Sheria za kufungua Baa, nyumba za Ibada ziangaliwe upya

Sheria za kufungua Baa, nyumba za Ibada ziangaliwe upya

Mpiga Paspoti

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2022
Posts
309
Reaction score
1,273
Habari JF?

Siku hizi kumeibuka wimbi la kufungua Baa/ groceries na nyumba za ibada katikati ya makazi ya watu! Mwisho wa siku, zinageuka kuwa kero kwa kufungua sauti kubwa kwa wananchi wanaozizunguka ambao kimsingi hizi bar au nyumba za ibada zimewakuta hawa wanachi!

Mfano mzuri, ninapoishi nimefanya ujezi wa hii nyumba miaka tisa iliyopita, hakukuwa na bar wala nyumba ya ibada katika eneo hili na mtaa ulikuwa ni tulivu sana.

Hivi karibuni kuna bar imefunguliwa, walinunua nyumba ikavunjwa na kujengwa bar. Mie ni jirani wa pili kutoka ilipo. Jamani....!! Natamani niuze nyumba nihame tu! Kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa kumi alfajiri wao wanafungulia muziki kwa sauti ya juu kabisa! Ni kero! Ni kero haswa!! Watoto mpaka wamekonda, hawana muda wa kupumzika!! Nikiwa ndani mwangu hata simu siwezi kupokea!

Papo hapo kuna nyumba ya sita kutoka nilipo kwa upande wa pili! Jirani kafungua kanisa ambalo usiku kucha nalo wanaweka CD ya maombi kwa sauti ya juu kabisa!! Hatuna pa kupumulia!!

Mamlaka husika hebu muangalie umuhimu wa kudhibiti na kuweka sheria kali kwenye ufunguzi wa hizi huduma na biashara katikati ya makazi ya watu! Zimekuwa kero kubwa kwa sasa!
 
Kelele za sauti kutoka kwenye mabaa na makanisa hususani ya walokole ni kero kwa wengi si wewe tu. Ila mamlaka husika wanaona na kufumbia macho.

Wanasubiri litokee jambo la uvunjifu wa amani ndio wajitokeze wakijibaraghuza kutaka kuchukua hatua, lakini kwa hali inavyoenda ipo siku balaa kubwa litatokea na kutia aibu hususani kutoka kwa haya makanisa ya kiroho.​
 
Mimi ninaishi na wapangaji ni KERO haswaa
Nimeshazungumza nimechoka khs makelele ya Muzik lkn wapi
Nyumbani kwangu pamekua pachungu huwezi ukasema ni sehemu ya kupumzika nimeamua kunyamaza nasubiri Kodi imalizike nisepe
Maana inanilazimu niondoke asubuhi mapema sana nakurudi usiku sana hata siku za mapumziko
Pia na jirani hapa Kuna makanisa mawili unaweza kudhani wanashindana kuongeza sauti hasa nyakati za usiku,
NB-na hapa nimekosa usingizi nimeamua niingie JF nakutana na hii thread kwakweli Sina hamu huwa naomba umeme ukatike lkn tatizo wanatumia Solar wengine Jenereta tabu tupu
 
Mimi ninaishi na wapangaji ni KERO haswaa
Nimeshazungumza nimechoka khs makelele ya Muzik lkn wapi
Nyumbani kwangu pamekua pachungu huwezi ukasema ni sehemu ya kupumzika nimeamua kunyamaza nasubiri Kodi imalizike nisepe
Maana inanilazimu niondoke asubuhi mapema sana nakurudi usiku sana hata siku za mapumziko
Pia na jirani hapa Kuna makanisa mawili unaweza kudhani wanashindana kuongeza sauti hasa nyakati za usiku,
NB-na hapa nimekosa usingizi nimeamua niingie JF nakutana na hii thread kwakweli Sina hamu huwa naomba umeme ukatike lkn tatizo wanatumia Solar wengine Jenereta tabu tupu
Mkuu pole Sana Ila wachawi maeneo hayo awasumbui
 
Kelele za sauti kutoka kwenye mabaa na makanisa hususani ya walokole ni kero kwa wengi ila wewe tu. Ila mamlaka husika wanaona na kufumbia macho.

Wanasubiri litokee jambo la uvunjifu wa amani ndio wajitokeze wakijibaraghuza kutaka kuchukua hatua, lakini kwa hali inavyoenda ipo siku balaa kubwa litatokea na kutia aibu hususani kutoka kwa haya makanisa ya kiroho.​

Ndiyo maana naona dawa ni kuwa na sheria kali kwa shughuli na biashara zote zinazohusiana na kutumia sauti kubwa!!

Inafika wakati asubuhi kuamka kwenda kazini huwezi mwili umechoka kweli kweli!!
 
Kawe na udogo wake kuna makanisa si chini ya arobaini ukibisha nakuhesabia moja baada ya lingine na bado ikifika jumapili shule ya msingi kawe A baadhi ya madarasa yanageuzwa makanisa.. Kimbembe kipo kwenye kugombea wateja (waumini)

Hili ni balaa, wakazi wa Kawe moja kwa moja mbinguni!!😃
 
Mimi ninaishi na wapangaji ni KERO haswaa
Nimeshazungumza nimechoka khs makelele ya Muzik lkn wapi
Nyumbani kwangu pamekua pachungu huwezi ukasema ni sehemu ya kupumzika nimeamua kunyamaza nasubiri Kodi imalizike nisepe
Maana inanilazimu niondoke asubuhi mapema sana nakurudi usiku sana hata siku za mapumziko
Pia na jirani hapa Kuna makanisa mawili unaweza kudhani wanashindana kuongeza sauti hasa nyakati za usiku,
NB-na hapa nimekosa usingizi nimeamua niingie JF nakutana na hii thread kwakweli Sina hamu huwa naomba umeme ukatike lkn tatizo wanatumia Solar wengine Jenereta tabu tupu

Nami ingekuwa nimepanga, kitambo sana nishahama! Nimetafuta eneo nje ya jiji kabisa niwe nakwenda kupumzika weekend!!

Shida ni ile ile pakishaanza kuchangamka, utashangaa bar au nyumba ya ibada inakuja kufunguliwa jirani na kero ishakufuata.

Sheria kali kali kama wenzetu wa Delhi huko India, jiji kubwa na limebanana kuliko letu lakini hakuna kelele iwe mchana au usiku!

Nyumba za ibada zina eneo maalum!!
 
Habari JF?

Siku hizi kumeibuka wimbi la kufungua Baa/ groceries na nyumba za ibada katikati ya makazi ya watu! Mwisho wa siku, zinageuka kuwa kero kwa kufungua sauti kubwa kwa wananchi wanaozizunguka ambao kimsingi hizi bar au nyumba za ibada zimewakuta hawa wanachi!

Mfano mzuri, ninapoishi nimefanya ujezi wa hii nyumba miaka tisa iliyopita, hakukuwa na bar wala nyumba ya ibada katika eneo hili na mtaa ulikuwa ni tulivu sana.

Hivi karibuni kuna bar imefunguliwa, walinunua nyumba ikavunjwa na kujengwa bar. Mie ni jirani wa pili kutoka ilipo. Jamani....!! Natamani niuze nyumba nihame tu! Kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa kumi alfajiri wao wanafungulia muziki kwa sauti ya juu kabisa! Ni kero! Ni kero haswa!! Watoto mpaka wamekonda, hawana muda wa kupumzika!! Nikiwa ndani mwangu hata simu siwezi kupokea!

Papo hapo kuna nyumba ya sita kutoka nilipo kwa upande wa pili! Jirani kafungua kanisa ambalo usiku kucha nalo wanaweka CD ya maombi kwa sauti ya juu kabisa!! Hatuna pa kupumulia!!

Mamlaka husika hebu muangalie umuhimu wa kudhibiti na kuweka sheria kali kwenye ufunguzi wa hizi huduma na biashara katikati ya makazi ya watu! Zimekuwa kero kubwa kwa sasa!
Hairuhusiwi kufungua baa kwenye makazi hadi kuwe na kibali au wakazi wenyewe mridhie pasina shaka kisheria baada ya eneo kubadilishwa matumizi ya awali.
 
Hairuhusiwi kufungua baa kwenye makazi hadi kuwe na kibali au wakazi wenyewe mridhie pasina shaka kisheria baada ya eneo kubadilishwa matumizi ya awali.

Sidhani kama hii sheria inafuatwa bar zinajiotea tu!! Ngoja nianze ufuatiliaji kama waliwahi kutuhoji na kubadilisha matumizi ya hilo eneo!!
 
Sidhani kama hii sheria inafuatwa bar zinajiotea tu!! Ngoja nianze ufuatiliaji kama waliwahi kutuhoji na kubadilisha matumizi ya hilo eneo!!
Anzisha vagi la maneno hadi kieleweke.Haiwezekani mjasiriamali mmoja atoke alipotoka na kufungua kanisa au baa ili afanye fujo tu.Ubinadamu ni kuheshimiana,kujaliana na kutii sheria.Binadamu si hayawani kwamba anajiamulia kufanya jambo bila utaratibu.Rules are rules.Without rules,we are all savages!
 
Watu wa mipango miji wao wanachojua ni kusubiri mishahara,semina,warsha,hafla na tafrija lakini suala la kufuatilia mambo ya ujenzi mtaani hawataki wakati ramani za mitaa wanazo. Kiukweli nyumba za ibada zinatakiwa zitengewe maeneo yake maalumu na ibada inahitaji utulivu,sasa unakuta mtaa una makelele ya bodaboda,baa,sherehe,yaani kero tupu. Pia sehemu za starehe zinatakiwa nazo zitengewe maeneo maalumu. Lakini haya yote yanasababishwa na wabunge na madiwani wao kwa kutowasimamia ipasavyo watendaji wa Serikali. Mwisho,siku hizi kuna SOUND PROOF kwa nini watu wasifunge ili kuzuia kelele kutoka nje..Naupongeza sana msikiti wa Taqwa Ilala Bungoni pamoja na ule wa pale karibu na Uwanja wa Uhuru,wao utasikia adhana tu kisha mambo mengine yanasikika ndani ya nyumba ya ibada tu nje huku husikii vile vipaza sauti..
 
Habari JF?

Siku hizi kumeibuka wimbi la kufungua Baa/ groceries na nyumba za ibada katikati ya makazi ya watu! Mwisho wa siku, zinageuka kuwa kero kwa kufungua sauti kubwa kwa wananchi wanaozizunguka ambao kimsingi hizi bar au nyumba za ibada zimewakuta hawa wanachi!

Mfano mzuri, ninapoishi nimefanya ujezi wa hii nyumba miaka tisa iliyopita, hakukuwa na bar wala nyumba ya ibada katika eneo hili na mtaa ulikuwa ni tulivu sana.

Hivi karibuni kuna bar imefunguliwa, walinunua nyumba ikavunjwa na kujengwa bar. Mie ni jirani wa pili kutoka ilipo. Jamani....!! Natamani niuze nyumba nihame tu! Kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa kumi alfajiri wao wanafungulia muziki kwa sauti ya juu kabisa! Ni kero! Ni kero haswa!! Watoto mpaka wamekonda, hawana muda wa kupumzika!! Nikiwa ndani mwangu hata simu siwezi kupokea!

Papo hapo kuna nyumba ya sita kutoka nilipo kwa upande wa pili! Jirani kafungua kanisa ambalo usiku kucha nalo wanaweka CD ya maombi kwa sauti ya juu kabisa!! Hatuna pa kupumulia!!

Mamlaka husika hebu muangalie umuhimu wa kudhibiti na kuweka sheria kali kwenye ufunguzi wa hizi huduma na biashara katikati ya makazi ya watu! Zimekuwa kero kubwa kwa sasa!
baa usifananishe na kanisa. umetukosea sana wanywaji
 
Back
Top Bottom