

Ukishangaa ya Musa utayaona ya Farao/ Firauni.
Sheria mpya ya uchaguzi itawasilishwa bungeni mapema November 2019 au February 2020. Lengo la sheria hii ni kuwabana wagombea urais waghaibu au diaspora ambao wanajipanga kuwania urais.

Sheria hii mpya ya uchaguzi itamtaka Mgombea Urais awe ameishi nchini Tanzania kwa miaka walau miwili mfululuzo hadi kufikia Mwezi August 2020 ili akidhi kigezo cha kupewa Fomu na NEC na hatimaye kugombea urais.

Chanzo changu nyeti serikalini kimeniambia mkakati huu umeiva na nitege sikio Bungeni November 2019 au February 2020.

Mimi nilimkatalia katakata lakini kasimama na msimamo wake.
Nilimuuliza je kama Mtaka urais kasafiri nje ya nchi siku moja au hata wiki mbili ndani ya hiyo miaka miwili itakuwaje?
Alijibu hili halina shida hata kidogo lakini ikiwa ni mwezi au miezi kadhaa basi hapo Mgombea atakosa sifa.

Yangu macho!!
Ya mfamaji tu hayo. Wakati wa mabadiliko ukifika mbinu zote zitakuwa abortive.....
 
Inategemea na definition ya kuishi. Itajumlisha
1. Matibabu?
2Masomo?
Lazima wameweka kipengelr cha kuumwa ndio maana wanasema miaka.miwili.mfululizo.

Lissu we ni nomaa, Lissu umefanya huku tunaishi.maisha magumu sana kisa wanakuogopa wewe. Kila.kinachoamuriwa kukukomoa wewe na sisi tunakomoka wakati hatuhusiki. Hivi kweli Mungu ulimleta Lissu awe chanzo cha mateso yetu??
 
Mimi nashauri wangetunga sheria mtu aliewahi kupigwa risasi zaidi ya kumi na hakufa asigombee.

Maana huyo hatakua binadamu wa kawaida.
Lissu ni kiumbe wa ajabu, bado hana wasi wasi ktk nafsi yake. Hafai.kuwa Rais......hahahaaa
 
Jinsi kura mil 3 unusu alizopata mtu zinavyomuumiza kichwa
Wapii unaambiwa ni laki tisa ndio maana jamaa ana nightmare na trauma hata BAWACHA tu wakiwa na mkutano wa ndani wanatawanywa na mabomu. Just imagine fearing unarmed innocent women gathering inside you send riot police witnh full gears to disperse them.
 
Ya mfamaji tu hayo. Wakati wa mabadiliko ukifika mbinu zote zitakuwa abortive.....
Nyingi zimeshafeli, walidhani kuzuia shughuli za kisiasa kutamshusha lissu au hata kumuua atapotea 100%, Kumnyanganya ubunge pia haijafaa kitu. Wanaone nyota yake inazidi kung'ara tu na uwezekano wa ku impair Magufuli's strength ni mkubwa mno.
 
Wapii unaambiwa ni laki tisa ndio maana jamaa ana nightmare na trauma hata BAWACHA tu wakiwa na mkutano wa ndani wanatawanywa na mabomu. Just imagine fearing unarmed innocent women gathering inside you send riot police witnh full gears to disperse them.
Kumbe jamaa alipata kura ndogo sana aisee, maana sio kwa kuweweseka huku.
 
Sheria huwa haiact kurudi nyuma, itaanza kuwa na effect tarehe na siku hiyo itakaposainiwa kwenda mbele si kwa kurudi nyuma, kwa hiyo wanajisumbua bure
Asante kwa ufafanuzi huu wa kisheria. Nakumbuka ilipopitishwa adhabu ya miaka 30 jela kwa kosa la kubaka. Haikuwagusa wabakaji kabla ya tangazo la sheria mpya.
 
Sheria huwa hairudi nyuma.... hiyo miaka miwili itaanza kuhesabiwa siku ikipitishwa, labda wana target zao? Is it constitutional lakini?
 
Inategemea na definition ya kuishi. Itajumlisha
1. Matibabu?
2Masomo?
Au ziara za kikazi
Au kuhudhuria sherehe za kuapishwa
Au magongamano ya kitaifa
Au kuhani misiba n.k
Umakini unahitajika maana Mchelea mwana .....
 
Wapii unaambiwa ni laki tisa ndio maana jamaa ana nightmare na trauma hata BAWACHA tu wakiwa na mkutano wa ndani wanatawanywa na mabomu. Just imagine fearing unarmed innocent women gathering inside you send riot police witnh full gears to disperse them.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Back
Top Bottom