Sheria zinatungwa na Mungu tumeumbwa kuzifata, Wakristo tukemee viongozi wanaoridhiana na LGBTQ bila kujali ukubwa wao, Mungu habadilishiwi sheria

Sheria zinatungwa na Mungu tumeumbwa kuzifata, Wakristo tukemee viongozi wanaoridhiana na LGBTQ bila kujali ukubwa wao, Mungu habadilishiwi sheria

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
LGBTQ = UPINDE

Hakuna tatizo pale mtu anaridhiana ama kusapoti lgbtq akiwa yeye kama yeye ama akiwa anatumia sheria za serikali lakini suala la mtu kujivika ukristo kwenye kufanya maridhiano ama kusapoti na hata kuhalalisha lgbtq hio haikubaliki hata kidogo.

Nashangaa kuliona kanisa kubwa leo hii viongozi wake wakiwa wanakaa meza moja kuwapa moyo, kuwapa matumaini, kufanya maridhiano na kwa baadhi yao wamefikia hadi steji ya kuhalalisha Lgbtq kwamba ni sawa Hii haikubaliki kabisa, Panya ukimpa maziwa atahitaji siagi na vingine, Yalianza mambo ya kuwasikiliza leo hii tulipo hawa lgbtq wanapaziwa sauti na viongozi kwamba wakaribishwe makanisani na hata kufungishwa ndoa makanisani !!

Kinachofanyika ni kwamba Mamlaka ya Mungu yanaanza kubadilishwa yaendane na wanachotaka watu flani, kama leo hii kanisa linaona ndoa ya mwanaume kwa mwanaume ama mwanamke kwa mwanamke ni sawa, Je ni kipi kinawazuia kuhalalisha ndoa ya mbwa na mwanamke / mwanaume ?

Mungu pekee ndie anaetengeneza sheria, Hata tunapoenda makanisani ni sisi ambao tumeenda kujikumbusha kubadilika ili tuweze kuwa katika vigezo anavyovitaka Mungu na sio sisi kumbadili Mungu akidhi vigezo tunavyotaka.

Hapo mwezi uliopita niliona kiongozi wa kanisa kubwa tu anawapigia debe lgbtq kwamba eti wakaribishwe makanisani, Nikiri sina tatizo kwa hawa watu kushiriki lakini tatizo lilipo ni kwamba watashiriki vipi kanisani huku wakiendelea kufanya ufuska wao na kuona kwamba hakuna shida yoyote ?

Kanisa lipo wazi kwa watenda dhambi wote kuanzia malaya, wezi, wazinzi, n.k. Kanisa lipo kwajili ya kuwasafisha kwa kutoa mafundisho ya, kukemea dhambi, n.k. lakini sio kuwahamasisha kundi flani la watenda dhambi kwamba ni sawa wanachotenda.

Ieleweke kwamba ukweli mchungu kwa wapenda dhambi ni kwamba ufalme wa Mungu ni lazima wauone una Ubaguzi nae pia Mungu ni mbaguzi kwa watu wasiozifata sheria zake, Kashaweka sheria zake endapo unataka umuabudu na kuwa sehemu ya ufalme wake. Kwa lugha nyepesi kabisa ni kwamba Ufalme wa Mungu sio kwa kila mtu, ni kwa wale tu wenye nia ya kufanya anachotaka na sio wao kufanya wanachotaka kwa kuzirekebisha Sheria zake. Ni jukumu la kila mkristo kutubu dhambi zake, kuzijutia, kuzigeuka kwa kuziacha na kufata njia impendezayo Mungu,

Kinachomchukiza Mungu ni dhambi na sio mtu alietenda maana sisi wote ni watoto wake tulioumbwa katika mfano wake na ndio maana huruma yake huwa ni kubwa sana kwetu kiasi cha kuwa tayari kutusamehe Lakini kwa sharti kwamba tuzifate sheria zake zinazotukemea dhambi ambazo alishaziorodhesha ikiwemo ushoga na usagaji, hata kanisani wanaotenda dhambi wanakaribishwa lakini hujutia dhambi walizofanya na kutambua kwamba wamemkosea Mungu, hivyo kuwashirikisha lgbtq sio shida lakini wao kuendelea na dhambi wakiona ni sawa ndipo penye tatizo linalowafanya wabaguliwe.

Niwaombe wakristo na hasa viongozi wasiwe mbwa mwitu walivaa vinyago vya kondoo kuwapeleka kondoo wao mahali siko, wasiwe walimu wa mchongo ambao biblia imeshatuonya, kumbukkeni wajibu wenu wa kulinda imani, acheni kufundisha mambo ya usawa ama kuwashirikisha watu wanaofanya dhambi bila kuwa na nia ya kubadilika na kutambua wanachofanya hakimpendezi Mungu.
 
Kujaribu kuonekana ni mwema badala ya kuwa mwema ni mzigo
 
Wakristo ni mizinguo sana aisee, sijui wanatumia kitabu gani kuhalalisha huo ufuska.
Hakuna kitabu kinahalalisha bali viongozi wa makanisa fulani wameanza kudhani kwamba wapo kwenye bodi ya watunga sheria za Mungu
 
Iko hivi mleta maada, nakuonea huruma sana, Kanisa halijaanza leo kubadili au kuingiza mambo yasiyofaa katika Dini, Sema mmefichwa mambo mengi katika historia. Baada ya miaka 300 ya kuondoka Yesu, ndiyo vilianza kuingizwa vitu chungu nzima, kama Yesu ni Mungu, Utatu mtakatifu na mambo chungu nzima.

Na hiyo ilitokana na utashi wa Viongozi wa kipindi hicho, bali siyo amri ya Mwenyezi Mungu. Kumbuka haya ya Ushoga baada ya miaka 300 ijayo, watu watakuja kuambiwa siyo dhambi, maana hilo siyo geni kwa kanisa, bali ni utamaduni wao toka zamani, ila ulikuwq umejificha.

Hivi inawezekana Mapadri wanaume wazima wenye afya njema ambao hawane wake, wakaishi nyumba moja?Tena wakati mwingine wanakunywa pombe na wanalewa? Au wanawake Masistar ambao wanakaa nyumba ambao hawana wanaume unategemea wataishije?

Au katika kipindi hiki cha Ushoga, uko tayali kumpeleka mwanao wa kiume akalelewe na Padri ambaye hana mke?

Mimi naona haya mambo yameanzia vyumbani mwao wenyewe
 
Sasa jiulize,hivi utaenda kwenye Dini na nyumba ya Ibada inayoruhusu Ushoga,na yawezekana na Viongozi wake wakawa mashoga,Au utaende kwenye Dini na nyumba inayokataza Ushoga,na ikatamka kwa kinywa mashoga wauwawe.

Inamaana kasoma hujui,hata picha tu unashindwa kuitambua maana yake nini?
 
Kwa maelezo ya papa kwamba sio kosa ni dhambi ,na kwamaazimio ya Anglikana pale London mungu kijinsia haeleweki. Kwakweli Dunia imefeli pahala. Lea familia Yako Kwa uangalifu, kwa haya yanatuonesha TAIFA la marekani ni mpango wa Dunia na sio marekani pekee
 
Hivi inawezekana Mapadri wanaume wazima wenye afya njema ambao hawane wake, wakaishi nyumba moja?Tena wakati mwingine wanakunywa pombe na wanalewa?Au wanawake Masistar ambao wanakaa nyumba ambao hawana wanaume unategemea wataishije?

Au katika kipindi hiki cha Ushoga, uko tayali kumpeleka mwanao wa kiume akalelewe na Padri ambaye hana mke?
Duuh! Maswali magumu na fikirishi sana haya. Ushoga unaweza kuwa umeanzia kwa hawa watawa na magerezani.
 
Wewe huna/ hutendi dhambi, na je huendi nyumba za ibada? Jibu lako ni muhimu!
 
Na walivyokua wapumbavu wakaamua watumie upinde wa mvua ambao kwenye biblia kitabu cha mwanzo kwenye habari za nuhu Mungu alimwambia nuhu ataweka upinde kama ishara ya maagano kwamba hata angamiza tena Dunia kwa garika, alafu wenyewe wame uchukua kujitambulisha washenzi kabisa hao wauwae mbwa hao
 
Wenzetu wamepewa uwezo mkubwa katika Dini yao kuongeza au kupunguza mambo ya Mwenyezi Mungu.Chukulua mfano huko nyuma kanisa katoliki lilikuwa linaungamisha dhambi kwa pesa, Yaani wewe tenda dhambi zako, unampa kiongozi wa Dini pesa, anakusamehe dhambi zake.

Ikafikia mda unaweza kusamehewa hata zile utakazofanya kwa mwaka mzima, unachotakiwa kufanya ni kutoa pesa tu, kwa hiyo wewe kalawiti,kaibe, uwa, kwani ulishasamehewa,

Ingawa huo utaratibu walishauto, imebaki kuungamisha.

Uisilamu sheria zilizowekwa sasa hivi zinatimiza karne 14, zinaenda karne ya 15, Funga ni ileile, Swala ni zilezile, zaka ni zilezile, na hata kuowa ni kulekule na mengineyo
 
Back
Top Bottom